Binti sokwe.

Binti sokwe.

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Njaa ilipozidi huko Gombe, wazee wakakaa kikao ili kupata ufumbuzi. Baada ya majadiliano ya muda mrefu, wakakubaliana watafute sokwe mrembo. Wamkate mkia na kumremba na kisha wamuoze kwa binadamu. Walijua kuwa binti yao huyo atawapa access ya kula mahindi kwenye shamba la binadamu kirahisi.

Wakafanya hivyo, wakampata binti mrembo, wakamkata mkia na kumpamba sana. Hata hakujulikana kama ni sokwe. Binti yule akajipitisha kwa mkulima mmoja mkubwa bachela aliyeitwa Maduhu. Maduhu akampenda na kumuoa.

a90eda91feec39337bf092232fe1db63.jpg
 
Sasa binti sokwe baada ya kuolewa akawa msaada mkubwa kwa sokwe wenziwe. Aliwaambia mahali ilipo mitego, na kuhusu ratiba ya Maduhu kuwepo shambani. Sokwe wale walikula wakashiba. Habari ya njaa ikawa haipo tena.
_G7H7895.jpg
 
Baada ya muda kidogo, sababu ya kupendwa sana na Maduhu, kiburi kikaanza kumjaa binti sokwe. Akajiona yeye ndiyo yeye. Akaona kama wale sokwe wenzake ni washenzi. Wanamaliza mahindi yao bure. Akaanza kuwafanyia visa. Akimwambia Maduhu muda watakaokuja shambani. Huku akiwadanganya mahali ilipo mitego.
4_CATERS_MONKEYS_WITH_A_WARDROBE_05-305x449.jpg
 
Ila maduhu chizi kweli...yaani hakuona hata mbususu ni tofauti na mbususu za binadamu..au maduhu hakuwahi kuto***?
 
Basi wazee wakakaa kikao, wakamtuma mjumbe mmoja aliyeitwa Pascalina kwenda kwa binti sokwe kuuliza mbona mambo yamebadilika. Mama yake Binti Sokwe akamwita Pascalina pembeni na kumpa ujumbe wake kwa binti sokwe, akimsihi sana amwambie asiwasahau na akumbuke alipotoka na kuwa yeye ndiye alimzaa. Pascalina akavalia nadhifu na kufunga safari hadi kwenye makazi ya Binti Sokwe. Binti Sokwe hakumruhusu hata kuingia ndani ya uzio, aliongea naye akiwa upande wa nje. Pascalina alimueleza kuwa wazee wanauliza kwa nini hali imebadilika tofauti na makubaliano? Na kama kuna mabadiliko kwanini asiwape taarifa na badala yake wanapata habari za uongo na wanaishia kupigwa, kuumizwa na hata kuuwawa?
Binti Sokwe akamwambia Pascalina, "Kawaambie wazee zama za kula bila kufanya kazi zimepitwa na wakati. Watafute kazi za kufanya." Na akaendelea kusema kuwa yeye amefika mafanikio yale sababu ya akili na uzuri wake, na kama kuna kitu walimsaidia tayari amekwisha walipa. Pascalina akasikitika sana. Mwishowe akauliza, "Vipi na mama yako, nimjibu nini?". Binti Sokwe akajibu, "Mwambie kunizaa isiwe sababu. Hata mimi ningetangulia ningemzaa." Pascalina akajiondokea kwa masikitiko, machozi yakimlengalenga, kichwa kainamisha chini. Alipofika karibu na kijiji chao moyo wake ukawa mzito kabisa, hakujua atawaeleza nini kijijini, hasa mama yake na Binti Sokwe. Nguo alizovaa akaziona nzito, akavua na kukaa chini akisikitika.
istockphoto-170615395-612x612.jpg
 
Mwishowe Pascalina akapata ujasiri, akainuka na kuelekea kwenye uwanja ambao Sokwe walikusanyika wakisubiri majibu. Waliposikia majibu ya Binti Sokwe, hasa majibu kwa mama yake, walipandwa na hasira kali sana. Mama yake Binti Sokwe alianguka na kuangua kilio kikubwa sana huku akigaragara. Mwenyekiti wao, bwana Seif alikasirika sana na aliongea kwa jazba kubwa huku akitetemeka. "Huku ni kutukosea adabu na matusi. Tutafute kazi ya kufanya! Kazi ya kutunza misitu hii nani anaifanya? Siyo Maduhu na watu wengine wamepora sehemu ya misitu yetu na kuiharibu! Halafu leo wanasema tutafute kazi! Tulikuwa na kila aina ya matunda, tulikula na kusaza. Tutafute kazi! kuna mtu hapa hataki kazi? kuna mtu hapa haamki asubuhi na mapema kujishughulisha kutwa nzima?" Sokwe wote walikaa kimya, lakini walitikisa vichwa kuonyesha kukataa. "Nani hapa hakumbuki tulivyolima na kula matikikiti hadi kusaza? eneo letu zuri la kulima matikiti lipo wapi leo?" Aliuliza Bwana Seif kwa sauti ya majonzi. Hapo sokwe wote waliguna kwa uchungu. Kumbukumbu ya jinsi walivyokuwa wakila matikiti hadi kusaza iliwaumiza moyo.
sokwe1.jpg
sokwe 6.jpg
sokwe 3.jpg
sokwe 2.jpg
sokwe5.png
soke 4.jpg
 
Baada ya kusikitika na kunung'unika, Seif akawageukia wananchi wake na kuwauliza nini kifanyike. Mawazo mengi yalitolewa. Wengine wakipendekeza kuhama, wengine wakisema waanzishe vita na mawazo mengine mengi. Sokwe mmoja mzee kwa jina Uswege akasimama na kutoa maoni yake, alisema. "Mi naona kabla ya kufikiria ni jambo gani tutafanya kwanza tumuadhibu huyu msaliti, tukomeshe kwanza jambo hili. Tumpelekee mkia wake!" "Kweli kabisa, kweli kabisa." zilisikika kelele kubwa sana. "Tumpelekee kia lake, tumpelekee kia lake," alianza kuimba Uswege. Sokwe wote wakaitikia.

Tumpelekee kia lake, tumpelekee.
Hata kama anaoga,
Rumpelekee kia lake tumplekee.
Hata kama amelala,
Tumpelekee kia lake, tumpelekee.
Hata kama anakula,
Tumpelekee kia lake, tumpelekee.

Basi hapo mambo yakafanyika haraka haraka, mkia wa Binti Sokwe ukaletwa. Maandamano makubwa yakaanza kuelekea kwa Binti Sokwe huku wimbo huo ukiimbwa kwa sauti kubwa sana. Muda huo Binti Sokwe alikuwa amekaa mezani na Maduhu wakila. Kadri sokwe wale walivyokuwa wanakaribia huku wakiimba, Binti Sokwe akaanza kuona mabadiliko. Kwanza mwili ulianza kumuwasha, mara nywele zikaanza kumuota miguuni. Walivyozidi kukaribia, ndivyo nywele nazo zilivyozidi kuota. Mara mkia nao ukaanza kuota, hata hakuweza kukaa vizuri. Maduhu akashangaa kuona mkewe akihangaika kitini.
Sasa sauti za sokwe wanaoimba zikaanza kusikika, nywele zikamfika Binti Sokwe usoni. Maduhu akaruka kitini akimwaga chakula, akasimama amepigwa na butwaa. Kelele za sokwe zikazidi kukaribia, ni kama walikuwa nje ya nyumba ya Maduhu. Binti Sokwe akainuka na kukimbia, huku nyuma mkia wake wote ukiwa umemsimama. Hakuonekana tena hadi leo.
 
Pia Msisahau kuistall maktaba app kutoka playstore ili kusoma vitabu mbalimbali. Kusoma ni bure. (hii hadithi haipo humo)
 
Back
Top Bottom