Bodi ya Mikopo (HESLB) wanakata zaidi ya deni, ukiwafuata unaambiwa omba kurejeshewa kwenye mtandao na usubiri kwa miezi mitatu

Bodi ya Mikopo (HESLB) wanakata zaidi ya deni, ukiwafuata unaambiwa omba kurejeshewa kwenye mtandao na usubiri kwa miezi mitatu

DT125

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2011
Posts
437
Reaction score
637
Makosa wafanye wao kukata zaidi ya deni mnufaika unalodaiwa halafu ukiwafuata wanakupa statement wenyewe inaonyesha kweli umekatwa zaidi. Badala ya kuhakiki deni lako na kukuandika hundi wanakwambia rudi nyumbani na kajisajiri kwenye mfumo udai kurudishiwa makato yaliyozidi.

Wanakwambia subiri baada ya miezi 3 ndipo watapitia kuhakiki malipo yako. Ukiwapigia kuwakumbushia muda umepita simu anapokea afisa mmoja ana kiswahili cha kule ndege ilikotua majini. Anakushambulia kwa maswali kuwa ulieleweshwa usubiri muda gani, utadhani wewe ndiye mwenye makosa kukatwa zaidi ya deni halisi.

Wakati mwingine japo kuna mambo sikukubaliana na mwendazake inabidi nimkumbuke tu. Hivi mama yetu huwezi kuwaambia watulipe ndani ya siku 3 badala ya miezi 3. Hivi Prof Mkenda na hili nalo ukiwambia watulipe ndani ya siku 3 watakugomea mpaka tena uwashitaki kwa Spika?
 
Du pole sana mkuu mie pamoja na kujaza ile refund portal yao kupitia mfumo nilisugua mwaka mzima ndo nikarejeshewa mpunga wangu, hyo wanayosema had baada ya miezi 3 imekaa kisiasa tu, ila kiukweli mojawapo ya Taasisi za serikali zilizo na customer care mbovu ni heslb yaani c Bora hata ww cm walipokea, yaan n wa hovyo kweli wameweka no za simu ila hazipokelewi, wapuuz sana wale jamaa.
 
Hii nchi kila Idara kuna vilio vya Wananchi...

Huyu Mama hata sijui anafanya kazi gani Ikulu...
JK tusaidie huyu mitano inatosha. Kwa sanduku la kura hatuwawezi. Labda tufunge na kuomba muumba mbigu na Dunia ampende zaidi.
 
Naunguliwa Muhimbili hosp. Nawadai wanirejeshe 1.7 M, niliingia refund account zaidi ya miezi 6 lakini kapa hawajahakiki kurudishiwa pesa yangu. Niko tayari wanipe hata milioni moja tu laki 7 niwaachie, niokoe maisha ya mgonjwa wangu. Ushauri wenu tafadhari nifanyeje?
 
Kwanini ukatwe zaidi kwani si kila mwezi unaona deni lako limebaki kiasi gani?
 
Makosa wafanye wao kukata zaidi ya deni mnufaika unalodaiwa halafu ukiwafuata wanakupa statement wenyewe inaonyesha kweli umekatwa zaidi. Badala ya kuhakiki deni lako na kukuandika hundi wanakwambia rudi nyumbani na kajisajiri kwenye mfumo udai kurudishiwa makato yaliyozidi.

Wanakwambia subiri baada ya miezi 3 ndipo watapitia kuhakiki malipo yako. Ukiwapigia kuwakumbushia muda umepita simu anapokea afisa mmoja ana kiswahili cha kule ndege ilikotua majini. Anakushambulia kwa maswali kuwa ulieleweshwa usubiri muda gani, utadhani wewe ndiye mwenye makosa kukatwa zaidi ya deni halisi.

Wakati mwingine japo kuna mambo sikukubaliana na mwendazake inabidi nimkumbuke tu. Hivi mama yetu huwezi kuwaambia watulipe ndani ya siku 3 badala ya miezi 3. Hivi Prof Mkenda na hili nalo ukiwambia watulipe ndani ya siku 3 watakugomea mpaka tena uwashitaki kwa Spika?
Changamoto kweli alafu mtu asipolipa aka diverge aonekane mbaya, Sasa Hela yako lakini unazungushwa na unaweza kuchoka uiache
 
Changamoto kweli alafu mtu asipolipa aka diverge aonekane mbaya, Sasa Hela yako lakini unazungushwa na unaweza kuchoka uiache
Ndiyo lengo lao, au ufe kwani ndugu wa marehemu wanajua hata hata kufuatilia hiyo akaunt ya loan refund. Serikali hii unatamani covid irudi.
 
Mimi tokea niombe Refund, ni mwaka sasa hawahanilipa, ninahisi hawatoi refund
 
Ndiyo lengo lao, au ufe kwani ndugu wa marehemu wanajua hata hata kufuatilia hiyo akaunt ya loan refund. Serikali hii unatamani covid irudi.
Hahaha. Covid irudi? Na mifuta hayo kifuani lazima ishikishwe adabu ivae bandage midomoni
 
Pole sana mkuu, ukiwabana, wanakujibu kua pesa ya serikali inao utaratibu wake wakuitoa. Pole sana.
hata mm nilikatwa kama laki 2 na zaidi lkn mpaka leo sijarudishiwa pamoja na kuzifuata hizo taratibu.sasa ni miaka kama tisa hivi niliamua kuacha tu sababu kwa sasa niko na shughuri zangu nimeona nitapoteza muda bure.
 
Hivi Mhe. Kigwangala si yumo humu akambane yule Prof. Mkenda na HESLB anaowalalamika kwa Bunge badala ya kuwapiga chini. Au hata CAG basi akague pesa hizi
 
Back
Top Bottom