Bunge la 12 na Katiba tuliyo nayo sasa uasisi wake hauna Tofauti , Waasisi walitukosea sana japo walikuwa na malengo mazuri

Bunge la 12 na Katiba tuliyo nayo sasa uasisi wake hauna Tofauti , Waasisi walitukosea sana japo walikuwa na malengo mazuri

Nehemia Kilave

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2022
Posts
1,414
Reaction score
3,118
Hayati Magufuli binafsi sina shaka na nia yake njema kwenye hili taifa na alionesha nia hiyo kwa mambo mazuri aliyofanya ndani ya muda mfupi .

Changamoto ni ile ile ya viongozi wa Afrika kuamini mawazo yao ni sahihi muda wote hivyo akaleta wabunge ambao hawatakuwa wanakwenda kinyume na anavyoamini ili mambo yaenda haraka akasahau kwamba kuna kifo .

Kwake yeye alikuwa na nia nzuri Changamoto ni kama ilivyotokea kaondoka kawaacha wabunge ambao ni wachache sana wenye sifa za kuwepo pale na wanafanya kile kile ambacho Hayati Magufuli alihitaji pasipo jali utashi wa yule aliye kileta kikubwa kiwe cha Serikali

Kwa hapa alitukosea sana na sawa katiba iliyopo inatoa mamlaka kubwa kwa Rais hivyo inafanya kila Rais aifurahie huku wananchi mkitegemea hekima na busara zake .

Kwa bunge hili na Katiba hii watanzania tumekosewa sana .

Nadhani ushauri kwa watanzania mnapenda kuwa viongozi siku mfikirie siku moja kutakuwa na kiongozi mwingine ambae atatumia maamuzi mliyo fanya au sheria mlizo ziweka .​
 
Bila ya kufumua katiba kuleta mpya yenye kuendana na wakati , kuweka independent organs sio mahakama kuwa chini ya organ fulani yenye mihimili iliyojikita chini, Bunge kuwa na bunge dogo lenye wabunge waliopataikana by merit na wasomi hatuhitaji mbunge asiyekuwa na masters tena isiwe ya fine arts. Hakuna maendeleo yatakayokuwa endelevu imagine waziri wa ujenzi na mbunge haoni tatizo mwendojasi inapojengwa chini ya kiwango au barabara ujue hakuna kitu hapo
 
Kwa Sasa bunge la Tanzania ni Bora tu likafutwa.halina tija.Ni kibaraka wa mhimili wa urais.limeshiliki kupitisha tozo kuwaumiza wananchi na faida za tozo hatuoni,limeshiriki kuuza maliasili zetu lakini faida ni zero.Bunge hili limetuaibisha sana wtz na limekuwa kama genge la wahuni na wavuta bangi.
 
Bila ya kufumua katiba kuleta mpya yenye kuendana na wakati , kuweka independent organs sio mahakama kuwa chini ya organ fulani yenye mihimili iliyojikita chini, Bunge kuwa na bunge dogo lenye wabunge waliopataikana by merit na wasomi hatuhitaji mbunge asiyekuwa na masters tena isiwe ya fine arts. Hakuna maendeleo yatakayokuwa endelevu imagine waziri wa ujenzi na mbunge haoni tatizo mwendojasi inapojengwa chini ya kiwango au barabara ujue hakuna kitu hapo
Katiba mpya muhimu sana
 
Back
Top Bottom