Bongo movie na BOT kunani.... ??

Bongo movie na BOT kunani.... ??

Moyibi

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2012
Posts
1,054
Reaction score
701
Nimebahatika kucheki movie kibao Sana za kibongo... Kwanini katika movie zenu lazma kuwe na haka ka scene ka kuonesha B.O.T ... Why always B.O.T na movie zenu haziwezi kukamilika bila kuonesha hilo jengo la B.OT !???

Kama kuna umuhimu au ulazima bhasi muoneshe hata mount Kilimanjaro.... Ziwa Victoria..... Nawasilisha hoja !!
1470330423156.jpg

1470330439743.jpg
 
BoT ni sehemu ya Skyline ya Dar es Salaam Mjini Kati na imekuwa utambulisho kwa muda mrefu.
Kwa kuwa Movie imetengezwa mji huo ni vema kuanza na sini ambayo itamfahamisha mtazamaji kwamba hapa ni Jiji la Makamba, kuna kukosekana kwa ubunifu, si kwenye kesi ya skyline, Bali Bongo Movie nzima.
Tuvumiliane tu, au kama unaweza uwe mwanaharakati wa filamu upiganie mabadiliko. Otherwise haya ni malalamiko ambayo hayatabadili tasnia wala uchumi wake zaidi ya kuonesha walimwengu vyenye tunajichukia.
 
Mdada anatoka sebuleni huyo hatua 1 .2 .3.4....... hadi anafungua geti gari inaingia pole pole inapaki dereva anashuka hao wanatembea hadi sebuleni hao wanawesha tv. (hiyo scene hapo wanaitumia dakika 30 - 35 )
 
Mdada anatoka sebuleni huyo hatua 1 .2 .3.4....... hadi anafungua geti gari inaingia pole pole inapaki dereva anashuka hao wanatembea hadi sebuleni hao wanawesha tv. (hiyo scene hapo wanaitumia dakika 30 - 35 )
Sasa si ili itoke pati one na two?
 
Sasa kila ukiwahoji wamesoma wapi kazi hiyo mtu anakwambia ni kipaji tu sasa kipaji bila msasa inakuwaje? Au ndo ile the sharp spear needs no Polish?
 
Ndo maana hata movie zao zinachuja sana maana hawana ubunifu wowote. Watazamani wamekuwa watoto na mahouse girl.
 
af kweli kwanini wasionyeshe jengo lolote la mkoani wanaonesha la dar (B.O.T? af kuna muvi moja ya mwanza wameonesha jengo la dar(B.O.T) akati scene iko mwanza
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Kuiga kubaya.
 
Back
Top Bottom