Wanabodi, kuna tabia inayozidi kuonekana ambapo bodi ya mikopo inatembelea ofisi za watu ikiwa na orodha ya wadaiwa wa mikopo.
Cha kushangaza, orodha hii mara nyingi inajumuisha majina ya watu ambao hawajawahi kuomba mkopo wala kujua chochote kuhusu bodi ya mikopo, kwani walijilipia ada zao kikamilifu tangu mwanzo hadi mwisho wa masomo yao.
Kinachokera zaidi ni kwamba, ukijaribu kuwaomba ushahidi wa mkopo unaodaiwa, kama jina la benki, namba ya akaunti walikoweka mkopo huo, au nakala ya fomu uliyotumia kuomba mkopo, hawana ushahidi wowote. Badala yake, wanakutaka uwape au uwatajie Index Number ya cheti chako cha kidato cha nne.
Na ukifanya hivyo, mara nyingi hukuta kuwa huusiki kabisa na deni hilo. Baada ya hapo, utasikia wakisema, “Samahani, udaiwi.”
Ni muhimu kuwaomba bodi hii ifanye kazi kwa umakini zaidi. Wanapokwenda kudai mkopo, wahakikishe kuwa wana taarifa kamili na sahihi kuhusu wadaiwa badala ya kutegemea bahati nasibu.
Ni jambo linaloleta usumbufu mkubwa kwa watu wasiokuwa na uhusiano wowote na mikopo hiyo.
Hii ni bodi inayosheheni wasomi na wataalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), hivyo inapaswa kuwa mfano wa usahihi na uwajibikaji.
Wanapaswa kuhakikisha kuwa kila hatua wanayochukua imezingatia ukweli wa taarifa walizonazo.
Kwa hiyo, tunasisitiza kwamba wanaodaiwa kweli walipe mikopo yao pamoja na faini wanazostahili. Lakini kwa wale wasiohusika, wasisumbuliwe bila sababu. Tafadhali bodi, simamieni kwa umakini zaidi hili suala
Cha kushangaza, orodha hii mara nyingi inajumuisha majina ya watu ambao hawajawahi kuomba mkopo wala kujua chochote kuhusu bodi ya mikopo, kwani walijilipia ada zao kikamilifu tangu mwanzo hadi mwisho wa masomo yao.
Kinachokera zaidi ni kwamba, ukijaribu kuwaomba ushahidi wa mkopo unaodaiwa, kama jina la benki, namba ya akaunti walikoweka mkopo huo, au nakala ya fomu uliyotumia kuomba mkopo, hawana ushahidi wowote. Badala yake, wanakutaka uwape au uwatajie Index Number ya cheti chako cha kidato cha nne.
Na ukifanya hivyo, mara nyingi hukuta kuwa huusiki kabisa na deni hilo. Baada ya hapo, utasikia wakisema, “Samahani, udaiwi.”
Ni muhimu kuwaomba bodi hii ifanye kazi kwa umakini zaidi. Wanapokwenda kudai mkopo, wahakikishe kuwa wana taarifa kamili na sahihi kuhusu wadaiwa badala ya kutegemea bahati nasibu.
Ni jambo linaloleta usumbufu mkubwa kwa watu wasiokuwa na uhusiano wowote na mikopo hiyo.
Hii ni bodi inayosheheni wasomi na wataalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), hivyo inapaswa kuwa mfano wa usahihi na uwajibikaji.
Wanapaswa kuhakikisha kuwa kila hatua wanayochukua imezingatia ukweli wa taarifa walizonazo.
Kwa hiyo, tunasisitiza kwamba wanaodaiwa kweli walipe mikopo yao pamoja na faini wanazostahili. Lakini kwa wale wasiohusika, wasisumbuliwe bila sababu. Tafadhali bodi, simamieni kwa umakini zaidi hili suala