Bill Gates mapumzikoni Pemba!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Kutokana na sababu nyeti habari hii sikuirusha mapema. Hata hivyo, Yule Bilionea Mkubwa wa Kimarekani Bill GAtes alikuwa nchini (nadhani bado yupo) akiwa mapumzikoni kule Pemba kwenye mojawapo ya visiwa vidogovidogo ambako yuko mapumzikoni.

Kitu ambacho kinafanya jambo hili la kukuna vichwa ni tetesi kuwa sehemu hiyo imeuzwa kwa tajiri huyo mkubwa duniani na imekuwa "nyumbani mbali na nyumbani".

Ni kwa kiasi gani wananchi wa Pemba au maeneo hayo yananufaika na ujio wa mara kwa mara wa tajiri huyo?
 
Mwanakijiji,
Unatutania au ndo kweli mbona hii mpya? well labda tuseme tuna bahati japo kutembelewa na huyu bwana mkubwa, but the question remains: ni namna gani hao wapemba au watanzania wengineo wanafaidika?
 
Mwanakijiji,
Unatutania au ndo kweli mbona hii mpya? well labda tuseme tuna bahati japo kutembelewa na huyu bwana mkubwa, but the question remains: ni namna gani hao wapemba au watanzania wengineo wanafaidika?
Khee sasa unahamaki kwa kuwa amete,mbelea Pemba. Usijali yote hiyo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Mwanakijiji,
Unatutania au ndo kweli mbona hii mpya? well labda tuseme tuna bahati japo kutembelewa na huyu bwana mkubwa, but the question remains: ni namna gani hao wapemba au watanzania wengineo wanafaidika?

duh.. sikutanii mkuu wangu.. katoto kanzi kalikototolewa Pemba kameleta habari za uhakika ambazo nimeweza kuthibitisha kutoka vyanzo huru. Huwa anakuja mara kwa mara mapumzikoni.
 
Niliposoma headline nilishangaa na kujiuliza Bilionea Bill Gate na Pemba wapi na wapi. Kwa hoteli gani ya hadhi yake!?. Baada ya kuisoma, nimekubali. This country every thing is possible na Wapembe hawafaidiki chochote zaidi ya cesspit ni ndani ya bahari yao.
Niliwahi kutaka japo kupata kinyaji Dongwe Club Vicanze ya Taliano. Safari yangu iliishia getini. Baada ya kuonyesha ID yangu ya wakati huo, ndipi nikaruhusiwa kufika reception na kuambiwa masharti
1,On line booking.
2. Payment in US $
3. Deposit in Italy
4 only Credit card
Nikajichokea na kujiondokea zangu. Hiyo ni hotel bussiness Zanzibar gets nothing, itakuwa kisiwa?.
 

This is going to be the land of MAFIA. Just wait and see!
 
....khaaaa!! (with a light touch)
....kwa hii habari kwenda kimya kimya, mimi namtolea lawama GT kwanza, kisha Abdulhalim na mwingine ni mr. Kibs!

....GT kwa kuwa mtu mwenye uelewa mkubwa katika mengi, international relations, curruption links, economics na mengine mengi kede wa kede, hili nahisi nalo analijua ila kaliminyia.
....GT kwa kuwa proponent wa great thinkers ideology lakini kutoifanyia kazi pale inapofaa na kuhitajika, haswa linapokuja swala la Pemba na visiwa vyake. (ame diverge resources kufatilia mambo ya Babaye Said Kubenea instead ya kufatilia Wapemba wanafaidika vipi na hii supposedly new investment)

....Abdulhalim, kwa kuwa mtu mwenye kuelewa mengi about his society lakini kuwa mchoyo wa kusambaza ILIM kwa watu wa MATAIFA YOTE yasiyo Ya Waisrael!!!

....Kibunango, kwa kuwa jirani sana na visiwa vya Pemba lakini badala ya kufatilia mambo haya makubwa makubwa kwa majirani zake, anafatilia Wazenji wanakunywa nini na vipi wanarusha vifuko mabarabarani!!!

Have a gud weeekend!

....BTW Mkjj, hicho kitoto cha inzi kinafata nini huko kwenye marashi ya karafuu?!! miye nilifikiri chenyewe ni kwenye uozo uozo tu..... haya bana, hebu miye......
 
....

....BTW Mkjj, hicho kitoto cha inzi kinafata nini huko kwenye marashi ya karafuu?!! miye nilifikiri chenyewe ni kwenye uozo uozo tu..... haya bana, hebu miye......

mmh.. hiki bado hakijajua kufuatilia uchafu..chenyewe kimesikia Pemba kuna harufu nzuri basi kikaruka kuifuata.
 
Duh na wewe mzee mzima kweli hupitwi na jambo ndugu yangu, hivi ni kweli au vipi??
 
du ebwanaaaaaaaaaaaeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
huyu huyu bili gates????

vile visiwa ni vizuri sana lakini hatuvitumii ki uchumi mweee kila kukicha ni kelele tu
 
Steeeve...! Are you serious...!?
 

Tafadhali tupatie jina la hicho kisiwa kidogo anakopumzikia Bwn. Bill Gate. Je amekuja na mkewe?
 
Tafadhali tupatie jina la hicho kisiwa kidogo anakopumzikia Bwn. Bill Gate. Je amekuja na mkewe?

mzee ningependa kufanya hivyo, lakini that will be beyond the intrusion of his privacy. Akishaondoka nitaweka hapa vinginevyo ninaweza kuattract unwanted attention wakati yeye kaja mapumzikoni tu.
 
Ungesema kafikia hotel gani , ingeleta maana zaidi. Lakini kumbuka mwkjj, mozambique kuna pemba ambayo ndo kivutio cha watalii kufa. Ukiwa sa [ot air port] utaona safari nyingi za kule. Tudhibitishie basi, sio kwa porojo za hear say.
 
Source: Why Visit Zanzibar in Africa - beach holidays - Zanzibar hotels

 
Source: Places to Visit during Tanzania and Zanzibar African Safari | African Portfolio

 
Ni kweli tuna maeneo mengi sana ambayo natural beauty yake haina mfano KAMA TUNGEKUWA TUMEKAA MKAO WA KULA tungeingiza pesa nying sana kutokana na utalii. Mtu mmoja amesema hapo juu kazi yetu sisi ni maneno maneno na bla bla tu.
Wapemba hawawezi kufaidika kwa lolote zaidi ya kodi anayolipa mwenye hotel serikalini. Wangeweza kufaidika kama kungekuwa na biashara za wazawa ambazo zingeguswa na ujio huo au kwa namna moja au nyingine zinafanya biashara na hiyo hotel. Tutaweza kuliepuka hili pale tutakapowezesha wazawa kuwa tayari kujiingiza kenye biashara na faida wanayopata waiwekeze hapa hapa nchini. Vinginevyo sisi tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu tu.
UMK.
 
Ndugu bill gates amekuwa anakuja visiwani mara nyingi hata mwaka jana alikuwa kule ni kweli kuna kisiwa fulani chenye hoteli haijulikani ni hoteli ya nani kwa sababu hata tra wanapojaribu kufuatilia huwa wanashindwa kisiwa hicho ndio kilichangia kwa kiasi kikubwa kumfukuzisha hata raisi mstaafu wa afkrika ya kusini kuna picha alipiga kule hata zuma aliwahi kutembelea kabla ya mbeki kujiuzuru wiki moja kabla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…