DOKEZO Bonde la Mto Msimbazi - Dar limeanza kuwa dampo, siyo jambo zuri kwa Afya ya Wakazi wa Vingunguti

DOKEZO Bonde la Mto Msimbazi - Dar limeanza kuwa dampo, siyo jambo zuri kwa Afya ya Wakazi wa Vingunguti

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katika pitapita za kila siku mtaani, hivi karibuni nilikatiza maeneo ya Vingunguti pembezoni mwa Bonde la Mto Msimbazi na kukutana na hali ya hatari kwa afya. Kiukweli mambo si shwari katika eneo hili, hasa usalama wa afya kwa wakazi waliozunguka eneo hilo.
IMG_1118.jpeg

Kingo za mto huo zimegeuka kuwa dampo la taka za kila aina ambazo zinatoa harufu kali. Watu wanaingia katika taka hizo kutafuta vitu mbalimbali kwa lengo la kuuza ili kutumia tena, jambo linalozua maswali kuhusu athari zake kiafya.

IMG_1139.jpeg

Baada ya kusogea mbele zaidi, nilishuhudia kundi la watoto wadogo wakiendelea na michezo kwenye taka bila kujua hatari za kiafya zilizopo. Hali hii ni ya kusikitisha, hasa ukizingatia kuwa mazingira wanayochezea yanawafanya kuwa hatarini kwa magonjwa.

IMG_1140.jpeg

IMG_1127.jpeg

Hatari hii inaweza kubwa ikitokea magonjwa ya mripuko ukizingatia, Nje kidogo kuna lango kuu la kuingilia ndani ya machinjio ya Vingunguti, unapishana na watu wengi wa kila rika, wakijipatia mahitaji yao ya kitoweo.

IMG_1113.jpeg

Jitihada za haraka zinahitajika kuboresha mazingira kwa ustawi wa wakazi, hasa watoto, na ni muhimu kwa serikali na wadau kushirikiana kulinda afya za wakazi wa Vingunguti na maeneo ya jirani.


 
Back
Top Bottom