Bima gani ni nzuri kwa bajaj

Bima gani ni nzuri kwa bajaj

renamaizo

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2014
Posts
2,134
Reaction score
3,064
Nataka ninunue bajaj kwa ajili ya biashara je bima gani ni nzuri.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Nataka ninunue bajaj kwa ajili ya biashara je bima gan ni nzuri

Natanguliza shukran zangu za dhati
Bima gani kwa maana ya Kampuni au aina ya Bima??
Kama ni Kampuni zote zinafanana tu, zaidi ningekushauri Alliance Insurance ninayoitumia.

Kama ni aina ya Bima basi Bima Kubwa (Comprehensive) ingefaa zaidi ili ikulinde na Chombo chako wewe.
 
Bima gani kwa maana ya Kampuni au aina ya Bima??
Kama ni Kampuni zote zinafanana tu, zaidi ningekushauri Alliance Insurance ninayoitumia.

Kama ni aina ya Bima basi Bima Kubwa (Comprehensive) ingefaa zaidi ili ikulinde na Chombo chako wewe.
Thanks !! Nimekusoma nimepewa copy ya mkataba apa kuna kifungu kimeandikwa io comprehesive insurance au bima kubwa nimeelewa kiasi naomba unipe ufafanuzi kidogo comprehesive bima ni nn ? Na je kuna aina gan zengine za bima ?

Kuhusu swala la kampuni its clear nimekuelewa
 
Thanks !! Nimekusoma nimepewa copy ya mkataba apa kuna kifungu kimeandikwa io comprehesive insurance au bima kubwa nimeelewa kiasi naomba unipe ufafanuzi kidogo comprehesive bima ni nn ? Na je kuna aina gan zengine za bima ?

Kuhusu swala la kampuni its clear nimekuelewa
Aina za Bima ziko nyingi, Ila kwa swala lako niseme ziko mbili tu, Bima ndogo na Bima kubwa. Kizungu ndio hiyo"Third party" na "Comprehensive".

Third party/Bima Ndogo faida yake ni kua bei/gharama yake ni rahisi tu. Hasara yake ni kwamba ikitokea jambo lolote baya (kuibiwa/ajali/kuungua) kuhusu chombo chako, yenyewe itamfidia "Kitu/Mtu" wa tatu tu. Wewe dereva na Chombo chako hamtahusika katika kufidiwa huko.

Comprehensive/Bima kubwa hii ni kua ikitokea jambo lolote baya (kuibiwa/ajali/kuungua) kuhusu chombo chako yenyewe itamfidia kila alieathirika na ajali hiyo ukiwemo wewe dereva pia. Na chombo chako kama kimepata madhara nacho kitafidiwa pia.

"Kitu/Mtu" wa tatu ni Nani? Hapa wewe unaendesha hicho chombo/Bajaji Ni wa Kwanza. Chombo/Bajaji yako ni ya pili, utakae msababishia ajali iwe ni mtembea kwa miguu, au chombo cha moto au hata nyumba, kibanda umegonga ndio "Kitu/Mtu" wa tatu.
 
Aina za Bima ziko nyingi, Ila kwa swala lako niseme ziko mbili tu, Bima ndogo na Bima kubwa. Kizungu ndio hiyo"Third party" na "Comprehensive".

Third party/Bima Ndogo faida yake ni kua bei/gharama yake ni rahisi tu. Hasara yake ni kwamba ikitokea jambo lolote baya (kuibiwa/ajali/kuungua) kuhusu chombo chako, yenyewe itamfidia "Kitu/Mtu" wa tatu tu. Wewe dereva na Chombo chako hamtahusika katika kufidiwa huko.

Comprehensive/Bima kubwa hii ni kua ikitokea jambo lolote baya (kuibiwa/ajali/kuungua) kuhusu chombo chako yenyewe itamfidia kila alieathirika na ajali hiyo ukiwemo wewe dereva pia. Na chombo chako kama kimepata madhara nacho kitafidiwa pia.

"Kitu/Mtu" wa tatu ni Nani? Hapa wewe unaendesha hicho chombo/Bajaji Ni wa Kwanza. Chombo/Bajaji yako ni ya pili, utakae msababishia ajali iwe ni mtembea kwa miguu, au chombo cha moto au hata nyumba, kibanda umegonga ndio "Kitu/Mtu" wa tatu.
Nimekusoma ebu naomba unisaidie gharama za comprehesaive bima
 
Kabda ya kununua bima zingatia Haya yafuatayo............

  • Hakikisha ni kweli unahitaji bima na itaendana na janga ambalo likitokea na hutoweza kulimudu kifedha. mfano matatizo ya afya, janga la wizi, moto au hasara ya kupoteza fedha katika biashara yako.

  • Angalia gharama ya bima kama utaweza kuzimudu na kwa muda mrefu hata kama malipo ni kwa kila mwezi.

  • Zingatia fidia utakayoipata kama itaendana na majanga utakayo yapata. mfano mkataba wa bima unasema fidia itakua ni 10 milioni endapo likitokea janga la moto katika biashara yako, je ukiangalia katika biashara yako janga la moto likitokea fidia ya 10 millioni itakidhi?

  • Zingatia mashari ya mtakaba wa bima na unaeleza nini endapo janga likitokea , utahisika vipi katika hatua za mwanzo na ni viambatanishi vipi vinajitajika katika kuwasilisha madai ya bima.

  • Zingatia ni kampuni ipi ya bima inatoa bima unayohitaji. hapa utaangalia ubora na uhakika wa kupata huduma haraka endapo majanga yakitokea.

  • Zingalia kuchagua wakala (agent) au dalali (Broker) wa bima ambae ni bora katika kutoa huduma za kibima kuanzia mwazo wa mauzo ya bima hadi pale janga likitokea.


Mwishio, bima ni ni mkataba wa ahadi kwa maana ya kwamba kampuni ya bima inakuahidi kukupa fidia endapo janga fulani likitokea na inakutaka wewe kulipa kiasi kidogo cha fedha kwa kipindi hicho cha makubalianio. Katika makubaliano anaweza kuwepo dalali wa bima au wakala ambaye atasimamia katika hatua za manunuzi ya bima na endapo janga husika likitokea.

Kwa Msaada wa madai ya bima wasiliana na mimi kupitia number +255 765 827 355
 
Back
Top Bottom