BOXING: Dillian Whyte apigwa KO ya mwaka na Povetkin

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,857
Reaction score
15,866
Kwa wale wapenzi wa masumbwi usiku wa leo kulikuwa na pambano kubwa kati ya haya majina mawili makubwa kwenye uzito wa juu duniani 'Heavyweight'; Dillian Whyte ambaye ni muingereza na Allexander Povetkin ambaye ni mrusi.

Pambano hilo lililomalizika Round ya 5, Dillian Whyte alionekana akidominate mchezo kwa round 4 huku akimdondosha Povetkin mara 2 japo haikutosha kumaliza mchezo, mwanzoni mwa Round ya 5 Povetkin alionesha uveteran wake kwa kumsurprise Whyte kwa uppercut nzito ambapo Whyte alidondoka na mchezo ukaishia hapo.

Dillian Whyte ambaye alikuwa WBC Interim champion pambano hili limemfanya apoteze mandatory status ambayo ingemfanya apigane na mshindi wa pambano lijalo la Deontay Wilder dhidi ya Tyson Fury

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…