Bikira Maria wa Mlima Kilimanjaro !

Bikira Maria wa Mlima Kilimanjaro !

Ligogoma

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2010
Posts
3,503
Reaction score
6,415
Habari wana JF?

Wiki moja iliyopita nilikuwa Moshi, nilikutana na mama amabaye alikuwa jirani yetu miaka ya 80 hadi 90 mwishoni, tulipiga sana story na akanikumbusha tukio la kuonekana Bikira Maria (Mama wa Yesu) kwenye mlima Kilimanjaro mwaka 90.

Kilichomfanya akumbuke ni kwamba mimi binafsi sikuwahi kumuona huyo Bikira Maria hapo mlimani kwa macho yangu ingawa nilikuwa naangalia kwa bidii zote, huyu mama alikuwa anamuona pamoja na wengine wengi wakati huo na hivyo akasema asiyemuona Bikira Maria basi ana dhambi na atakufa soon.

Nililia sana siku hiyo na siku kadhaa za tukio hilo maana wenzangu wote walikuwa wanamuona ila mie mpaka habari hizo zinaisha sikuwahi kumuona hata siku moja. Kwa hali hii nikajikuta nakumbuka tukio hili kubwa la kihistoria liliowahi kutokea Moshi na inaonekana limesahaulika kabisaa katika jamii yetu

Lilikuwa ni tukio lilifanya mji wa Moshi kuzizima na macho ya wakazi wake kuelekea Mlima Kilimanjaro kumuangalia Bikira Maria, wapo wanaodai walimuona na wengine kama mimi hatukumuona.

Walowahi kumuona wanadai (akiwepo huyu mama) walimuona mama wa Kizungu kajitanda kama jinsi picha za Virgin Mary zinavyokuwa na alikuwa anaonekana kama anafanya maombi vile. Pia kuna siku nyingine alikuwa anaonekana kichwa tu kwenye barafu za kilele cha mlima na alikuwa akigeuka huku na huko (hafanyi maombi).

Humu tumo wengi na naamini wakati wa tukio hili kuna watu humu wanaweza kuwa walikuwepo, walishuhudia au walisikia chochote kutokana na tukio hilo la wakati huo.

Hebu tukumbushane hili tukio na mwisho wake ilikuwa ni nini hasa?? Maana mie binafsi nilikuwa bado kijana mdogo na sikumbuki liliishia wapi.

Nawasilisha
 
ahh hizo zilikuwaga tuu swaga....za wazee na watu wa mlimani...Walimuona mzungu wa hivyo wakadai ni bikira maria......

Wao hata walikuwa wakimuona mzungu mwanaume mwenye nywele ndefu utasikia ni yesu..
 
ahh hizo zilikuwaga tuu swaga....za wazee na watu wa mlimani...Walimuona mzungu wa hivyo wakadai ni bikira maria......

Wao hata walikuwa wakimuona mzungu mwanaume mwenye nywele ndefu utasikia ni yesu..

Binadamu wa kawaida akiwa kule mlimani na wewe ukiwa mjini huwezi kumuona kwa macho ya kawaida kamwe!! Ila yule alikuwa anaonekana toka mlimani kule kwenye ice bila kifaa chochote, I wish hili saga lingejirudia enzi hizi za mitandao hahahaaa
 
umenikumbusha kuna mzee kule kenya anajiita jehova mungu wanyonyi!
 
Ha ha ha mkiambiwa nanyi mjiambie maryam bint imran yani mamayake isaa alahi salam hakuna mzungu na yeye ashakufa Leo aonekani mfu hufufuka ?
 
Kilichomfanya akumbuke ni kwamba mimi binafsi sikuwahi kumuona huyo Bikira Maria hapo mlimani kwa macho yangu ingawa nilikuwa naangalia kwa bidii zote, huyu mama alikuwa anamuona pamoja na wengine wengi wakati huo na hivyo akasema asiyemuona Bikira Maria basi ana dhambi na atakufa soon.

Kama kweli hukumuona mbona hukufa 'soon'?

Je hao wote waliomuona (wasio na dhambi) hawakufa 'soon'?

Hivi mantiki ya kumuona bikira Maria ni kuletewa ujumbe kuwa huna dhambi?
 
Kama kweli hukumuona mbona hukufa 'soon'?

Je hao wote waliomuona (wasio na dhambi) hawakufa 'soon'?

Hivi mantiki ya kumuona bikira Maria ni kuletewa ujumbe kuwa huna dhambi?

Wakati huo nilikuwa mdogo kiasi cha kuamini yanenwayo na wakubwa na kwa maadili ya kipindi hicho nahisi ilikuwa ni sahihi kwangu. Niliamini hilo kwa sababu mbili, umri mdogo na yaliyonenwa wakati wa tukio hilo ndugu yangu.

Hiyo dhana ya kuwa msafi ndo uwaone ' watakatifu wa Mungu' tumejengewa toka tangu na tangu!! Refer maandoko tuliyopewa yanasema wazi waliokuwa wanapata nafasi ya kuonana au kuongea na Mungu ni wale wasafi tu kina Ibrahimu, Mussa, Yesu, Mtume Mohammed etc.
 
Kama huyo bibi alikuambia hivyo eiether alisahahu au aliamua kukudanganya tu

Nyakati hizo anaedaiwa kuwa Bikira maria hakuonekana kwenye mlima Kilimanjaro bali alionekana Kibosho kwa kijana mmoja hivi na watu walikuwa wanakwenda huko sana kwaajili ya maombi

Nilikuwa Moshi wakati huo na nilikuwa nasoma hivyo hili tukio nalikumbuka vizuri sana

Pia hakukuwa na suala la kumuona na kufa mapema hizo ni hadithi tu,ni kama nyakati hizo kulikuwa na story za kidudumtu,nadhani kama utakuwa na umri wa kutosha kidogo utakumbuka hili sakata ambalo liliwafanya watu kutokula mboga za majani kwani ilisemekana kama ukila na ukamla kididimtu basi utakufa

Sikumbuki kama hilo lilithibitishwa na wizara ya afya chini ya Rais Ali Hassani Mwinyi!
 
Loh!

Hebu tusubir. Naamini watapatikana mashuhuda watusaidie ktk hili. Naikubali JF!
 
Wakati huo nilikuwa mdogo kiasi cha kuamini yanenwayo na wakubwa na kwa maadili ya kipindi hicho nahisi ilikuwa ni sahihi kwangu. Niliamini hilo kwa sababu mbili, umri mdogo na yaliyonenwa wakati wa tukio hilo ndugu yangu.

Hiyo dhana ya kuwa msafi ndo uwaone ' watakatifu wa Mungu' tumejengewa toka tangu na tangu!! Refer maandoko tuliyopewa yanasema wazi waliokuwa wanapata nafasi ya kuonana au kuongea na Mungu ni wale wasafi tu kina Ibrahimu, Mussa, Yesu, Mtume Mohammed etc.

Hakuna hata swali moja ulilojibu kati ya niliyokuuliza...

Katika mada yako kuu umeandika nadharia ambazo hazijathibitika na umeshindwa kuzitetea...

1. Ambaye hakumuona bikira Maria iliaminika atakufa soon

- Je wewe uliyeshindwa kumuona mbona ungali hai hata sasa?

- Je hao wengine wote ambao walimuona huyo bikira Maria ni kwa kuwa hawakuwa na dhambi?
 
Kama huyo bibi alikuambia hivyo eiether alisahahu au aliamua kukudanganya tu

Nyakati hizo anaedaiwa kuwa Bikira maria hakuonekana kwenye mlima Kilimanjaro bali alionekana Kibosho. kwa kijana mmoja hivi na watu walikuwa wanakwenda huko sana kwaajili ya maombi

Nilikuwa Moshi wakati huo na nilikuwa nasoma hivyo hili tukio nalikumbuka vizuri sana

Pia hakukuwa na suala la kumuona na kufa mapema hizo ni hadithi tu,ni kama nyakati hizo kulikuwa na story za kidudumtu,nadhani kama utakuwa na umri wa kutosha kidogo utakumbuka hili sakata ambalo liliwafanya watu kutokula mboga za majani kwani ilisemekana kama ukila na ukamla kididimtu basi utakufa

Sikumbuki kama hilo lilithibitishwa na wizara ya afya chini ya Rais Ali Hassani Mwinyi!
Tya bikira Maria nakumbuka nilikua majengo moshi pale watu walikusanyana kuangalia mlima kilimanjaro...binafsi inina tabia ya kupuuzia baadhi ya mambo ingawa nilikua mdogo lakin sikujishughulisha kwenda kushangaa
Ya kidudumtu nilikua interested kumuona so kila wakinunua mboga za majani nilikua sichez mbali ili nimuone
 
Sio hayo tu. Kuna kidudu mtu, vibwengo, popobawa, babu wa loliondo, sheikh yahaya, na wengineo.

Stori hizi huvuma sana kipindi chenye utata kisiasa au kiuchumi Tz.

Mara zote huishia kuwa ulaghai wa walio madarakani kupumbaza wananchi wasiuone uhalisia wa mambo nchini.
 
Wakipita CCMscrow uchaguzi mkuu, subiri ajabu lingine tokea Tz mida ya Feb/Machi mwakani. Labda upinzani ukubali matokeo moja kwa moja.

Usishangae mchungwajima au mzee wa upako/transfoma 'akapalizwa' Mbinguni.
 
Ha ha ha mkiambiwa nanyi mjiambie maryam bint imran yani mamayake isaa alahi salam hakuna mzungu na yeye ashakufa Leo aonekani mfu hufufuka ?

Mkuu mbona ushàanza kuleta habar nyingine.....?
 
Habari wana JF?

Wiki moja iliyopita nilikuwa Moshi, nilikutana na mama amabaye alikuwa jirani yetu miaka ya 80 hadi 90 mwishoni, tulipiga sana story na akanikumbusha tukio la kuonekana Bikira Maria (Mama wa Yesu) kwenye mlima Kilimanjaro mwaka 90.

Kilichomfanya akumbuke ni kwamba mimi binafsi sikuwahi kumuona huyo Bikira Maria hapo mlimani kwa macho yangu ingawa nilikuwa naangalia kwa bidii zote, huyu mama alikuwa anamuona pamoja na wengine wengi wakati huo na hivyo akasema asiyemuona Bikira Maria basi ana dhambi na atakufa soon.

Nililia sana siku hiyo na siku kadhaa za tukio hilo maana wenzangu wote walikuwa wanamuona ila mie mpaka habari hizo zinaisha sikuwahi kumuona hata siku moja. Kwa hali hii nikajikuta nakumbuka tukio hili kubwa la kihistoria liliowahi kutokea Moshi na inaonekana limesahaulika kabisaa katika jamii yetu

Lilikuwa ni tukio lilifanya mji wa Moshi kuzizima na macho ya wakazi wake kuelekea Mlima Kilimanjaro kumuangalia Bikira Maria, wapo wanaodai walimuona na wengine kama mimi hatukumuona.

Walowahi kumuona wanadai (akiwepo huyu mama) walimuona mama wa Kizungu kajitanda kama jinsi picha za Virgin Mary zinavyokuwa na alikuwa anaonekana kama anafanya maombi vile. Pia kuna siku nyingine alikuwa anaonekana kichwa tu kwenye barafu za kilele cha mlima na alikuwa akigeuka huku na huko (hafanyi maombi).

Humu tumo wengi na naamini wakati wa tukio hili kuna watu humu wanaweza kuwa walikuwepo, walishuhudia au walisikia chochote kutokana na tukio hilo la wakati huo.

Hebu tukumbushane hili tukio na mwisho wake ilikuwa ni nini hasa?? Maana mie binafsi nilikuwa bado kijana mdogo na sikumbuki liliishia wapi.

Nawasilisha
Chuki zimekujaa sana wewe. Mambo ya miaka ya 80 inakupa faida gani leo?
 
Back
Top Bottom