A
Anonymous
Guest
Nakumbuka hivi karibuni Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilitangaza kufungia jumla ya Application 69 zilizokuwa zinatoa mikopo kidijitali bila leseni.
Hatua hii ilikuwa ni muhimu katika kudhibiti sekta hiyo na kulinda haki za watumiaji.
Hata hivyo, licha ya kuwepo kwa sheria na hatua za kufungia baadhi ya apps, bado kuna changamoto, kwani app ya mikopo, ya Credit Lab (Dragon Loan), bado wanaendelea kukiuka sheria kwa kutuma SMS za udhalilishaji kwa wateja wao na mpaka kwa ndugu wa wateja.
Hali hii haivunji tu haki za faragha za wateja, bali pia inaleta fedheha na mateso ya kisaikolojia kwa wahusika.
Ni wazi kuwa ukiukaji huu wa sheria unaashiria dharau kwa mamlaka na sheria zilizopo, jambo ambalo linapaswa kukemewa kwa nguvu zote.
Hatua hii ilikuwa ni muhimu katika kudhibiti sekta hiyo na kulinda haki za watumiaji.
Hata hivyo, licha ya kuwepo kwa sheria na hatua za kufungia baadhi ya apps, bado kuna changamoto, kwani app ya mikopo, ya Credit Lab (Dragon Loan), bado wanaendelea kukiuka sheria kwa kutuma SMS za udhalilishaji kwa wateja wao na mpaka kwa ndugu wa wateja.
Hali hii haivunji tu haki za faragha za wateja, bali pia inaleta fedheha na mateso ya kisaikolojia kwa wahusika.
Ni wazi kuwa ukiukaji huu wa sheria unaashiria dharau kwa mamlaka na sheria zilizopo, jambo ambalo linapaswa kukemewa kwa nguvu zote.