Huyu Wema mie ananishangaza sehemu moja tu!! Kwenye movie na interview zake, ni full viingereza, utafikiri kakulia kwenye English speaking country na tangu aje Bongo hana hata mwaka!! Nikaja kukoma siku ametembelewa na akina Bibi Bomba; duh....hata mbele ya akina Bibi Bomba, vi-english kwa kwenda mbele!! Ana sahau kabisa kwamba hao wanaofahamu Viingrereza wenyewe wala hawana time na movie za Kibongo....huku ni kutowatendea haki wafuasi wakuu wa movie, dada zetu wa kazi za ndani na watu wa kawaida huku Uswahilini.