Binti wa dukani ana mimba, aendelee kubaki ama aondoke?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Wenye maduka nawaombeni msaada wenu.

Nimeajiriwa lakini nina biashara za pembeni likiwemo duka ambalo nimemweka binti, mshahara wake ni laki 1 pamoja na elf 4 ya kila siku (chakula, nauli, choo)

Kwa sasa karibu wiki 6 mfululizo lazima siku moja ya kazi anaenda clinic hafungui siku nzima, mfano wiki hii juzi siku ya jumanne hajafungua kabisa.

Baada ya kukaa chini na kutafakari, hilo suala la clinic nikaona lisiwe shida acha aende tu kwasababu hospitali za serikali kuna foleni.

Ila shida inakuja kwamba aliempa mimba ni kijana wa chuoni, kuna dalili zote kwamba hataweza kuhudumia mtoto, litakuwa ni jukumu lake binti peke yake na hili linanipa hofu zaidi endapo akabanwa kiuchumi ashawishike kunipiga.
 
Mkuu kwa mujibu wa sheria za kazi,huwezi kumbagua kwa sababu ya kuwa na mimba
 
Tafuta mbadala.

Kliniki gani kila wiki? Ana complications zozote? Mimba ina muda gani kwa sasa?
 
Hakuna clinic za kila week,

#2. Hii post umeiba ipo humu humu jf
Nahisi ana mis carriage ama complications za yeye kwenda kila wiki

Niliwahi kuweka post kama hii,

ila yote kwa yote nipo njia panda
 
Mkuu
Sisi siyo waajiri wake. Mlete hapa atoe dukuduku lake tubalansi stori
 
Mabinti muwe makini hii changamoto naiona sana kwa mabinti wengi wa madukani. Vijana wana kauli yao moja inasema, ukiajiri binti umewasogezea wajuba mke.
 
Muache akae---fikiria ni mtoto wako wa kike au dada yako.Tafuta mtu wa kubadili akiwa 3rd trimester na umshirikishe,.
Pole,ndio changamoto za maisha.
 
Ongea nae mwambie,tumekaa mwaka mzima na tumeaminiana,hivyo kwa hali ilipofikia naomba nikutoe uende nyumbani ukSikilizie jambo lako,na Mwenyezi Mungu atakapofanya heri yake utarudi kama mazingira yataruhusu.
 
ndio tafuta loophole umkatae ila sio kigezo ana mimba ..hiyo ni ishakuwa tabulele laa yako😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…