BRICS ni OPEC mpya?

BRICS ni OPEC mpya?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Kwanza ninaona ni jambo zuri kwa hegomony ya USA kwenye uchumi wa dunia kuwa challenged. Kama ambavyo dola ya Marekani ilivyoiangusha paundi ya Uingereza kama sarafu ya dunia, ndivyo inapaswa nayo kuanguka. Lakini safari hii itapendeza kupata mchanganyiko wa sarafu zenye nguvu. Matumizi ya dola kama sarafu ya dunia umekuwa wizi wa mchana kweupe uliofanyika kwa miaka mingi sana.

Sasa basi, dola hiyo kama sarafu ya dunia nguvu yake kubwa inatokana na kutumika kwenye biashara ya mafuta. Biashara kubwa kuliko zote duniani. Na nchi zinazoipinga US na ubabe wa dola ni wazalishaji wakubwa wa mafuta duniani. Katika nchi zinazoongoza kuzalisha mafuta duniani, Tano zimo ndani ya BRICS. Baada ya kuingia kwa UAE, IRAN na Saudi Arabia.

Duniani wazalishaji wakubwa kumi wa mafuta ni USA, Saudi Arabia, Russia, Canada, China, Iran, Iraq, UAE, Kuwait na Brazil. Hapo utaona nchi tano zipo tayari ndani ya BRICS. Je BRICS ni kama OPEC(umoja wa nchi zinazozalisha mafuta) mpya? Kwa kuwa na wazalishaji wakubwa wa mafuta, tunaweza kusema BRICS imeishika Marekani penyewe?
 
Paundi ya Uingereza haijawahi kuwa sarafu ya dunia.
 
Kwa nini OPEC imeshindwa kuishika Marekani penyewe??
 
Paundi ya Uingereza haijawahi kuwa sarafu ya dunia.
Siyo kwa level za dolar ila ilikuwa ndiyo yenye kupendelewa zaidi kama reserve currency. Kumbuka dola ya Uingereza ilitawala asilimia kubwa ya watu duniani.
 
Kwa nini OPEC imeshindwa kuishikMarekani penyewe??
OPEC haikuwa na lengo la kuondokana na ubabe wa dola. Lengo lake hasa lilikuwa kupata bei nzuri ya bidhaa yao. Lakini wote ni kama "vikundi vya wazalishaji wakubwa wa mafuta."
 
Siyo kwa level za dolar ila ilikuwa ndiyo yenye kupendelewa zaidi kama reserve currency. Kumbuka dola ya Uingereza ilitawala asilimia kubwa ya watu duniani.
Wakati wa utawala wa ukoloni wa Uingereza huko India walikuwa wanatumia Rupee, hapa Africa Mashariki tulikuwa tunatumia shillingi.
 
Wakati wa utawala wa ukoloni wa Uingereza huko India walikuwa wanatumia Rupee, hapa Africa Mashariki tulikuwa tunatumia shillingi.
Hata leo tunatumia Tsh na India Rupee. Lakini tukitaka kufanya biashara kati ya India na Tz. Au sisi na US lazima tutumie dola. Ndivyo ilivyokuwa. Ukitaka kufanya biashara kati ya India na Tz au India na UK, Sterling ilitumika
 
Back
Top Bottom