Bongo land

Okol36

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2015
Posts
1,544
Reaction score
738
Hii ndio Bongo

Ilikuwa Ijumaa mida ya saa 10 jioni, mzee mmoja aliingia na kibinti kizuri kwenye yard ya magari mapya. MZEE: Chagua gari unalotaka mpenzi....kabinti akazunguka yard yote mwisho akachagua Verrosa metallic . BINTI: Mi naitaka hii MZEE: Hakuna tatizo kabisaaa, mtoto mzuri kama wewe lazima upate gari uloichagua mwenyewe. Mzee akatoa kitabu cha cheki na kuandika palepale na kumpa mwenye yard MUUZAJI: Sasa Mzee kwa kuwa umetoa cheki, gari utakuja chukua Jumatatu tukishahakikisha kuwa Account yako ina pesa benki. Naomba namba yako ya simu Mzee MZEE: Hakuna tatizo (akampa namba). Haya twende zetu sweetie Jumatatu tunakuja wote kuchukua gari lako... Siku ya Jumatatu mwenye yard kampigia simu Mzee. MUUZAJI: We Mzee kavu sana, akaunti yako haina hata senti tano. MZEE: Hilo nilijua, lakini wiki endi yangu ilikuwa tamu sana.
 
Asante mjomba hiyo ndio dawa ya vidafa vinavyopenda vinavyoonekana kwa nje ila ukweli wa mambo anaujua muhusika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…