#COVID19 BioNTech yaomba kibali cha matumizi ya chanjo kwa watoto wadogo

#COVID19 BioNTech yaomba kibali cha matumizi ya chanjo kwa watoto wadogo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1643868397573.png

Kampuni ya nchini Ujerumani ya teknolojia ya biolojia - BioNTech pamoja na mshirika wake wa kimarekani, Pfizer, wameomba kibali cha dharura nchini Marekani, cha matumizi ya chanjo dhidi ya virusi vya corona kwa watoto wa chini ya miaka mitano.

Makampuni hayo mawili yamesema kuwa chanjo hiyo itaweza kutumiwa kwa wajili watoto wachanga kuanzia umri wa miezi sita. Ikiwa Taasisi ya Marekani ya usalama wa chakula na dawa, FDA itaridhia kibali hicho, chanjo ya BioNTech itakuwa ya kwanza duniani kwa watoto wa umri huo.
 
Beberu bana, yaani wamekomaa. Sasa watatuletea variety ya kirusi kitakachoua watoto wadogo, ambayo tutake tusitake tutawachanja la sivyo kadibya clinic inakuwa na mapungufu!

Nimesikia tetesi uvumi mahali eti vijijini huko wamama wakipeleka watoto wao kupata zile chanjo za awali wanalazimishwa na wao mama au Baba kuchanjwa COVID. Sijui kuna ukweli??
 
Kuna sehemu nimeskia ukichanjwa unapewa 10000 hp Jijini,nimeambiwa na majirani zangu wawili.
Kazi iendelee kwa juhudi
 
Back
Top Bottom