Shigganza
Senior Member
- May 24, 2018
- 160
- 412
Bodi ya utalii Tanzania(TBT) kwa kushirikiana kushirikiana na taasisi ya Magnet Youth Sports Organization inatarajia kumleta mshambuliaji wa kimataifa wa Denmark mwenye asili ya Tanzania ambaye hivi sasa anayechezea klabu ya RB Leipzig inayoshiriki ligi kuu ya ujerumani ' Bundesliga' YUSSUF POULSEN kwa ajili ya kuzuru Nchini kwa shughuli za kitalii.
Ujio wa POULSEN unafuatia ziara ya kitalii ya makocha Andreas Pach na Martin Hammel wa ujerumani ya kupanda mlima Kilimanjaro Februari 15 hadi 19 mwaka huu na vivutio vingine lengo likiwa ni kutangaza utalii.
Ziara ya POULSEN Nchini Tanzania inatarajiwa kuitangaza zaidi Tanzaniakatika suala la utalii, ikizingatiwa mwanasoka huyo anacheza katika ligi ya Ujerumani ambayo ni miongoni mwa ligi kuu bora kabisa Duniani yenye mashabiki lukuki kutoka kila pande ya Dunia. Aidha ujio wa mwanandiga huyo unafungua ukurasa mpya kwa wanasoka wengine kutoka ligi ya ujerumani kuja Nchini kwa shughuli za kitalii.
Bila kumung'unya maneno Serikali ya awamu ya tano iko serious na imejizatiti kuhakikisha sekta ya utalii inaliingizia taifa fedha nyingi za kigeni.
Ujio wa POULSEN unafuatia ziara ya kitalii ya makocha Andreas Pach na Martin Hammel wa ujerumani ya kupanda mlima Kilimanjaro Februari 15 hadi 19 mwaka huu na vivutio vingine lengo likiwa ni kutangaza utalii.
Ziara ya POULSEN Nchini Tanzania inatarajiwa kuitangaza zaidi Tanzaniakatika suala la utalii, ikizingatiwa mwanasoka huyo anacheza katika ligi ya Ujerumani ambayo ni miongoni mwa ligi kuu bora kabisa Duniani yenye mashabiki lukuki kutoka kila pande ya Dunia. Aidha ujio wa mwanandiga huyo unafungua ukurasa mpya kwa wanasoka wengine kutoka ligi ya ujerumani kuja Nchini kwa shughuli za kitalii.
Bila kumung'unya maneno Serikali ya awamu ya tano iko serious na imejizatiti kuhakikisha sekta ya utalii inaliingizia taifa fedha nyingi za kigeni.