Bongo Fleva ya zamani tulikuwa tunapewa story.. siku hizi tunapewa nini?

Nimeajiiwa kwenye ajira niliojiajiri,
Nasiwa utendaji wangu kazi ni mzuri,
Navumilia Wenda ntapata kivuli,
Ntapata kivuli inshakata miaka miwili,
Ndimu na ugali maisha makali elimu iko mbali,
Lile jasho la halali mpaka kabali,boss katili,
Naghairi,mnameza mate ya akili,
Mbona sina kiburi nina lumba na jua Kali,
Asubuhi alasiri na adhuhuri,
Mwendo wa kuunga kandambili,ndio yangu staili,
Jero nauli baki mia mbili,kazi na ugali,
Si ubahili Mama sina pesa kweli,
Mara dalali Mara tapeli sina habari,
MIE SINA ZALI,SISAKI MALI NASAKA UGALI,

ukiaangaliaaaa inaumaaaa ooohhh
Ukifikiriaa inachomaaa eeehh
Inaumaaaa ...inachomaaa

#20%
 
Tumevuka mabonde na milima/
Vikwazo vingi tulisimama wima/
Walishazusha vingi vioja/
Asali wangu wa moyo tupo pamoja/
Penzi letu likumbwa na vikwazo sana/
Sisi tulivumilia hatuachana/
Walikuambia kila siku nabadilisha wasichana/
Uliwapuuza hukujari yao dhana/
Hao wazushi hao
Hao wazushi hao
(Asali wa moyo part 2 )

Kahena Haruna aka inspekta haroun aka babu katika ubora wake.

Sina muda wa kukariri bongo flavor za sasa ni headache tu....
Come on
Afande selle
Jaymo
Imamu abbas
Nature
Dojo na domo kaya
Solo Thang Mteule
Wagosi
Squeezer
University corner
Waswahili wazee wa pengo
Sister p
Kali popote kali p
Zay b
Gk
Luteni karama
Daz nundaz
Mchizi mox
Jafarai
O ten
Hardmad Kidume Mkushi
Mpo wengi sitaki kuamini tatizo ni airtime mlitamba kipindi redio na tv zipo chache sana hata mitandao ya kijamii haikuepo..
Mungu awatie nguvu
 
Hahaa we jamaa umenikumbusha mbali. yule msanii kichaa sana. Nimejikuta namkumbuka na msanii mmoja anaitwa Pig Black alikuwa na ngoma moja hatari sana.
 
Elimu mitaani dot com mnaionaje? D KNOB
Safi sana!!!

"Wenzio waniogopa ka'Ukimwi"
D Knob!!!
Wakati mwingine unaweza kujisemea moyoni kwamba nyakati hizi hatuna wasanii.
 
Wimbo wa "Huna Jipya" niliupenda, hakika yupo vyema P the MC.
Ktk album hiyo hiyo kuna track moja story moja imeanzia posta mpaka bom bronx. Nayo noma. "Kweli siku hazifanani, miti itateleza tu siku hakifa nyani"
 
"Kuanzia Leo Mimi sio Polisi tena"

Kali -P.
Aiseeee burudani ilikuwa ya kutosha.!
 
Kwenye makundi ambayo niliwahi kuyakubali ni hawa solid ground family.
Kuna ile mechi Kali timu ya kifo na timu ya uhai.
 
Watu wenywe skuhiz,wanashindia
Chips yai plus kushera
Vipodoz na dada zao unafkir

Story watapata wap
[emoji23] [emoji23] [emoji23] si humo humo kwa dada zao.like

KIJUSO.[emoji125]
 
Chemsha bongo- Prof Jizoo
Niko mikononi mwa Polisi- Mr II
Mambo ya pwani-Solo Thang
Nakuhitaji
 
Siku hizi ukitaka Story Telling Rap msikilize Songa....kwa miaka ya karibuni jamaa Amekuja kushika nafasi ya wakongwe kwenye hili.

-Usiku
-Beki tatu
-Beef
-Ninapotoka
-Ndege
-Sorry
-Kikosi cha mizinga.

Sikiliza hizi at least utapata utamu ule wa enzi zile....Kwangu jamaa ni Best Story Teller Rapper kwa kizazi chase.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…