G-Mdadisi
Senior Member
- Feb 15, 2018
- 165
- 100
Moja ya maamuzi muhimu ambayo yatafanywa na Serikali na kimsingi yanachochea tabasamu zaidi kwa mamilioni ya watanzania ni hili la BIMA KWA WOTE ama 'Bima kwa kila Mtanzania.'
Nimefarijika sana kuona hata waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Afya Nchini, Dkt. Gwajima kuthibitisha kwamba zaidi 85% ya watanzania wapo nje ya mfumo wa bima ya Afya. Hii ni hatari kwa taifa.
Kumbuka hawa watanzania 85% wanaozungumziwa hapa wote ni wale wazazi/ndugu zetu vijijini ambao hatma ya afya zao wakiugua wanategemea wauze kilo ya mahindi, Mpunga, uwele, dagaa au kulima vibarua. Ndipo wapate shilingi elfu 1 wakanunue Panadol dukani angalau ili wapoze maumivu ya kichwa baada ya siku ndefu ya kuunguzwa na jua kali.
Hizo 15% zilizobaki ni mchanganyiko wa wale wenye vibarua vidogo ambavyo taasisi zao zinawalipia bima kule NHIF au kwingineko pamoja na wale watanzania daraja la kwanza ambao akiumwa na kichwa bima yake inamruhusu kwenda Hospital yoyote aipendayo bila kikwazo.
Wakati ambapo serikali inaelekea kukamilisha mpango huu marhaba kwa watanzania, ni lazima kwanza ijibu swali la iwapo mpango huu utafanikiwa, 'je, ni katika hospitali, vituo vya vyote (public/private) ambapo watanzania wataruhusiwa kwenda wakati wowote kupata huduma waitakayo kwa kutumia hizi bima? Au ni bima za kumsaidia mwananchi kuepukana na ulipaji wa TOZO za kuonana na daktari kifuatacho ni "Nenda pharmacy kanunue dawa hizi hatuna"
Moja ya kilio kilichopo kwa sasa hasa kwa wale wenye bima za kawaida wanakutana na wakati mgumu wanapohitaji huduma kwani vituo na hospitali nyingi zimegubikwa na ubaguzi wa aina ya bima ambazo zinapokelewa na kupelekea mhusika kutumia kiwango kikubwa cha pesa kuipata huduma hiyo jambo ambalo linakatisha tamaa wengine kujiunga na bima za afya kwa kuamini si msaada kwao tena.
BIMA YA AFYA kwa wote ni wazo jema sana, wema na ubaya wake utabaki mikononi mwa serikali juu ya namna itaamua kulitekeleza.
Bima hizi zikitumika kama tiketi za kupunguza gharama za kumuona daktari huku Dawa na huduma nyingine muhimu zikakosekana, bado ni tatizo.
Wasalaaam
#GMdadisi
Nimefarijika sana kuona hata waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Afya Nchini, Dkt. Gwajima kuthibitisha kwamba zaidi 85% ya watanzania wapo nje ya mfumo wa bima ya Afya. Hii ni hatari kwa taifa.
Kumbuka hawa watanzania 85% wanaozungumziwa hapa wote ni wale wazazi/ndugu zetu vijijini ambao hatma ya afya zao wakiugua wanategemea wauze kilo ya mahindi, Mpunga, uwele, dagaa au kulima vibarua. Ndipo wapate shilingi elfu 1 wakanunue Panadol dukani angalau ili wapoze maumivu ya kichwa baada ya siku ndefu ya kuunguzwa na jua kali.
Hizo 15% zilizobaki ni mchanganyiko wa wale wenye vibarua vidogo ambavyo taasisi zao zinawalipia bima kule NHIF au kwingineko pamoja na wale watanzania daraja la kwanza ambao akiumwa na kichwa bima yake inamruhusu kwenda Hospital yoyote aipendayo bila kikwazo.
Wakati ambapo serikali inaelekea kukamilisha mpango huu marhaba kwa watanzania, ni lazima kwanza ijibu swali la iwapo mpango huu utafanikiwa, 'je, ni katika hospitali, vituo vya vyote (public/private) ambapo watanzania wataruhusiwa kwenda wakati wowote kupata huduma waitakayo kwa kutumia hizi bima? Au ni bima za kumsaidia mwananchi kuepukana na ulipaji wa TOZO za kuonana na daktari kifuatacho ni "Nenda pharmacy kanunue dawa hizi hatuna"
Moja ya kilio kilichopo kwa sasa hasa kwa wale wenye bima za kawaida wanakutana na wakati mgumu wanapohitaji huduma kwani vituo na hospitali nyingi zimegubikwa na ubaguzi wa aina ya bima ambazo zinapokelewa na kupelekea mhusika kutumia kiwango kikubwa cha pesa kuipata huduma hiyo jambo ambalo linakatisha tamaa wengine kujiunga na bima za afya kwa kuamini si msaada kwao tena.
BIMA YA AFYA kwa wote ni wazo jema sana, wema na ubaya wake utabaki mikononi mwa serikali juu ya namna itaamua kulitekeleza.
Bima hizi zikitumika kama tiketi za kupunguza gharama za kumuona daktari huku Dawa na huduma nyingine muhimu zikakosekana, bado ni tatizo.
Wasalaaam
#GMdadisi