Bodaboda wa Tanzania wanafiki kama Wajumbe CCM

Bodaboda wa Tanzania wanafiki kama Wajumbe CCM

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,935
Hawana tofauti na zile kampuni za kukodishwa kulia na kuomboleza misibani!

Ambao huweza kulia kwa machozi tosha,ilhali hata Marehemu mwenyewe hawakuwahi kumuona kavla ya kufariki. Achilia mbali hata unasaba!

Kwao Boda oda, huangalia ujazo wa matenki ya Pikipiki(Bodaboda) zao! Wako tayari kutumika na chama chochote cha siasa, ilimradi mshiko wao uwepo tu.

Kwenye kipindi cha Kampeni, bodaboda mmoja,anaweza Participate misafara ya vyama tofauti hata vitatu kwa siku moja!

Hawajali kuhusu sera,hoja wala uelewa wa kile wanachokwenda kukiandamani,wao ni sera ya kujaziwa Mafuta tu.

Baada ya kufika eneo husika, huwa hawasubiri kusikiliza, hoja au sera za yule aliyewajazia Mafuta.

Huwa wanawahi vituoni kwao,ili wakayatumie yale Mafuta na kupata pesa zao.

Hoja yangu,wanasiasa wenye mtindo wa kuwajazia mafuta bida boda,wajuwe huwa wameliwa!

Na pia waelewe kwamba wananchi wanajua huo mchezo,kwa hiyo,huwa haileti ushawishi wowote kwa mwananchi kuweza kuhadaika!

Labda kwa vyama ambavyo huwa vina chukua video clips na kutuma kwa wafadhili wao,kuwahadaa kwamba wana uungwaji mkono kindakindaki,ilhali ukweli ukiwa tofauti.

Ndio maana nimewafananisha na wajumbe wa chaguzi mbalimbali za CCM,ambao hupokea pesa toka kwa kila mgombea huku wakimuhadaa kwamba wako nyuma yake mpaka kieleweke. Mwisho wa siku huwa ni kumbwaga chali mhusika

Jiwe hili ni kwa wanaohusika

Alamsikhi.
10101.
 
Kwani wewe una tofauti gani na hao bodaboda?Mbona tulishang'amua mapema kuwa ukimaliza siku yako kwa kuandika nyuzi kadhaa za kuwakandia na kuwasagia kunguni wapinzani unalipwa?[emoji23][emoji23]Wewe na hao Boda ni kitu kimoja!
 
Kwani wewe una tofauti gani na hao bodaboda?Mbona tulishang'amua mapema kuwa ukimaliza siku yako kwa kuandika nyuzi kadhaa za kuwakandia na kuwasagia kunguni wapinzani unalipwa?[emoji23][emoji23]Wewe na hao Boda ni kitu kimoja!
Ninalipwa kupitia wapi mkuu!

Kwa hiyo,kila anaesema na kuwapa za uso huwa amelipwa?

Kwa hiyo,post zote tunazoziona humu zina malipo??

Halafu mbona umehamaki ki-vile,au ndio mmojawapo wa Niliowataja humu kwenye Topic yangu?
 
Kwa nini boda boda waliojitokeza kwa Lisu wamekuuma? Boda boda ndo unawaona leo? Mwacheni mama ameamua kuruhusu mageuzi katika nchi, acheni kuumia sasa ni wakati was kuikubali halu mpya iliyoletwa na mama.
 
Kwa nini boda boda waliojitokeza kwa Lisu wamekuuma? Boda boda ndo unawaona leo? Mwacheni mama ameamua kuruhusu mageuzi katika nchi, acheni kuumia sasa ni wakati was kuikubali halu mpya iliyoletwa na mama.
Hayo ni maoni yako,sambamba na ya kwangu!

Hakuna mahala nimetaja jina la taasisi wala chama cha siasa zaidi ya CCM!

Huu ndio ulikuwa wakati muafaka kuliongelea hili,maana kila jambo na wakati wake!

Jiwe la gizani huleta maudhi!
Hasa kwa linaempata sawia.
 
Hawana tofauti na zile kampuni za kukodishwa kulia na kuomboleza misibani!

Ambao huweza kulia kwa machozi tosha,ilhali hata Marehemu mwenyewe hawakuwahi kumuona kavla ya kufariki. Achilia mbali hata unasaba!

Kwao Boda oda, huangalia ujazo wa matenki ya Pikipiki(Bodaboda) zao! Wako tayari kutumika na chama chochote cha siasa, ilimradi mshiko wao uwepo tu.

Kwenye kipindi cha Kampeni, bodaboda mmoja,anaweza Participate misafara ya vyama tofauti hata vitatu kwa siku moja!

Hawajali kuhusu sera,hoja wala uelewa wa kile wanachokwenda kukiandamani,wao ni sera ya kujaziwa Mafuta tu.

Baada ya kufika eneo husika, huwa hawasubiri kusikiliza, hoja au sera za yule aliyewajazia Mafuta.

Huwa wanawahi vituoni kwao,ili wakayatumie yale Mafuta na kupata pesa zao.

Hoja yangu,wanasiasa wenye mtindo wa kuwajazia mafuta bida boda,wajuwe huwa wameliwa!

Na pia waelewe kwamba wananchi wanajua huo mchezo,kwa hiyo,huwa haileti ushawishi wowote kwa mwananchi kuweza kuhadaika!

Labda kwa vyama ambavyo huwa vina chukua video clips na kutuma kwa wafadhili wao,kuwahadaa kwamba wana uungwaji mkono kindakindaki,ilhali ukweli ukiwa tofauti.

Ndio maana nimewafananisha na wajumbe wa chaguzi mbalimbali za CCM,ambao hupokea pesa toka kwa kila mgombea huku wakimuhadaa kwamba wako nyuma yake mpaka kieleweke. Mwisho wa siku huwa ni kumbwaga chali mhusika

Jiwe hili ni kwa wanaohusika

Alamsikhi.
10101.
Hata kahaba huwa na upendo kwa baadhi ya wanaume anaolala nao.... hutamani kuwarudia ingawa wanaume hawanaga muda tena. We kahaba chadema haina muda na wewe unaiwaza sana.
 
Back
Top Bottom