Uta Uta
JF-Expert Member
- Feb 2, 2016
- 3,740
- 8,751
Habari wanajamvi?
Leo katika kuperuzi peruzi u-tube nikakutana na interview moja aliyofanyiwa msanii, muongozaji na muandaaji nguri wa kimataifa wa filamu za action Aston Barnabas aka Vanbrado aka Van Damme. Katika interview hiyo alikuwa anaelezea juu ya uandandaaji na bifu la msanii mwenzake aitwaye Neylish, kilichonishtua ni kwamba walikubaliana waandae movies kwa gharama ya Tsh 2,500,000.00/= yaani Tshs millioni mbili na laki tano na senti sifuri tu. Sasa mi nikashangaa sana na kuhisi hawa wasanii wametuchoka sisi watanzania na hawako serious kabisa. Milioni mbili unatengeneza filamu kabisa ambayo unategemea kuja kuliteka soko la filamu Tanzania, kwa kiasi hicho utafanya nini hasa cha kuwavutia watanzania wa rika tofauti, uelewa tofauti na kushindana na filamu kutoka nchi nyingine? pia hizo filamu zenu mna malengo ziangaliwe tu kwa mtogore, Nzasa, Kibudi, Kwakopa na Kwamfuga mbwa pekee si nje ya nchi?
Pili hiyo kazi ya u director, u producer mnaipata kwa vigezo gani? maana mtu anatoka na filamu moja leo kesho unasikia keshakuwa director, producer, location manager, costumes (sijui ndio kitu gani), nk.
La mwisho ambalo linakela zaidi unakuta wewe director mke wako au mchepuko wako co-director, mwanao location meneger, mdogo wako mpambaji, wifi yako sijui anafanya nini, sasa hao wote wanakuwa na utaalam wa hayo mambo au ndio ili mradi si wabongo hatujui viwango. Ushauri wa bure kama mna milioni mbili mbili basi kusanyikeni hata watu hamsini mpate milioni 100 ili muandae filamu zinazoeleweka na kumvutia kila mmoja.
Kwa uhondo zaidi sikiliza interview wewe mwenyewe hii hapa chini;
Leo katika kuperuzi peruzi u-tube nikakutana na interview moja aliyofanyiwa msanii, muongozaji na muandaaji nguri wa kimataifa wa filamu za action Aston Barnabas aka Vanbrado aka Van Damme. Katika interview hiyo alikuwa anaelezea juu ya uandandaaji na bifu la msanii mwenzake aitwaye Neylish, kilichonishtua ni kwamba walikubaliana waandae movies kwa gharama ya Tsh 2,500,000.00/= yaani Tshs millioni mbili na laki tano na senti sifuri tu. Sasa mi nikashangaa sana na kuhisi hawa wasanii wametuchoka sisi watanzania na hawako serious kabisa. Milioni mbili unatengeneza filamu kabisa ambayo unategemea kuja kuliteka soko la filamu Tanzania, kwa kiasi hicho utafanya nini hasa cha kuwavutia watanzania wa rika tofauti, uelewa tofauti na kushindana na filamu kutoka nchi nyingine? pia hizo filamu zenu mna malengo ziangaliwe tu kwa mtogore, Nzasa, Kibudi, Kwakopa na Kwamfuga mbwa pekee si nje ya nchi?
Pili hiyo kazi ya u director, u producer mnaipata kwa vigezo gani? maana mtu anatoka na filamu moja leo kesho unasikia keshakuwa director, producer, location manager, costumes (sijui ndio kitu gani), nk.
La mwisho ambalo linakela zaidi unakuta wewe director mke wako au mchepuko wako co-director, mwanao location meneger, mdogo wako mpambaji, wifi yako sijui anafanya nini, sasa hao wote wanakuwa na utaalam wa hayo mambo au ndio ili mradi si wabongo hatujui viwango. Ushauri wa bure kama mna milioni mbili mbili basi kusanyikeni hata watu hamsini mpate milioni 100 ili muandae filamu zinazoeleweka na kumvutia kila mmoja.
Kwa uhondo zaidi sikiliza interview wewe mwenyewe hii hapa chini;