Bodi ya mikopo imepeleka Tsh bilioni 122.8 vyuoni

Bodi ya mikopo imepeleka Tsh bilioni 122.8 vyuoni

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema imeshapeleka Tsh Billioni 122.8 katika vyuo na taasisi za elimu 81 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi.

Imesema wanafunzi wanaostahili kupata mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 ni 132,119, fedha wanazopewa ni kwa ajili ya malazi, posho na ada na kufafanua kuwa fedha za malazi na posho ni za siku 60 kuanzia Juni Mosi hadi Julai 30, 2020.

Hatua hiyo imekuja baada ya Rais John Pombe Magufuli alitangaza kufungua vyuo kuanzia Juni 1 na aliwapa siku tisa za kujiandaa ili kusiwe na changamoto kwa wanafunzi na vyuo wakisharudi shuleni.

Rais ameruhusu wanafunzi wa vyuo na wanafunzi wa kidato cha sita kuendelea na masomo akisema kuwa ni watu wazima ambao wanaweza kujichunga dhidi ya #CoronaVirus.
 
Safi sana, Rais Magufuli anawamwagia vijana mapesa
 
Kwahiyo ile ‘quarter’ ya March - June inafunikwa.?

Hii dhulma haikubaliki.
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.
Daah kwahiyo tufanyeje hapo mkuu vipi tufute mikopo ya Elimu ya juu au sio?!
 
Kuwa na vyuo vikuu vingi katika nchi ni kuongeza idadi ya masikini nchini,Hawa wakimaliza wanarudi kuwa mizigo ya familia zao kwanza hawana skills za kujiajiri zaidi kutegemea kuajiriwa.
Tuanzishe vyuo vya maendeleo kila kata vijana wakopeshwe ujuzi Kisha waingie mtaani wachochee uzalishaji.
Mfano pesa iliyotumika kununua ndege ingetumika kujenga vyuo kila kata , ikatumika kuendeleza kilimo tungetatua tatizo la ajira.Sema tu vipaumbele vya watawala huwa si vipaumbele vya wananchi.
Tunakosa mipango sahihi tunashindwa endelea tunaishia kuwalaumu wazungu Hali tuna kila kitu, isipokuwa sera tu na utekelezaji ndo tatizo
 
Daah kwahiyo tufanyeje hapo mkuu vipi tufute mikopo ya Elimu ya juu au sio?!
Tujenge vyuo vingi vya maendeleo mfano wa veta yaani mtu akimaliza la saba,sekondari akajifunze ujuzi,Kama ilivokuwa mfumo wa elimu wa kikoloni wa vitendo ulikuwa mzuri Sana uliwaandaa watu kufanya kazi tuliuharibu sababu tulipomchukia mkoloni tulimchukia na mazuri yake pia.Elimu ya chuo kikuu iwepo kwa anaetaka lkn sio lzm wote waendee chuo kikuu wakafundishwe uoga wa maisha.Je unajua informal sekta wanaingiza pesa nyingi Sana kuliko sekta rasmi za ajira ambazo wengi ili utoke ni lzm upate mwanya wa kuiba.
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.
mbona vihela vidogo ivo vimekuuma mkuu
 
mbona vihela vidogo ivo vimekuuma mkuu
Ishu sio kuuma ishu ni tuangalie tija ya hio mikopo.Kumbuka hizo pesa hazirudi Hadi waingie sekta rasmi ambazo unaweza kaa hata miaka 10 ndo upate napo sio garantii.Tusisome Kama fasheni then tunakuja kuwa mizigo kwa taifa
 
Ishu sio kuuma ishu ni tuangalie tija ya hio mikopo.Kumbuka hizo pesa hazirudi Hadi waingie sekta rasmi ambazo unaweza kaa hata miaka 10 ndo upate napo sio garantii.Tusisome Kama fasheni then tunakuja kuwa mizigo kwa taifa
kwa gharama ya vyuo watu wasinge soma mkuu kumbuka iloo hata hao unasema wamedhagaa mitaani wasinge kuwepo na n watoto wa masikin tu. wenye pesa mtoto anafanya field kwanye kampuni ya babayakee
 
Kuwa na vyuo vikuu vingi katika nchi ni kuongeza idadi ya masikini nchini,Hawa wakimaliza wanarudi kuwa mizigo ya familia zao kwanza hawana skills za kujiajiri zaidi kutegemea kuajiriwa.
Tuanzishe vyuo vya maendeleo kila kata vijana wakopeshwe ujuzi Kisha waingie mtaani wachochee uzalishaji.
Mfano pesa iliyotumika kununua ndege ingetumika kujenga vyuo kila kata , ikatumika kuendeleza kilimo tungetatua tatizo la ajira.Sema tu vipaumbele vya watawala huwa si vipaumbele vya wananchi.
Tunakosa mipango sahihi tunashindwa endelea tunaishia kuwalaumu wazungu Hali tuna kila kitu, isipokuwa sera tu na utekelezaji ndo tatizo
Wazo la aliyefeli
 
kwa gharama ya vyuo watu wasinge soma mkuu kumbuka iloo hata hao unasema wamedhagaa mitaani wasinge kuwepo na n watoto wa masikin tu. wenye pesa mtoto anafanya field kwanye kampuni ya babayakee
Kusoma sio tatizo,tatizo ni matokeo baada ya kusoma.
Kumbuka mifumo yetu ya elimu uwaandaa watu kuajiriwa.
Labda tu Kama tungechochea ukuaji wa ajira hapo sawa.
Ajira ziko zile zile tena zikizidi pungua Hilo kundi utalipeleka wapi.
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.

Dokta unamaanisha nini.?

Kama ni daktari MD ni vema ujue kuwa wanapata GRANT sio LOAN, jiridhishe na hilo sio unashikwa maskio na madaktari uchwara... hoja yako ina msingi kasoro mfano uliotumia.
 
Dokta unamaanisha nini.?

Kama ni daktari MD ni vema ujue kuwa wanapata GRANT sio LOAN, jiridhishe na hilo sio unashikwa maskio na madaktari uchwara... hoja yako ina msingi kasoro mfano uliotumia.
Hata sio dokta vipi professional zingine si the same wanarudi kumaliza soli za viatu.
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.
Mwananchi ndo mnufaika wa kodi

Ndomaana primary na secondary school hawalipi ada. Ifike mahali tujue tunasoma kuongeza maarifa Pasi na kutegemea kuajiriwa
 
Then wanamaliza vyuo wanarudi mtaani kuendesha bodaboda,Kodi zetu ndo zimepotea hivo.
Case study pana wanandoa wote wamesoma kwa mkopo mmoja dokta, mwingine Mwalimu.
Mume kawa dereva taxi mke kafunguliwa saloon wameona mda unaenda ajira rasmi hakuna,means taaluma zao si tija kwao wameingia taaluma zingine ili maisha yasonge.Hapa pana zaidi ya milioni 20 Kodi yetu imepotea.
Hivi mfano hio pesa unaweza ukawalipia vijana si chini ya 100 wakapata elimu ya ufundi wakajiajiri tungesaidia Vijana wengi kuweza kupata taaluma kuliko kuwekeza kwa watu 2 ambao awazitumii.

Mkuu, inaelekea kuna hoja unataka kutoa lakini sauti yako ni ya chini mno - hatukusikii. Unataka kusema elimu ya chuo kikuu sio muhimu? Au unasema mikopo kwa ajili ya elimu ya chuo kikuu isitolewe kila mtu ajijue mwenyewe? Au umeandika tu?
 
Mnavyojipamba utadhani izo pesa mmewapa bure wakati ni mkopo wa riba tena kubwa tu.
 
Back
Top Bottom