Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Ilisikika sauti toka ndani ya kaburi " Lete dongo, Lete reli, Lete ubao, lete majani". Nilikuwa miongoni mwa watu watano ambao wali bahatika kuchaguliwa kuingia ndani ya kaburi kumzika huyu shangazi yangu,na ndiyo ilikuwa mara ya Kwanza kufanya hivyo
Amekufa akiwa na Miaka 96 yaani bado minne Tu afikishe miaka 100. Shangazi huyu kama wiki mbili zilizo pita tulienda kumsalimia nikiwa na ndugu zangu,na kuna mdogo wangu anatarajia kuolewa October 2022, sasa Shangazi alisisitiza Sana kuwa lazima ndoa hii ya mdogo wangu ikafungwe kwake,alisisitiza kiasi ambacho akatuacha njia panda, je ndoa itaendaje kufungwa kwake wakati ilishapangwa kufungwa nyumbani Kwa Mzee,kutokana na utu uzima wake ikabidi Mimi niitikie Sawa ili siku ipite huku nikiwa najiuliza itakuwaje.
Kumbe alichokuwa hajui kuwa tayari visa yake ya kuishi hapa duniani ilikuwa imebakisha siku chache na hivyo kutakiwa kurudi Kwa Mola wake, September 20 ndiyo tuliyo mzika,nikiwa ndani ya kaburi naupokea mwili wake na kuuweka ndani ya mwanandani, nikawa najiuliza, Shangazi iko wapi ahadi yako ya kutaka ndoa ifungwe nyumbani kwako? Mbona umeondoka kabla ndoa haijafungwa?
Moral of the story:
Kwanza, kama binadamu huwa tuna mipango mingi Sana lkn huwa hatujui kesho yetu ikoje? Kikubwa ni kumcha Mwenyezi Mungu, mda wowote tupo safarini.
Pili, kwa Jambo lolote lile usipende kusema nitalifanya kesho, au nitajenga mwakani au nitaoa mwishoni mwa mwaka huu,Ila useme Mungu akipenda nitafanya kadhaa wa kadhaa, ndio maana Tunatakiwa na Mwenyezi Mungu tuseme insha'Allah Kwa maana "Mungu akipenda" kwasababu hatuna tunachokimiliki au kukiweza isipokuwa akipenda yeye.
Ni hayo tu!
Amekufa akiwa na Miaka 96 yaani bado minne Tu afikishe miaka 100. Shangazi huyu kama wiki mbili zilizo pita tulienda kumsalimia nikiwa na ndugu zangu,na kuna mdogo wangu anatarajia kuolewa October 2022, sasa Shangazi alisisitiza Sana kuwa lazima ndoa hii ya mdogo wangu ikafungwe kwake,alisisitiza kiasi ambacho akatuacha njia panda, je ndoa itaendaje kufungwa kwake wakati ilishapangwa kufungwa nyumbani Kwa Mzee,kutokana na utu uzima wake ikabidi Mimi niitikie Sawa ili siku ipite huku nikiwa najiuliza itakuwaje.
Kumbe alichokuwa hajui kuwa tayari visa yake ya kuishi hapa duniani ilikuwa imebakisha siku chache na hivyo kutakiwa kurudi Kwa Mola wake, September 20 ndiyo tuliyo mzika,nikiwa ndani ya kaburi naupokea mwili wake na kuuweka ndani ya mwanandani, nikawa najiuliza, Shangazi iko wapi ahadi yako ya kutaka ndoa ifungwe nyumbani kwako? Mbona umeondoka kabla ndoa haijafungwa?
Moral of the story:
Kwanza, kama binadamu huwa tuna mipango mingi Sana lkn huwa hatujui kesho yetu ikoje? Kikubwa ni kumcha Mwenyezi Mungu, mda wowote tupo safarini.
Pili, kwa Jambo lolote lile usipende kusema nitalifanya kesho, au nitajenga mwakani au nitaoa mwishoni mwa mwaka huu,Ila useme Mungu akipenda nitafanya kadhaa wa kadhaa, ndio maana Tunatakiwa na Mwenyezi Mungu tuseme insha'Allah Kwa maana "Mungu akipenda" kwasababu hatuna tunachokimiliki au kukiweza isipokuwa akipenda yeye.
Ni hayo tu!