ibanezafrica
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,261
- 6,553
Natumaini wana bodi nao huwa wanatazama hizi mechi hasa za Nbc Premier League. Najua na wao wanaona kama tuonavyo sisi, wanapata muda wa kutafakari, kuchambua kati ya pumba na mchele.
Basi tuombe kwa nafasi zao wasiishie kuguna guna, bali utokeapo utata na sintofahamu katika matokeo ya mchezo na maamuzi ya waamuzi tata wao kama bodi wafike mbali zaidi, ikiwezekana hata kuwatumia TAKUKURU ili kuunusuru mchezo wetu pendwa wa kandanda.
Na itapendeza itokeapo timu mbili zimehusika kwenye mchezo mchafu wa kupanga matokeo timu zote zipate adhabu ya kushushwa daraja, zikacheze ligi daraja la kwanza zigombee kurudi tena Premier.
Nayasema haya ili kuokoa mchezo huu, kuuletea heshima, lakini pia kuzipa changamoto timu zifanye maandalizi mapema, usajiri mzuri na si kushindwa kusajiri vizuri na mwishowe kuanza kutumia njia za ujanja ujanja kununua waamuzi na kuhonga wachezaji.
Bodi ya ligi hili mlitazame sasa.
Nawasilisha.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Basi tuombe kwa nafasi zao wasiishie kuguna guna, bali utokeapo utata na sintofahamu katika matokeo ya mchezo na maamuzi ya waamuzi tata wao kama bodi wafike mbali zaidi, ikiwezekana hata kuwatumia TAKUKURU ili kuunusuru mchezo wetu pendwa wa kandanda.
Na itapendeza itokeapo timu mbili zimehusika kwenye mchezo mchafu wa kupanga matokeo timu zote zipate adhabu ya kushushwa daraja, zikacheze ligi daraja la kwanza zigombee kurudi tena Premier.
Nayasema haya ili kuokoa mchezo huu, kuuletea heshima, lakini pia kuzipa changamoto timu zifanye maandalizi mapema, usajiri mzuri na si kushindwa kusajiri vizuri na mwishowe kuanza kutumia njia za ujanja ujanja kununua waamuzi na kuhonga wachezaji.
Bodi ya ligi hili mlitazame sasa.
Nawasilisha.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app