Billionea aliyemnunulia raila gari aina ya Hummer ampongeza ruto kwa kumtoa jela

Billionea aliyemnunulia raila gari aina ya Hummer ampongeza ruto kwa kumtoa jela

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Don Bosco alikamatwa na kufungwa nchini Tanzania 2013
Bosco na rafikiye ambaye ni wakili walipatikana na kosa la kusambaza noti bandia
Akakubali makosa na kufungwa jela miaka mitano
Mwanabaishara tajika Don Bosco Gichana amejitokeza wazi na kumpongeza pakubwa Naibu Rais William Ruto kwa kusaidia katika kumtoa jela baada ya kifungo cha muda wa miaka mitano.Tanzania
Ingawa hakueleza kuhusu alichofanya Ruto katika kumtoa jela, bilionea huyo alibainisha kuwa Naibu Rais alimsadia na kuwa walikuwa wakizungumza muda wote alipokuwa jela.
Alimpongeza pakubwa Naibu Rais William Ruto kwa kumtoa jela.
Mwanabishara huyo mwenye umri wa miaka 41 amefanya mikutano kadhaa na viongozi wakuu serikalini akiwemo Naibu Rais William Ruto.

‘’ Asante sana kwa mchango wako katika kuachiliwa huru kwangu. Mungu akubariki William Ruto kwa ushauri wako muda huu wote,’’ alisema alipokuta na Ruto Alhamisi, Okotoba 25.
Mwanasiasa huyo ambaye aligonga vichwa vya habari 2007 baada ya kumzawidi Raila odinga gari aina ya Hummer SUV amekuwa jela tangu 2013.
Bosco alikamatwa akiwa Namanga baada ya kumtembelea wakili rafikiye Median Mwale aliyezuiliwa katika kituo cha polisi cha Arusha ya Kati.
Wawili hao wakifungwa baada ya kukubali makosa ya kusambaza noti bandia.

Maelfu walihudhuria sherehe ya kumkaribisha humu nchini Ijumaa, Oktoba 26 katika kaunti ya Kisii.
 
Kenyan politics nimegundua inafwatiliwa sana, With all our neighbors. I was reading an Ethiopian Journalist article analysing deep Kenyan politics hadi unadhani ni mkenya, Tanzanians are even worse. A primary school child might even be knowing all the governors in kenya plus their politics but knows nothing about his country's politics[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Pambaneni na hali zenyu.
Halafu Ruto anaeza kuwa next Presda wa Kenya. Jukwaani ana kwambia hapendi ufisadi na wizi! Kenya na wizi ni kama pete na kidole
 
Anashukulu nn wakati kama liza kifungo chake ?
 
Halafu Ruto anaeza kuwa next Presda wa Kenya. Jukwaani ana kwambia hapendi ufisadi na wizi! Kenya na wizi ni kama pete na kidole
Umenikumbusha kuhusu rais flani aliyeamuru wabakaji waachiliwe kabla hawajamaliza kutumikia kifungo chao. Sijui na yeye pia tutamuitaje.
 
Kenyan politics nimegundua inafwatiliwa sana, With all our neighbors. I was reading an Ethiopian Journalist article analysing deep Kenyan politics hadi unadhani ni mkenya, Tanzanians are even worse. A primary school child might even be knowing all the governors in kenya plus their politics but knows nothing about his country's politics[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Pambaneni na hali zenyu.
✅ ✅ ✅
 
Umenikumbusha kuhusu rais flani aliyeamuru wabakaji waachiliwe kabla hawajamaliza kutumikia kifungo chao. Sijui na yeye pia tutamuitaje.
Inahitaji moyo wa kujitolea kusaidia maskini aliye kwenye matatizo, hasa kwa kufuata sheria. Ila mtu anayemsaidia tajiri aliye kwenye shida inajulikana ana sukumwa na nini hasa akitumia nguvu za ziada kutimiza lengo lake.
 
Kenyan politics nimegundua inafwatiliwa sana, With all our neighbors. I was reading an Ethiopian Journalist article analysing deep Kenyan politics hadi unadhani ni mkenya, Tanzanians are even worse. A primary school child might even be knowing all the governors in kenya plus their politics but knows nothing about his country's politics[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Pambaneni na hali zenyu.


Ni kweli kabisa, Mtanzania wa kawaida anajua zaidi kuhusu Kenya kuliko kinyume chake, nimefika Kenya mara nyingi na ukiondoa Raisi Magufuli, hakuna Kiongozi wanayemjua, kwanza nilishangaa hata hawajui kama TZ kuna makamu wa Raisi achilia mbali jina la Waziri mkuu wetu, Wakenya webgi walijua kwamba TZ kuna Makamu Raisi siku ya kuapishwa Uhuru Kenya ambapo Raisi wetu aliwakilishwa na Mama Samia Makamu wetu wa Raisi, lkn hapa Bongo wanaweza kukwambia majina ya Viongozi wote wa Kenya hadi hata Upinzani!

Hata ukiangalia TV ya TZ hukosi news ktk Kenya au sijui UG, lkn ukiwa Kenya au Uganda kuona news za JMTZ ni mara chache sana!
 
Halafu Ruto anaeza kuwa next Presda wa Kenya. Jukwaani ana kwambia hapendi ufisadi na wizi! Kenya na wizi ni kama pete na kidole
Heehe. Cool boy. I am 'telleble solle' kwa kukusumbua .Nimekuuliza maswali ya kijinga mara mbili.'connection and citizenship'
Nilifanya hivyokimakusudi
I owe you an apology.
 
Inahitaji moyo wa kujitolea kusaidia maskini aliye kwenye matatizo, hasa kwa kufuata sheria. Ila mtu anayemsaidia tajiri aliye kwenye shida inajulikana ana sukumwa na nini hasa akitumia nguvu za ziada kutimiza lengo lake.
Kwahivyo rais ambaye aliamuru watuhumiwa wa ubakaji, tena ubakaji unaohusu watoto, waachiliwe bila sababu zozote za kimsingi. Kabla hawajamaliza kutumikia kifungo chao ana haki ya kufanya hayo zaidi ya kiongozi ambaye amefanikisha kuachiliwa kwa raia wa nchi yake aliyetupwa korokoroni ungenini? Okei.
 
Ni kweli kabisa, Mtanzania wa kawaida anajua zaidi kuhusu Kenya kuliko kinyume chake, nimefika Kenya mara nyingi na ukiondoa Raisi Magufuli, hakuna Kiongozi wanayemjua, kwanza nilishangaa hata hawajui kama TZ kuna makamu wa Raisi achilia mbali jina la Waziri mkuu wetu, Wakenya webgi walijua kwamba TZ kuna Makamu Raisi siku ya kuapishwa Uhuru Kenya ambapo Raisi wetu aliwakilishwa na Mama Samia Makamu wetu wa Raisi, lkn hapa Bongo wanaweza kukwambia majina ya Viongozi wote wa Kenya hadi hata Upinzani!

Hata ukiangalia TV ya TZ hukosi news ktk Kenya au sijui UG, lkn ukiwa Kenya au Uganda kuona news za JMTZ ni mara chache sana!
Serikali ya kenya imewafanya Wananchi wake mazezeta walahi
 
Heehe. Cool boy. I am 'telleble solle' kwa kukusumbua .Nimekuuliza maswali ya kijinga mara mbili.'connection and citizenship'
Nilifanya hivyokimakusudi
I owe you an apology.
Nimesha kuzoea, unanikumbusha ........... wanjiru. Manzi wa Nai nilikua nae kipindi nasoma. Alikua anazingua kama wewe [emoji2]
 
Ni kweli kabisa, Mtanzania wa kawaida anajua zaidi kuhusu Kenya kuliko kinyume chake, nimefika Kenya mara nyingi na ukiondoa Raisi Magufuli, hakuna Kiongozi wanayemjua, kwanza nilishangaa hata hawajui kama TZ kuna makamu wa Raisi achilia mbali jina la Waziri mkuu wetu, Wakenya webgi walijua kwamba TZ kuna Makamu Raisi siku ya kuapishwa Uhuru Kenya ambapo Raisi wetu aliwakilishwa na Mama Samia Makamu wetu wa Raisi, lkn hapa Bongo wanaweza kukwambia majina ya Viongozi wote wa Kenya hadi hata Upinzani!

Hata ukiangalia TV ya TZ hukosi news ktk Kenya au sijui UG, lkn ukiwa Kenya au Uganda!
Sasa ulitegemea nini wakati wengi wenu mmekata tamaa na wanahabari wa kitz, na media zenu na siasa zenu? Mnatizama T.v za Kenya na kufatilia siasa za Kenya zaidi ya hata wakenya wenyewe! Mbona habari za Uganda, Rwanda, Ethiopia, S.Sudan na hata Zimbabwe huwa zinafatiliwa sana na wakenya? Jombaa, acha ukweli usemwe tu, hatuwamaindi kama mnavotumaindi. [emoji1]
 
Sasa ulitegemea nini wakati wengi wenu mmekata tamaa na wanahabari wa kitz na media zenu na siasa zenu? Mnatizama T.v za Kenya na kufatilia siasa za wakenya zaidi hata ya wakenya wenyewe. Mbona habari za Uganda, Rwanda, Ethiopia, S.Sudan na hata Zimbabwe huwa zinafatiliwa sana na wakenya? Jombaa, ukweli usemwe tu, hatuwamaindi kama mnavotumaindi. [emoji1]


Ndiyo ukweli wenyewe huo uliousema!
 
Nimesha kuzoea, unanikumbusha ........... wanjiru. Manzi wa Nai nilikua nae kipindi nasoma. Alikua anazingua kama wewe [emoji2]
Kusema ukweli, nimejaribu sana kuona kama utanitusi kama wenzako. Tangu niingie humu nimepokea kila aina ya matusi hususan nyani. Nilishangaa kuona ulivyo tofauti na wao. Hauna ubaguzi wa kijinsia. Licha ya kukuuliza maswali ambayo hata mwanafunzi wa darasa la pili hawezi uliza hukuhemka na kunitusi. Unajiondoa tu kistaarabu.
You handle situations very well man. You are a gentleman.
 
Kwahivyo rais ambaye aliamuru watuhumiwa wa ubakaji, tena ubakaji unaohusu watoto, waachiliwe bila sababu zozote za kimsingi. Kabla hawajamaliza kutumikia kifungo chao ana haki ya kufanya hayo zaidi ya kiongozi ambaye amefanikisha kuachiliwa kwa raia wa nchi yake aliyetupwa korokoroni ungenini? Okei.
Mkuu ile kesi ilikua na mambo mengi sana ifuatilie vizuri utanisoma... Magufuli anaye julikana dunia nzima kwa kukemea ufisadi na uonevu wa maskini unahisi anaeza kujichafua kwa kutoa msamaha kwa mtu ambae anakosa ili iweje!? Ili apate nini? Kuhusu Ruto, mwanasiasa anae kumbatia ma bwanyenye ni hatari sana kwa mustakabali wa nchi yenu. Naomba ukumbuke ushauri wangu utakapo enda ku vote next time.
 
Kusema ukweli, nimejaribu sana kuona kama utanitusi kama wenzako. Tangu niingie humu nimepokea kila aina ya matusi hususan nyani. Nilishangaa kuona ulivyo tofauti na wao. Hauna ubaguzi wa kijinsia. Licha ya kukuuliza maswali ambayo hata mwanafunzi wa darasa la pili hawezi uliza hukuhemka na kunitusi. Unajiondoa tu kistaarabu.
You handle situations very well man. You are a gentleman.
Hahahaa.. Ngoja niandae mahali, nije na ng'ombe ngapi? Au bado unasoma..
 
Back
Top Bottom