Brazil walazimika kutumia mashine maalum za kupumulia baada ya kubanwa na Bolivia

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253

Jana michuano ya kufudhu kwa faiinali za kombe la dunia zitakazopigwa nchini Urusi ziliendelea, katika bara la America Kusini michezo mbali mbali ilipigwa lakini vinara wa bara hilo Brazil walikutwa na makubwa baada ya mechi yao.

Brazil waliokuwa wakicheza dhidi ya Bolivia walitoka suluhu ya bila kufungana lakini hiyo haikuwa habari kubwa kama habari ya wachezaji wa Brazil kutumia mask za Oxygen ili kuweza kupumua.

Uwanja wa Estadio Hernando upo 4000m kutoka usawa wa bahari hali inayoifanya eneo hili kuwa na kiwango cha juu sana cha joto tofauti na mji mkuu wa Brazil wa Rio Di Jeneiro.

Dani Alves, Neymar, Gabriel Jesus na Paulinho ni moja kati ya nyota ambao walipata wakati mgumu kupumua na kuonekana wakiwa wamevaa mask hizo ili kuwasaidia kupata hewa.

Mchezaji ghali duniani Neymar Dos Santos ameitaja hali ya hewa ya Bolivia kama hali mbaya sana kuwahi kucheza soka siku za karibuni na kusema hawakufurahia kabisa mazingira ya mchezo huo.

Hali hii imekuja siku moja baada ya mchezaji wa Ecuador Antonio Valencia kuonya kwamba kati ya vitu vinaifanya michuano ya bara hilo kuwa migumu ni kutokana na hali tofauti ya hewa ambayo inaweza kusumbua wachezaji.

Lakini pamoja na hali hiyo mbaya lakini haikuwazuia Brazil kupata alama moja iliyofanya kufikisha idadi ya michezo 11 bila kupoteza huku ikiwa timu pekee kushiriki fainali zote za kombe la dunia tangu mwaka 1930.

shaffih Dauda
 
Bolivia sio sehemu salama pakuchezea soka aisee hata Messi huwa anatapika huko.
 
Ila Bolivia wajanja kinoma wanatumiaga uwanja wa nyumban kuzipiga timu
 
hahahahhahaha bolivia wahuni hao, walichagua uwanja utakao wapa mateso hao mabishoo.

bolivia wameleta uhuni wa wauza madawa ya kulevya hahaaha
 
Tatizo sio joto ni air pressure ndogo kitu kinachofanya mwili wako kupata shida kupokea Oxygen.
 
Kuwa juu sana kunakuwa na baridi na si joto. Pia pressure ya hewa inakuwa ndogo hivyo hewa inashindwa kuingia vizuri hasa kwa wale waliozoea mazingira ya uwanda wa chini. Inaweza wakuta wachezaji wa dar wakienda sehemu kama Njombe.
 
Hahaha,Bolivia ni hatari kina Messi huwa wanakula kipigo na kutapika juu,Brazil kajitahid sana kutoa hiyo droo.Ile hali wanaiweza wenyewe wa Bolivia..Air pressure ni ndogo kule juu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…