Brazil waliokuwa wakicheza dhidi ya Bolivia walitoka suluhu ya bila kufungana lakini hiyo haikuwa habari kubwa kama habari ya wachezaji wa Brazil kutumia mask za Oxygen ili kuweza kupumua.
Uwanja wa Estadio Hernando upo 4000m kutoka usawa wa bahari hali inayoifanya eneo hili kuwa na kiwango cha juu sana cha joto tofauti na mji mkuu wa Brazil wa Rio Di Jeneiro.
Dani Alves, Neymar, Gabriel Jesus na Paulinho ni moja kati ya nyota ambao walipata wakati mgumu kupumua na kuonekana wakiwa wamevaa mask hizo ili kuwasaidia kupata hewa.
Mchezaji ghali duniani Neymar Dos Santos ameitaja hali ya hewa ya Bolivia kama hali mbaya sana kuwahi kucheza soka siku za karibuni na kusema hawakufurahia kabisa mazingira ya mchezo huo.
Hali hii imekuja siku moja baada ya mchezaji wa Ecuador Antonio Valencia kuonya kwamba kati ya vitu vinaifanya michuano ya bara hilo kuwa migumu ni kutokana na hali tofauti ya hewa ambayo inaweza kusumbua wachezaji.
Lakini pamoja na hali hiyo mbaya lakini haikuwazuia Brazil kupata alama moja iliyofanya kufikisha idadi ya michezo 11 bila kupoteza huku ikiwa timu pekee kushiriki fainali zote za kombe la dunia tangu mwaka 1930.
shaffih Dauda