Bilioni moja na Happy Joseph

chambimagaka

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2017
Posts
288
Reaction score
338
Tuanze na BILIONI 1.
Naona watu wanaitajataja sana bila ufafanuzi wa kueleweka. . . Kuna wanaoifananisha na mikopo Ya elimu Ya Juu, wengine darasa katika shule. . . Nk. . .

Ngoja Mimi niiseme kwa ulaini kabisa. . .
Bilioni moja ni sawa na milioni elfu moja. . . Yaani watu wakipanga foleni, na KUANZA hesabu namba kuanzia moja hadi elfu, WOTE wanaweza kugawiwa milioni moja " keshi " . . . .

Ngoja kwanza. . . . Watu elfu moja unaelewa ni kama kiasi gani hivi ?
Hebu funga macho kumbuka darasani uliposoma shule Ya msingi mlikuwa wangapi, au shule yenu ilikuwa na wanafunzi wangapi. . . Kama hawakuwa elfu, mfano shuke nlosoma mie walikuwa wanafunzi mia nne, Sasa hapo nikisema. Mara Mbili wanafika mia nane. . . Halafu nikiongeza kanusu hapo wanafika elfu. . .

Sasa tuachane na Hawa wanaopanga mstari kiholela. . . .
Tuseme Hivi, uchukue vijana elfu moja wamachinga, uwape kila mmoja fedha taslimu shilingi milioni 1 waongezee mtaji, ama mama ntilie 1000 uwape milioni kila mmoja waboreshe biashara zao. . . Au uwatafute "shuu shaini" elfu uwape milioni kila mmoja waviweke smati vibanda vyao. . .

Au uingie sokoni manzese, ugawe milioni moja kwa kila mfanyabiashara atakayeweza kuimba beti Mbili Za wimbo wa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo WOTE [emoji16] hadi wafike elfu moja. . . Waambie waboreshe biashara zao. . . Ama ukapita salon Za kike na Za kiume ukagawa mil moja Za kuwawezesha kuimarisha biashara zao. . .

Labda tuachane na Hao. . .
Ukaamua upite maduka Ya madawa elfu moja. . . Uwakabidhi. . . Mtaji huo. . . . Ama pale feri ukawakabidhi wachuuzi 1000, milioni kila mmoja, waboresha biashara zao. .
[HASHTAG]#Hebu[/HASHTAG] ongezea, watu elfu moja wanaweza kupewa milioni kila mmoja wafanyie nini cha maendeleo?
[HASHTAG]#hapo[/HASHTAG] ulipo va vyuma vilivyo na kutu, ukipewa milioni utaifanyia nini. . . Kama ni Mfugaji Utanunua mifuko mingapi Ya Chakula cha mifugo ? Kama Wewe ni mkulima, mbegu na. Mbolea ni vipi hapo ? Kama ni seremala, vipi mashine Ya kugonga misumari ?

[HASHTAG]#nimeamua[/HASHTAG] kuielezea bilioni kwenye maisha Ya kawaida Ya watu wengi. . . Ukiielezea kwenye ujenzi wa darasa, wanaweza wasielewe hasa wale ambao hawajawahi kujenga. . . Ama kuielezea kama mkopo kwa elimu Ya juu, Kuna watu hawaelewa, watasema hawajawahi kwenda chuo kikuu. . .
[HASHTAG]#tunabana[/HASHTAG] matumizi
[HASHTAG]#uchumI[/HASHTAG] wa viwanda
[HASHTAG]#tunapambana[/HASHTAG] na matumizi mabaya Ya fedha
[HASHTAG]#viwanda[/HASHTAG] kila mtaa
[HASHTAG]#tunawatumikia[/HASHTAG] wanyonge
[HASHTAG]#tunasema[/HASHTAG] ukweli Na tunamwogopa Mungu

[emoji767] BIBI HAPPY J
 
Kama tungewagiwa mifuko ya mbolea za kukuzia mazao yao wakulima wa bonde la usangu I think tungeinua kilimo cha mpunga kwa asilimia kubwa kwani karibia wakulima elfu tano wangenufaika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…