Bila kufuta kesi ya Mbowe, Siri za Serikali na Mambo ya ulinzi yanatufikia Raia hata tusiojua kusoma alama za nyakati

Ipo siku akina Mahita,Kingai na genge lao watafungwa jela maana Wana jinai nyingi .Nimesema hivo na itatokea kweli waache wafurahi lakini kwa utawala ujao watakua na Hali ngumu sana .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Isifutwe ili nasi tuzijue hizo siri za SERIKALI
 
Bila kesi hii kufutwa, kuna majina yanatajwa sana sana hadi sisi mangumbalu tunahisi ndio wale wasiojulikana na sasa wanajulikana, Kuna Polisi wanahusishwa na utesaji mikoa tofauti na kauli za kupotezana
Isifutwe ili nasi tuzijue hizo siri za SERIKALI na magaidi kwa ujumla wake
 
Hiyo si ndiyo vizuri, ambavyo miaka yote mnataka wasiojulikana wajulikane! Kwahiyo kesi ya Mbowe isifutwe ili kila kitu kijulikane.
Hawa jamaa wanatumia mitandao ya kijamii kuishinikiza mahakama itende watakavyo,wanajua Makengeza hachomoki huu msala
 
Acha kesi uendelee haki itendeke,fahamu kupata haki stahiki ina gharama zake,usihofu kuhusu gharama
 
Bila kesi hii kufutwa, kuna majina yanatajwa sana sana hadi sisi mangumbalu tunahisi ndio wale wasiojulikana na sasa wanajulikana, Kuna Polisi wanahusishwa na utesaji mikoa tofauti na kauli za kupotezana
Acha watajane. Kama alivyosema Pythagoras hapo juu, acha mvua inyeshe tuone panapovuja.
Hii ni avenue nyingine ya matengenezo ya nchi
 
Wacha inyeshe tuone panapovuja
Jambo la dhahiri kabisa ni kuwa JESHI limebaki uchi. Madhila ya vijana kupata matatatizo ya akili baada ya opereesheni na kisha kutelekezwa yanatafakarisha sana. Anyway ngoja tuone
 
Acha mchwa waotoke tuone mbayuwayu wanavyochekelea!!!!!
 
Kesi isifutwe twende hadi Mahakama ya Rufaa ili kuthibitisha kuwa CCM ni genge la kigaidi linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendelea kutawala kidhalimu

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Mungu akitaka kuangusha utawala uwa anawaondolea kwanza akili na busara,mnashangaa nini?

Ndivyo alivyofanya uko nyuma tangu wakati wa mfalme Suleiman.

Adui mpige kichwani.
 
Mbona mnaweweseka sana enyi wafuasi wa mfalme Mbowe?

Huku mnasema serikali itaumbuka!

Kule mnaomba kesi ifutwe,kama mnao ushahidi wa kutosha kumtoa mbowe hatiani, kwa nini msiuweke hadharani badala ya kukesha mitandaoni mkiingilia Mahakama?

Acheni mahakama huru ifanye kazi yake na haki yenu itapatikana tu.
 
Kuna msemo kwamba 'If you you leave your children in mud you can't complain that they are playing with mud."
 
Acha iendelee kunyesha ili tuone panapovuja
 
Kuna mambo yanayokea ili historia ijiandike!

NB: Haya yatokeayo leo ni machache na mepesi kuliko mengi na mazito yatakayotokea huko mbele ya safari!
Enough is enough!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…