Bundle la Simu ku expire, mbunge ataka mlaji alindwe

Bundle la Simu ku expire, mbunge ataka mlaji alindwe

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869




Mbunge Salome Makamba ametaka serikali kuwalinda wateja wa simu za mkononi ambao wanabanwa na mikataba isiyo ya usawa, kuwalazimisha kutumia salio za vifurishi huku walaji hao wakiwa hawana mtetezi wa kuuliza makampuni ya simu dhima na sababu ya kulazimisha walaji kutumia vifurushi vilivyosalia .

Mbunge huyo amesema suala la kulazimisha wateja kumalizia salio halipo ktk nchi zingine zilizoendelea na kutaka TCRA / Ombudsman yaani ofisi ya kushugulikia malalamiko ya wateja wa simu za mkononi Tanzania kuwanusuru na adha hiyo ya kuburuzwa kwa kisingizio mkataba unawabana walioingia wakati wateja hawana nguvu kupingana na makampuni hayo makubwa ya simu.
 
Hili jambo sijui ni kwa nini kila siku linaongelewa, lakini utekelezaji 0. Sababu ya ku expire kwa bundle imekaa kiwizi wizi sana.
 
Wapo kutupa mb 30 Kwa 500 ......... halafu zisiishe muda wake ..
 
Utashangaa Hakuna Jibu Mambo Yatabaki Kama Mwanzo
Nadhani Viongozi Wanapewa Bahasha
 
... ukitaka lisi-expaye hiyo option mbona ipo? Nenda na utaratibu wa muda wa maongezi badala ya bundle. Unapewa offer halafu unampangia masharti mtoaji!
 
Majibu ya waziri husika , Si ya kuridhisha - Na hana mpango wa kulifanyia kazi
 
Utashangaa Hakuna Jibu Mambo Yatabaki Kama Mwanzo
Nadhani Viongozi Wanapewa Bahasha
Watajibu pale ambapo na wenyewe wataona madhara, kama mtu ana mshahara wa milioni 5, anaweza kuiba mali ya umma bila kushtukiwa, mabilioni na mabilioni, kwa nn aongee. Hana sababu ya kuongea. Ni mwanafalsafa tu ndo anaweza kua true kwenye haya mambo. Ila viongozi wote ni wafanya biashara

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
JPM ingekuwa kitu cha dakika kushughrika na zuluma hii.
 
Expire date ya bundle masaa 24. Kama ni udhulumati huu umekubuhu.
 
Back
Top Bottom