Ni ajabu na kweli baada ya yote yaliyotokea Moshi mwezi uliopita Mwamposa atunukiwa udaktari wa heshima. Mshana Jr alitabiri kupanda cheo kwa Mwamposa na sasa yamekuwa kweli. Watu wanapaswa kufunguka macho kuhusiana na yanayoendelea ulimwenguni tena siku hizi yapo wazi kabisa. Kuweni waangalifu sana watu wa Mungu!
Tukio la Mwamposa Moshi lingempata mtu wa upande wa pili tungepigiwa kelele hadi masikio yakaziba wasemaji wangekuwa kama wote. Leo msiba umebaki kwa ndugu
.
Mkuu wa Mitume na Manabii , wa kanisa la Raise and Shine, Dkt Bonifance Mwamposa, (Buldoza) siku ya leo ametunukiwa shahada ya Uzamili ya heshima na Chuo cha Lead impact University kilichopo Colorada nchini Marekani.
Tukio hilo la kuwatunukiwa vyeti hivyo limefanyika mapema leo katika ukumbi wa KARIMJEE jijini Dar Es Salaam, Mgeni rasmi akiwa ni mmiliki wa Chuo hicho ambacho masomo yake hutolewa Online ila makao makuu yakiwa Marekani Dkt. Cletus Bassey ambaye ni mzaliwa wa Nigeria ila makazi yake yakiwa Marekani.
Akizungumza baada ya kutunukiwa Udocta huo, Mwamposa alisema kuwa unapofanya kazi unaweza usijuwe umegusa jamii kwa kiwango gani, lakini wapo watakaojuwa na kuona hayo unayoyafanya.
Baada ya kuuliza kuhusu tukio lililotokea mkoani Kilimanjaro kwamba anaongeleaje alichosema ni kwamba Changamoto zipo katika kila kitu ila watu wanatakiwa kujua kwamba Aliye juu ndiye anayeweza kumnyanyua aliye chini ila aliye chini hawezi kumnyanyua aliyoko juu
Tukio la Mwamposa Moshi lingempata mtu wa upande wa pili tungepigiwa kelele hadi masikio yakaziba wasemaji wangekuwa kama wote. Leo msiba umebaki kwa ndugu
.
Mmeshaambiwa mkuu wa Chuo ni mzaliwa wa Nigeria.
Mimi nilimwambia mdogo wangu kuwa aliyemtuma kutoa kafara ndiye atakayemtetea mbele ya vyombo vya Dola na Mahakama.