Bodi ya ligi watumieni waamuzi toka Zanzibar

Bodi ya ligi watumieni waamuzi toka Zanzibar

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Wakati wakiendelea kulalamikiwa na wakati semina yao ikiendelea bado wameendelea kutuacha vinywa wazi kwa maamuzi yao tata.

Mechi ya juzi ya Yanga dhidi ya Biashara tumeshuhudia yanga akinyimwa magoli mawili clear kabisa eti mfungaji alikua ameotea!..hili limeshangaza wengi...hata ukitazama replay yake unajiuliza offside ilikua wapi?

Hawakuishia hapo mechi ya jana baina ya Simba na Ruvu goli la kwanza aliloshinda simba na lingine hapo la Chama ilikua ni clear offside lakini waamuzi wetu wakayaona kuwa ni magoli halali!. si kama naandika kiushabiki lakini waliotazama game hizo zote mbili watakubaliana nami la hasha nakuomba utazame marudio ya mechi hizo.

Mwezi januariy tulioangalia mechi zile zilizochezwa zanzibar mapinduzi tuliridhishwa sana na aina ya uchezeshaji wa waamuzi wa kule visiwani.

Sasa tuombe watu wa bodi muda huu wakati hawa waamuzi wa bara wakiwa semina tuletewe wale kutoka zanzibar watupe burudani
Nawasilisha.
 
Both, yanga na simba ni wanufaika wa mahaba ya referees..Maeneo yanayotumika kuumiza underdogs ni utata wa offside, penalty za jionjion, red card na ongezeko la dk za nyongeza...ukipona kwny hayo umetoboa!
 
dk 0-75 Waamuzi wetu huwa hawana shida sana..shida huanzia robo ya mwisho ya mchezo na endapo timu KUBWA haijafunga...timu kubwa ikiongoza toka mapema huwa hakuna malalamiko...mbona ulaya timu kubwa kama man utd, psg, bayern, au barcelona zinashikwa shati kila leo na 'gwambina' za huko!
 
Screenshot_20220206_194731.jpg.jpg
 
Zanzibar kuna mechi wanatokaga hadi 19 : 3 watu wanapigana hadi magoli 20 bora ata wa bongo
 
Both, yanga na simba ni wanufaika wa mahaba ya referees..Maeneo yanayotumika kuumiza underdogs ni utata wa offside, penalty za jionjion, red card na ongezeko la dk za nyongeza...ukipona kwny hayo umetoboa!
Kweli simba marefa wanatujali sana.
 
Zanzibar kuna mechi wanatokaga hadi 19 : 3 watu wanapigana hadi magoli 20 bora ata wa bongo
Lakini magoli si yalikua halali? Hapo laumu timu km zilipanga matokea, refa anahusikaje na timu kufungana magoli mengi?
 
Ukisema haya pia uwe unaangalia michezo ya kihuni wanayocheza hizo timu unaita underdogs.

Unapolalamikia muda kuongezwa,pia kemea kitendo cha wachezaji kupoteza muda pasipo sababu za msingi.
Lengo la soka ni magoli yafungwe.Muda ukiongezwa,haipewi timu moja kucheza.Hii ni akili ya kijinga sana kulalamikia muda kuongezwa.
Makosa ya offside ni ya kibinadamu,kwa hiyo ukitarajia ucheze offside trick kila saa,unacheza under your own risk.Maana sio lazima mwamuzi aone.Mwamuzi hayupo uwanjani kukulinda wewe usifungwe.Jilinde mwenyewe.Waambieni wachezaji wacheze mpira waache ujinga ujinga.Kama huna uwezo kubali kufungwa tu.
Both, yanga na simba ni wanufaika wa mahaba ya referees..Maeneo yanayotumika kuumiza underdogs ni utata wa offside, penalty za jionjion, red card na ongezeko la dk za nyongeza...ukipona kwny hayo umetoboa!
 
Udini utakuumiza.

Kama wanatenda haki kama malaika,mpira wao ukoje kimataifa?

Mbona wanafanya makosa mengi sana ya kibinadamu?Acheni mambo ya udini,mtaharibu soka mkianza kuingiza itikadi za kidini
Waamuzi wa kule wanatenda haki,wanachukua udhu kwanza kabla ya kuingia mzigoni kwahiyo ni haki bin haki
 
Back
Top Bottom