Wima FC kutoka Mburahati Barafu imeibuka bingwa wa Kitila Jimbo Cup baada ya kuifunga Baruti FC kutoka Kimara kwa magoli 3-1 kwenye mchezo wa Fainali uliochezwa uwanja wa Kinesi, Shekilango, Ubungo.
Kitila Jimbo Cup ni mashindano yaliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ubongo ambaye pia ni Waziri wa Mipango na Uwekezaji Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo.
Baada ya mchezo wa Fainali, Mhe. Kitila Mkumbo ameweka wazi lengo la mashindano na kutaja zawadi walizopata washindi huku akiahidi kuboresha eneo la zawadi kwa msimu ujao.
Timu za kimara haziwez kuwafunga timu kama Midizini Mabibo, Mburahati huku ni uswahilini na madogo wanapiga boli kweli, kimara Shimbonii mashishaaa nyingi na hawa ndugu zetu na mpira ni tofauti kidogo ππππ