HPAUL
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 410
- 567
Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi VPL amesema TFF inafanyia kazi maoni ya Mh. Rais Magufuli, na ligi itarejea Juni bila ya watazamaji.
======
ALMAS Kasongo, Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) amesema kuwa wanakwenda kuifanyia kazi kauli ya Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli.
Jana, Aprili 3, Magufuli alisema kuwa anafikiria kurejesha ligi za Tanzania ambazo zilisimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona.
Kasongo amesema Kamati ya Uongozi ya TFF imeazimia kuwa ligi iendelee kulingana na maelekezo ya Serikali na mechi zitachezwa bila mashabiki kuanzia mwezi Juni mwaka huu.
======
ALMAS Kasongo, Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) amesema kuwa wanakwenda kuifanyia kazi kauli ya Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli.
Jana, Aprili 3, Magufuli alisema kuwa anafikiria kurejesha ligi za Tanzania ambazo zilisimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona.
Kasongo amesema Kamati ya Uongozi ya TFF imeazimia kuwa ligi iendelee kulingana na maelekezo ya Serikali na mechi zitachezwa bila mashabiki kuanzia mwezi Juni mwaka huu.