Boss kukufokea

Kukaaa kimya ilikua na faida zaidi kuliko kuripoti! Na kilichomfanya apate hasira sio kosa lililofanyika ila kwann mm sikuliripoti
 
Umenikumbusha kuna boss alinitesa sana kila akikuta nahudumia demu mzuri lazima anigombeze bila sababu ilimradi demu aone yeye ndo tajiri

Siku moja nilikasirika sana nilisimama kwa hasira bila kusema neno nikawa namsogelea akawa anarudi nyuma kwa uoga nikajua kumbe ni pimbi tu nikaachana nae ila hakurudia tena
 
Wivu lazima.

Labda alikuwa anakupenda anataka ukambandue jicho.
 
Kukaaa kimya ilikua na faida zaidi kuliko kuripoti! Na kilichomfanya apate hasira sio kosa lililofanyika ila kwann mm sikuliripoti
pole sana aise maana Maboss wengi huwa na tabia ya kupandikizia au kutengeneza spies 9tabia ya kuchongeana) miongoni mwa wafanyakazi,inawezekana naye alikuwa na lengo hilo hilo hivyo lazima afoke
 
Kama na yeye ameajiriwa basi huyo sio bosi bali ni kibarua mwenzako; nawe umfokee tu; ila kama ni kampuni yake na amekuajiri, kuwa mpole kwa sababu ndio anayekuweka mjini.
Aise labda kama siyo Supervisor wake au mtu ambaye amemzidi cheo,maana unaweza jikuta kibarua kimeota nyashi kwa utovu wa nidhamu tu,ambapo ungeweza kukausha tu na usipungukiwe chochote kwa wakati huo,Muda mwingine ukimya ni bora kuliko maneno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…