Kwani kuitwa mme mtarajiwa ni kutongozwa? Mkuu unahitji lecture ya kutofautisha kati ya taarifa na kutogozwa! Kaka hapo umepewa taarifa so act now kadiri ya moyo wako. Be serious man
Sina imani na huyo binti. Mmekutana mara moja tu katika basi anaanza meseji hizo! Isitoshe ulimpa namba yako ya simu ya nini kama hukuwa ukikaribisha mawasiliano baada ya hapo? Uamuzi unao mwenyewe, kusuka au kunyoa. Ila kama ushauri, achana naye...
Kama ulimpa simu yako ili muwasiliane sasa unataka tukusaidie nini si muwasiliane kwamba wewe humtaki atafute mwingine. usimshitaki mtu wakati ulimkubalia mkapeana simu, unamvunjia heshima yake. kumbuka kwamba naye ana hisia kama zako, kama huna time naye mweleze ataacha.
Kwetu tunaamini ng'ombe akija mwenyewe nyumbani hakuna kufukuza ni bahati unakamua, kaka kama una demu ukute hiyo ndiyo fursa pima mzigo kama unafaa beba ila usikamue halafu ukamwacha kihuni si vizuri ila pia usiingia kichwa kichwa utajuta kaka maradhi. sikia ushauri wa watu humu wanavyokwambia then changanya na zako kama mbayuwayu alivyowahi sema Dk. JK.
Zingatia malengo kaka, kwamba mnapiga msuli sana haina mantik katika swala zima la mahusiano na ndoa.
labda anakutengenezea mazingira ujikute unatafuta nauli ya Loliondo
mimi hapo kaka sioni shida , cha kufanya kama na wewe unampenda lakini jenga nae kwanza mazoea kama rafiki kwanza ukiwa unamsoma tabia halafu baadae ndo muendelee kwenye nyanja nyingine kama ukiona mwaendana. Kila la kheri kaka yangu