BIG RESULTS NOW: Tanzania iache kukopi wasiyoweza kupest

BIG RESULTS NOW: Tanzania iache kukopi wasiyoweza kupest

KALOKAGATHOS

Member
Joined
Jul 9, 2013
Posts
38
Reaction score
6
Sera ya waziri mkuu wa Malaysia ilikuwa nzuri hususan katika mandhari ya Malaysia,mpaka kufikia anatangaza mpango wake huo wa kuikomboa nchi yake kimaendeleo,utafiti umefanywa wa kutosha,jopo la wataalam lilikaa likatafakari kwa kina na kwa wakati,likaona mapungufu,likatoa mapendekezo,sasa ni utekelezaji.Lakini huku Bongo kama ilivyo ada,kupakua na kupakia,wameibeba sera hii na kuibandika katika mazingira hatarishi kana kwamba Tanzania ya leo imekuwa Malaysia.Hata kama wote tulitawaliwa na Malkia,ndo kusema wote tunafanana?,kiuchumi hatuendani,viwango wa rushwa hatulingani,tena hapo tumewapiga gepu kubwa sana,unajua Malaysia kuja kuifikia Tanzania kwa viwango vya ufisadi ni baadae sana,labda miaka 200 ijayo,huku kodi za walala hoi ni vocha za mafisadi tena za kuongea na mahawara zao,sasa maendeleo yatatoka wapi?..Au mnadhani kuona majengo mengi ya Dar ndo ishara ya maendeleo? vipi kuhusu maisha ya mtu mmoja mmoja?,waingereza wanaita "per capita income"...hebu linganisha na ya Malaysia halafu uniambie BRN.
 
copying good things si shida... ila unaonyesha hujaelewa concept ya BRN wala nini

take time to learn about it
 
copying good things si shida... ila unaonyesha hujaelewa concept ya BRN wala nini

take time to learn about it

Bora ukasome kwanza wewe mwenyewe ndo uje ucomment,unadhani hayo nimeyaokota? Au nimekugusa? We fisadi au?
 
Mkuu KALOKAGATHOS Kinacho tuangusha ni CCM na viongozi wake dhaifu..

Huwezi kuilinganisha hata na Kenya..Malaysia mbali sana mkuu..

Kwanza hawana walilojifunza kutoka Malaysia...Wata-enjoy muda gani?

Totoz,shopping..nk ndio vinavyo wapeleka nje..
 
Last edited by a moderator:
Hayo ndo maneno kijana,TOTOZ,SHOPING,GIFTS ndo zinawakimbiza viongozi wa TZ huko nje,hawana uwezo wa kubuni mambo yanayoendana na uzito wa nchi yao!,kuiga mpaka lini? Wanaharakati mnasemaje?,tuendelee kuiga au tutengeneze yetu? kwani madhara ya Ujamaa yakoje? kila kitu tuliiga kwa wachina,tukawa masikini,sasa tena kwa Malaysia,tunatarajia nini?
 
BRN wameintroduce bila kushirikisha wadau, kitu kingine BRN imeletwa na watu waliochokwa ndio maana hata waseme nn wanaonekana hawana jipya hivyo kukosa ushirikiano.

Watu hawana imani na waleta sera.
 
Back
Top Bottom