Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Mshukiwa alirejea nyumbani akiwa amechelewa na hivyo kumlazimu mama yake kumuuliza sababu za kukosa kuandaa chajio
Mama huyo anadaiwa kukerwa baada ya mama yake mzazi kumuagiza kuwaandalia wanawe chajio ambao tayari walikuwa wamelala bila kula. Alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga malaika hao wawili wenye miaka saba na miwili
Winfred pia alijaribu kumuua mama yake mzazi lakini alimshinda nguvu na kumtupa nje ya nyumba
Mshukiwa aamekuwa akitishia kuwaua watoto hao kabla ya kisa hicho
Polisi katika Kaunti ya Nairobi wanachunguza kisa ambapo mama mmoja mwenye umri wa miaka 24 aliwadunga kisu na kuwaua wanawe wawili Jumamosi, Mei 2 usiku, katika mtaa wa Kayole.
Mshukiwa aliyetambuliwa kama Winfred Nduku, anadaiwa kukerwa baada ya mama yake kumuagiza kuwaandalia wanawe chajio ambao tayari walikuwa wamelala bila kula.
Mshukiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Mama Lucy. Picha: UGC.
Nduku alirejea nyumbani akiwa amechelewa huku akiwa kwenye simu na hivyo kumlazimu mama yake kumuuliza sababu za kukosa kuandaa chajio kama ilivyoripoti CitizenTV.
Ni katika harakati hiyo ndipo alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga malaika hao wawili wenye miaka saba na miwili, kisha kujaribu kujitoa uhai na kisu hicho.
Picha ya wakazi wakitazama kisa cha awali Kayole. Nduku alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga kisu watoto wake Picha:UGC.
Baada ya kutekeleza maovu hayo, Winfred pia alijaribu kumuua mama yake mzazi lakini alimshinda nguvu na kumtupa nje ya nyumba.
Watoto hao walikimbizwa hospitalini lakini tayari walikuwa wamekata roho kutokana na majeraha.
Mama yake mshukiwa aliwaambia maafisa wa polisi kuwa binti yake amekuwa akitishia kuwaua watoto hao kabla ya kisa hicho cha Jumamosi.
Kamanda wa Polisi Kaunti ya Nairobi, Philip Ndolo alisema kwa sasa mshukiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Mama Lucy na atakabiliwa na mashtaka ya uhalifu baada ya kupona.
Chanzo: tuko.co.ke
Mama huyo anadaiwa kukerwa baada ya mama yake mzazi kumuagiza kuwaandalia wanawe chajio ambao tayari walikuwa wamelala bila kula. Alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga malaika hao wawili wenye miaka saba na miwili
Winfred pia alijaribu kumuua mama yake mzazi lakini alimshinda nguvu na kumtupa nje ya nyumba
Mshukiwa aamekuwa akitishia kuwaua watoto hao kabla ya kisa hicho
Polisi katika Kaunti ya Nairobi wanachunguza kisa ambapo mama mmoja mwenye umri wa miaka 24 aliwadunga kisu na kuwaua wanawe wawili Jumamosi, Mei 2 usiku, katika mtaa wa Kayole.
Mshukiwa aliyetambuliwa kama Winfred Nduku, anadaiwa kukerwa baada ya mama yake kumuagiza kuwaandalia wanawe chajio ambao tayari walikuwa wamelala bila kula.
Mshukiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Mama Lucy. Picha: UGC.
Nduku alirejea nyumbani akiwa amechelewa huku akiwa kwenye simu na hivyo kumlazimu mama yake kumuuliza sababu za kukosa kuandaa chajio kama ilivyoripoti CitizenTV.
Ni katika harakati hiyo ndipo alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga malaika hao wawili wenye miaka saba na miwili, kisha kujaribu kujitoa uhai na kisu hicho.
Picha ya wakazi wakitazama kisa cha awali Kayole. Nduku alikimbia jikoni, kuchukua kisu na kuanza kuwadunga kisu watoto wake Picha:UGC.
Baada ya kutekeleza maovu hayo, Winfred pia alijaribu kumuua mama yake mzazi lakini alimshinda nguvu na kumtupa nje ya nyumba.
Watoto hao walikimbizwa hospitalini lakini tayari walikuwa wamekata roho kutokana na majeraha.
Mama yake mshukiwa aliwaambia maafisa wa polisi kuwa binti yake amekuwa akitishia kuwaua watoto hao kabla ya kisa hicho cha Jumamosi.
Kamanda wa Polisi Kaunti ya Nairobi, Philip Ndolo alisema kwa sasa mshukiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Mama Lucy na atakabiliwa na mashtaka ya uhalifu baada ya kupona.
Chanzo: tuko.co.ke