Bilioni 12 Kutumika Kukijanisha Jiji la Dodoma

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Serikali imesema kiasi cha shilingi Bilioni 12 kitatumika katika utekelezaji wa mradi wa kukijanisha jjiji la Dodoma ikiwemo kupanda miti na maua katika hifadhi za Barabara ili kutunza mazingira na kupendezesha mandhari ya jiji hilo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa Juni 11, 2024 jijini Dodoma katika kikao cha pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Selemani Jafo ambapo Mradi huo wa Green Solution Project (GSP) unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ambayo inafadhili mradi wa ujenzi wa Barabara ya Mzunguko wa Jiji la Dodoma (km 112.3).

“Naamini Timu za Wataalam wa Ofisi ya Makamu wa Rais na Wizara ya Ujenzi na Taasisi zake zikishirikiana na kujadili suala la utunzaji wa mazingira hususan katika jiji la Dodoma watakuja na mikakati bora ya utekelezaji wa mradi huu”, amesema Bashungwa.

Bashungwa ameeleza kuwa kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo katika jiji la Dodoma utafungua mawanda mapana kwa Serikali kutafuta wadau wa maendeleo watakaoshirikiana na Serikali kukijanisha maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Bashungwa amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,kuisimamia TANROADS kuandaa usanifu na upembuzi yakinifu ambao hautaathiriwa na mabadiliko na uboreshaji wa miundombinu ya barabara ikiwemo upanuzi wa barabara ambao umekuwa ukisababisa ukataji wa miti ambayo imepandwa hivi karibuni.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo ameipongeza Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS kwa zoezi la upandaji miti na kuitunza hususan katika barabara Chimwanga- Ihumwa Jct jijini Dodoma.
Dkt. Jafo amesema Serikali ina mpango wa kukutana na wamiliki na wawekezaji wa maeneo yaliyo pembezoni mwa barabara ili kuweka mkakati wa pamoja wa upandaji miti na bustani za maua ili kuendelea kukijanisha nchi.

Naye, Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka TANROADS, Julius Luhuro, amesema kuwa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) itaendelea kukijanisha hifadhi za Barabara kwa barabara zilizopo na zinazojengwa katika maeneo mengi nchini hususan Dodoma na kusisitiza kuwa mkakati huo ni zoezi endelevu lengo ni kuhifadhi mazingira.

 
Wana siasa kuna wakati lazima muwe serious,haya mambo hapo Dodoma tumeyashuhudia sana,inapofika kipindi cha kiangazi mnaanzisha kampeni za kupanda miti,mlikuwa wapi wakati mvua ziliopokuwa zinanyesha.Dodoma ina kipindi cha kiangazi cha miezi karibu 7 mpk 8 ni kiangazi kikali,hiyo miti itamwagiliwa na nini muda wote huo...?
 
Waweke na mkakati wa kuimwagilia angalu mara Tatu kwa wiki
 
Sijasikia popote kuyafikisha maji ya Victoria yaliyokomea Igunga jijini Didoma kama ilivyokuwa dhamira ya Magufuli.

Utakijanishaje eneo bila kuwa na vyanzo vya maji vya uhakika ili kumwagilia hizo bustani na vipandwa mbali mbali watavyovianzisha?

Bil. 12 kupanda bustani pakame, hiyo ni harufu ya upigaji.
 
Upo sahihi mkuu.
 
Bila kupata suluhisho la watu kuachana au kuponguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya mkaa, bado ukataji wa miti utaendelea.
 
Hili suala wanataka kulikuza tu na kuweka mabajeti ya kutupeleka barabarani kama GEN Z. Nawapa ushauri ambao siwadai consultancy fee....peleka fedha za transportation na chakula kwa magereza na JKT kazi kwisha.
 
Wasisahau kupanda miti ya matunda. Waarabu waliopanda maembe toka Bagamoyo hadi ujiji hawakuwa wajinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…