VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Nazungumza nawe Brigedia Jenerali Hassan Mabena, Mkuu wa Tawi la Utawala-Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), juma lililopita ulitangaza kuhusu mafuzo ya kujitolea ya JKT kwa vijana wa kitanzania. Ukawataka watanzania wazalendo wajitokeze na kujiunga na mafunzo hayo.
Vijana wenye sifa zitakiwazo walikusikia, wako tayari. Tayari kujiunga na mafunzo ya kujitolea ya JKT. Wanamiminika kwenye wilaya zao ambapo ulisema ndiko kutakaporatibiwa zoezi hilo. Vijana, kwenye wilaya zao, wanajibiwa kuwa matangazo bado hayajafika huko.
Brigedia Mabena, tafadhali fanya jambo, vijana wako tayari kujiunga na mafunzo ya kizalendo na yenye upendo kwa nchi yao Tanzania. Matangazo yatolewe, wenye vigezo wachukuliwe.
Sensa si siasa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwa sasa Dodoma)
Vijana wenye sifa zitakiwazo walikusikia, wako tayari. Tayari kujiunga na mafunzo ya kujitolea ya JKT. Wanamiminika kwenye wilaya zao ambapo ulisema ndiko kutakaporatibiwa zoezi hilo. Vijana, kwenye wilaya zao, wanajibiwa kuwa matangazo bado hayajafika huko.
Brigedia Mabena, tafadhali fanya jambo, vijana wako tayari kujiunga na mafunzo ya kizalendo na yenye upendo kwa nchi yao Tanzania. Matangazo yatolewe, wenye vigezo wachukuliwe.
Sensa si siasa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwa sasa Dodoma)