SoC01 Bodaboda na hatari iliyoko mbele yetu kama Taifa

SoC01 Bodaboda na hatari iliyoko mbele yetu kama Taifa

Stories of Change - 2021 Competition

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,290
Reaction score
2,468
bodaboda.png

Hii picha nimeitoa mtandaoni

Ipo changamoto inayoonekana kwa sasa kukua kwa kasi sana na ambayo isipofanyiwa kazi mapema basi tutakuwa na watoto/vijana wengi wenye matatizo ya kifua. Kwa sasa wimbi la bodaboda limeshika kasi. Ndio usafiri wa watu wa kati katika kuwahi shughuli zao za kila siku. Kama tunavyojua unapopanda kwenye huu usafiri, mwili wako unakuwa nje, na lolote linaweza kutokea, iwe ajali au maradhi kama mafua, kikohozi, na hata pneumonia.

Mimi ni mwendeshaji wa pikipiki. Wakati fulani nyuma huko niliwahi kupatwa na huu ugonjwa wa pneumonia. Ulinitesa sana. Ni kutokana na baridi kupiga kifuani na usoni hasa pale ambapo hujajikinga vyema.

Sasa kuna hawa watoto ambao wameanza chekechea. Wengi pia utakuta shule zao ziko mbali, na kusema wazazi watumie usafiri wa umma ni kwamba mtoto atachelewa. Wakisema mtoto atumie basi la shule, ni kwa wale wenye uwezo, na shule zenye aina hiyo ya usafiri. Hivyo basi kuna kundi la wazazi wameingia makubaliano na madereva wa boda boda kwa lengo la kuwapeleka watoto wao mashuleni asubuhi na kuwafuata mchana au jioni.

Ieleweke kwmba watoto hawa ni kati ya miaka minne hadi kumi hivi. Sasa kwa usalama ni kwamba dereva wa bodaboda humuweka mbele yake kama inavyoonekana kwenye picha hapo. Mtoto hana kinga yoyote usoni wala mwilini. Tena kwa nyakati za asubuhi hali ya hewa huwa na ubaridi sana. Pia ukiongezea na mwendo wa madereva hawa wa bodaboda njiani basi inakuwa tabu sana.

Njiani wiki kama mbili nikiwa nami kwenye pikipiki yangu dereva wa bodaboda akawa kampakiza mama mmoja ambaye alikuwa na watoto wawili. Mmoja kakaa nae na mwingine yuko mbele ya dereva. Ilibidi kuongeza mwendo ili nimfikie yule dereva na kumpa ishara kuwa huyo mtoto hapo mbele anaathiriwa na upepo. Watafute namna ya kumkinga. Mama yake anatoa macho tu. Dereva wa bodaboda kama alinielewa akachukua begi kama la shule na kumuwekea kifuani lakini inavyoonekana ni kama halikukaa vizuri. Nadhani aliliondoa. Mimi nikaongeza mwendo, la msingi ujumbe niliwafikishia.

SIku tatu tena hivi zimepita nikamwona dereva wa bodaboda kampakiza mtoto wa miaka minne hivi mbele. Japo kavaa sweta, bodaboda ilikuwa kasi sana kiasi unaona kabisa mtoto anapata shida kutazama mbele. Bado kwa sweta lile na mwendo ule ni ngumu kumkinga mtoto na athari za upepo hasa ukitegemea umri wao.

Kwa mwendo huu tunatengeneza janga lingine. Nashauri pawepo na taratibu zinazoeleweka za usafiri wa vyombo hivi hasa linapokuja suala la watoto. Ikiwezekana pawepo na helmet za watoto, lakini pia wazazi wahahikishe watoto wao wanakuwa salama katika vyombo hivi. Ni ngumu kuzuia vyombo hivi kutumika ila ni rahisi kudhibiti matumizi na kujali wengine pale wanapotumia vyombo hivi.

Nasisitiza kwa wazazi, wasiangalie tu mtoto kuwahi shule. Wahakikishe usalama wa watoto wao wanapokuwa wanaenda shule. Unaweza kufurahia mtoto kuwa anawahi lakini baada ya muda ukaanza kuwa mhudhuriaji mzuri wa mahospitali. Tuwe makini.

Updates: Hiyo clip nimeiweka hapa baada ya kuiona mitandaoni. Hii inakuja baada ya kuwa tayari nimewekahili bandiko hapa, hivyo waandaaji wa huu mchakato jaribuni kufanyiakazi nilichosemakwenye post yangu chini huko
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2021-08-17 at 21.47.42.mp4
    14.9 MB
Upvote 8
Miongoni mwa vitu navyokerwa na baadhi ya bodaboda ni pale wanapopita njia za wapita kwa miguu spidi kubwa na honi nyingi nyingi za kijinga.
Miundombinu ya barabara imejengwa kufuatana na watumiaji.Njia za wapita kwa miguu ziheshimiwe.Hii issue ni 'comon' sana kwa jiji la dar es salaam.Wakati mwingine kimesababisha ajali zisizo na sababu.

Nashukuru mtoa mada umeliona hilo kuwa ttz
 
Miongoni mwa vitu navyokerwa na baadhi ya bodaboda ni pale wanapopita njia za wapita kwa miguu spidi kubwa na honi nyingi nyingi za kijinga.
Miundombinu ya barabara imejengwa kufuatana na watumiaji.Njia za wapita kwa miguu ziheshimiwe.Hii issue ni 'comon' sana kwa jiji la dar es salaam.Wakati mwingine kimesababisha ajali zisizo na sababu.

Nashukuru mtoa mada umeliona hilo kuwa ttz
Pamoja sana
 
Nimeona clip moja jana kupitia group ya whatsapp kuwa traffick police mmoja akizungumzia jambo hili hili. Bahati mbaya simu yangu leo imevunjika nilitaka kutupia hiyo clip hapa. Nilichoandika na alichoongea ni asilimia mia. Sasa JF mtuambie, haya mawazo yetu huwa mnayagawa kisekta? Hii clip ni very recent kulinganisha na mada hii. Hivyo nawasihi sana JF kindly consider impact ya hii mada. Huwezi kujua hawa jamaa walipita humu ndio akapata wazo la kukuza mada yao waliyoongelea

Pia natoa wito kwa JF kutozingatia sana mfumo wa kupigiana kura kwa kuwa sio mfumo objective kabisa. Hamuwezi kupata mnachotaka kama utaratibu ndio huo. Angalieni mada iliyopo na uzito wake kwa jamii. Mfano mdogo tu ni hiki nilichoandika hapo na reaction toka jeshi la polisi usalama barabarani.
Kama kuna mdau ameiona hiyo clip tafadhali muiweke hapa.

Mwisho nina imani kuwa sitakosekana kwenye tatu bora za washindi 😉
 
Wakuu nimepata ile clip na nimeiweka hapo juu kwa ufafanuzi zaidi
 
Kwa kweli hili suala la bodaboda ni pasua kichwa ingawa mambo mengine yanasababishwa na uelewa wetu mdogo juu ya matumizi sahihi ya hivi vyombo.

Watanzania wengi tunachojali ni kupanda tu chombo basi bila kujali kama tumekaa kwa usalama.

Afya ni jambo muhimu na huzorota kwa kusababishwa na mkisanyiko wa kutokujali mambo madogomadogo kama haya.
 
Kwa kweli hili suala la bodaboda ni pasua kichwa ingawa mambo mengine yanasababishwa na uelewa wetu mdogo juu ya matumizi sahihi ya hivi vyombo.

Watanzania wengi tunachojali ni kupanda tu chombo basi bila kujali kama tumekaa kwa usalama.

Afya ni jambo muhimu na huzorota kwa kusababishwa na mkisanyiko wa kutokujali mambo madogomadogo kama haya.
Kweli kabisa. Nimeenda shule moja ya chekechea anayosoma mwanangu, mwalimu mkuu nae analalamika kuhusu wazazi kuwatmia sana hawa bodaboda kwani licha ya madhara ya kiafya niliyotaja, anasema pia kuna suala la udhalilishaji wa kingono
 
Back
Top Bottom