Binti wa Kichaga- tuijiandaaje kwa Posa?

Binti wa Kichaga- tuijiandaaje kwa Posa?

Twilumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2010
Posts
12,576
Reaction score
14,522
Habari wanajamvi!
Nina ndugu yangu wa karibu sn amebahatika kupendana na binti wa kichaga. Wapo katika hatua za awali kwenda kupeleka posa huko Marangu kwa wazazi wa huyu dada!

Swali:
Je tujiandaeje kwa ajili ya kupeleka posa hiyo kwa namna nyingine ni vitu gani tuviandae ikiwa ni pamoja na vile vya kimila ili kufanikisha zoezi hili muhimu tusije kosa mke!

Naomba kuwasilisha kwa mchango!
Asante.
 
mbege lazima kama debe tano,mbuzi. vingine nimesahau ngoja wadau wafike.
 
Habari wanajamvi!
Nina ndugu yangu wa karibu sn amebahatika kupendana na binti wa kichaga. Wapo katika hatua za awali kwenda kupeleka posa huko Marangu kwa wazazi wa huyu dada!

Swali:
Je tujiandaeje kwa ajili ya kupeleka posa hiyo kwa namna nyingine ni vitu gani tuviandae ikiwa ni pamoja na vile vya kimila ili kufanikisha zoezi hili muhimu tusije kosa mke!

Naomba kuwasilisha kwa mchango!
Asante.

Ana nyumba huyo, ana gari huyu, akaunti yake ya benki iko sawia, anafanya kazi gani na asisahau kubeba kuwa na kadi ya NBC Master Card! Natania mkuu ila kwa ushauri wangu ni kwamba mtafuteni mzee wa kichaga mmarangu atawajuza juu ya mambo yao ya kikabila la marangu
 
mbege lazima kama debe tano,mbuzi. vingine nimesahau ngoja wadau wafike.
Debe tano ni zamani, last month tulimsindikiza mkaka mmoja kupeleka posa nkashangaa manake aliambiwa mbege debe 48, mbuzi 5, na makorokoro kibao. Kwa mahesabu ya haraka anahitajika kupeleka kama 1m na zaidi manake wamempigia mahesabu ya debe 1 ya mbege times 48.. Na hapo huyo binti wanaishi wote na wamepata mtoto mmoja ( ana 6 month)...huko ni marangu pia.
 
msisahau mgolele wa babu na kilemba cha bibi
 
Debe tano ni zamani, last month tulimsindikiza mkaka mmoja kupeleka posa nkashangaa manake aliambiwa mbege debe 48, mbuzi 5, na makorokoro kibao. Kwa mahesabu ya haraka anahitajika kupeleka kama 1m na zaidi manake wamempigia mahesabu ya debe 1 ya mbege times 48.. Na hapo huyo binti wanaishi wote na wamepata mtoto mmoja ( ana 6 month)...huko ni marangu pia.

hizo debe 48 wanakunywa ukoo mzima?
 
Mbege na ndafu lazima, maana ulabu ni kama kupiga mswaki kwa maji
 
msisahau mgolele wa babu na kilemba cha bibi


Asante mkuu ndyoko hii hata kule kwetu ipo, tutazingatia! Ingawa kule kwetu huwa rangi zinazingatiwa pia!
 
hizo debe 48 wanakunywa ukoo mzima?

we si unataka mke, toa tu hizo debe 48 usitake kujua wanakunywa wangapi. Toa hiyo pombe chukua kinyoya chako yaishe uende ukaanzishe genge then duka mtoto akuletee maendeleo na maisha yaendelee. Wamarangu wako poa tu hawana kwere!
 
we si unataka mke, toa tu hizo debe 48 usitake kujua wanakunywa wangapi. Toa hiyo pombe chukua kinyoya chako yaishe uende ukaanzishe genge then duka mtoto akuletee maendeleo na maisha yaendelee. Wamarangu wako poa tu hawana kwere!

Tutatoa mkuu!
 
mwaka huu umekuwa wa wachanga
haya endeleeni kuwadadavua.

Japo naamini unachangamsha baraza
sababu ana wazee wake wanaweza kufuatilia vizuri.
 
Jiandae na Mbege na Debe 20 hivi za kunywa Ndugu, Jamaa na Marafiki na Mjirani, Blanketi la Bibi, Kuna vitenge vya Mashangazi, Mbuzi kadhaa na Bia Kreti kama tano hivi
 
mwaka huu umekuwa wa wachanga
haya endeleeni kuwadadavua.

Japo naamini unachangamsha baraza
sababu ana wazee wake wanaweza kufuatilia vizuri.

JF ni zaidi ya uifikiriavyo!
 
hizo debe 48 wanakunywa ukoo mzima?
Ukoo mzima pia bado hawatazimaliza, labda wanawagawia na majirani...afu hawataki mbege live, wanataka pesa mf. Debe 1 inauzwa sh elfu 30, unafanya 30'000 times 48 then unawapa cash yao... Papo kwa hapo zilinunuliwa debe 5 za ukweli afu ndio akaambiwa hizo 48 zilizobakia alete pesa... Ila labda itakuwa ni tofauti kati ya ukoo na ukoo..
 
Huku huwa hawatoi kaniki ya bibi?
 
Back
Top Bottom