Bila mzungu tunaemlalamikia ni mbaguzi waafrika tungekuwa na hali ngumu sana, biashara ya utumwa ingeendelea, tungebaguliwa zaidi

Bora mkoloni mweupe kuliko mkoloni mweusi.

Maisha ya mwafrika yalikuwa na afadhali kabla ya Uhuru.

Ubepari ndio mfumo sahihi hata Mwenyezi Mungu anaubariki, faida za ubepari kila mtu anapata ajira na Kodi inaongezeka.

Ujamaa ni mfumo wa kuwafanya wengi wawe masikini ili waweze kutawaliwa.
 
Arabuni Kuna weusi wengi tu,huko Oman maeneo ya pwani,saudia Hadi familia ya kifalme Kuna weusi,unabugia tu propaganda Kama ugoro
 
Eti afadhali mkoloni mweupe?? Wazungu maskini kwao wamejaa sema haujafika kuenda UK, US ujionee .
Tena sio wachache wengi sana , hakuna mkoloni aliye nafuu ila matajiri wenu ndo huleta maendeleo . Sasa nyote mkiwa watumwa mnasaidikaje. Hayo mawazo yamekufanya mkoloni akilini .
Kama kulikuwa na unafuu mbona wazee wako walijitolea kupigania uhuru, usiwatukane , mbona hao wazungu wanawapa Ukraine silaha kimpinga mrusi ??? Kwani yy sio mzungu. Mbona mchina ametamba??? Shida wabunge mnawachagua kina babu tale n.k pale unatarajia mwimbaji wa muziki ajue nn in economic analysis and planning , so heri muwape waalimu viti angalau hata na mapungufu yao wana elimu kidogo .uongozi ndo mbovu tu nchini
 
Hao masikini USA na ulaya Magharibi ni waliojitoa kwenye mfumo wengi ni mateja, wagonjwa wa akili nk kama foreigner anapata ajira sembuse mzawa.
Hao wapigania uhuru walipigania maslai yao binafsi kwa kuwahadaa waafrika wengi na baada ya uhuru wakajigeuza wakoloni weusi kwa kuwatendea mabaya na ukatili sana waafrika wenzao kuliko hata alivyotenda mkoloni mweupe,unamjua kamuzu Banda,dikteta moi, Mugabe, Mobutu,nguema,bokasa au we ni generation Z.mbona baada ya uhuru walishindwa kuleta maendeleo.
Msoto wanaosota waafrika wengi ni matokeo ya kiherehere cha wapigania uhuru.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…