Watanzania wenzangu hebu tutafakari hili pamoja. Hoja yangu ni kuwa bunge letu kama chombo kilichoainishwa katika katiba yetu kama muhimili wa wananchi wenye dhamana ya kusimamia na kuishauri serikali kwa niaba ya wananchi. nasikitika kusema muhimili huu umeporwa na vyama vya siasa na kuufanya uwanja wao wa kuendeshea propaganda za kuimarisha vyama vyao.
bunge ni chombo ambacho tunakitegemea kiwe na umoja katika kusimamia serikali kwa maana tunategemea bungeni tuone pande mbili tu. yaani bunge upande mmoja wakiwa kama bodi ya kusimamia kampuni na serikali upande wa pili ikija na hoja za mikakati inayotaka kutekeleza.
kitendo cha kugawa bunge letu ki vyama linadhoofisha bunge na kulipotosha bunge kwani hoja za vyama ndio zinapewa kipaumbele. hoja inaungwa mkono au kupingwa kutokana na imetolewa na upande gani? sasa kwa staili hii kweli kwa nini tusiseme kuwa utaratibu tuliojiwekea unalipotosha bunge letu.
Hivi kweli ukiwa na bodi ya kusimamia kampuni iliyogawanyika inaweza kuwa na ufanisi kweli? Ni madhambi mangapi ambayo bunge linayanyamazia kisa bunge limegawanyika ki vyama, ni mara ngapi tumeona kambi moja ikiweka msimamo maovu fulani yakemewe lakini kambi ya walio wengi ikipuuza, rasimali za taifa zinaporwa na wizi huo ukihalalishwa? ni wakati wa kutafakari ni wapi tulipokosea.
Suluhisho hapa ni kurejesha utawala kwa wananchi, na wananchi kwa umoja wao mhimili wao ni bunge hivyo ili kurejesha utwala kwa wananchi ni kurudisha bunge kuwa mhimili wa wananchi kutoka kwa vyama vya siasa vilivyopora mhimili huu. hii itafanyika kwa kila mbunge anayeingia bungeni kwa tiketi ya chama, anapoingia bungeni chama chake kinabaki mlangoni, mbunge awe ni mwakilishi mkazi wa eneo husika mda wote akifanya kazi katika ofisi ya mbunge jimboni kwake, kazi yake ni kufuatilia miradi ya maendeleo iliyopitishwa utekelezaji wake, kusikiliza matatizo ya wananchi na bungeni anakuja akiwa na takwimu alizokusanya jimboni kwake na huo ndio mjadala wa bunge.
mbunge awe full time mbunge na hapa tutakuwa tumetenga siasa na biashara kwa kiwango fulani. tunataka bunge liwe kitu kimoja katika kutetea wananchi. mojadala ya vyama irudi TCD
bunge ni chombo ambacho tunakitegemea kiwe na umoja katika kusimamia serikali kwa maana tunategemea bungeni tuone pande mbili tu. yaani bunge upande mmoja wakiwa kama bodi ya kusimamia kampuni na serikali upande wa pili ikija na hoja za mikakati inayotaka kutekeleza.
kitendo cha kugawa bunge letu ki vyama linadhoofisha bunge na kulipotosha bunge kwani hoja za vyama ndio zinapewa kipaumbele. hoja inaungwa mkono au kupingwa kutokana na imetolewa na upande gani? sasa kwa staili hii kweli kwa nini tusiseme kuwa utaratibu tuliojiwekea unalipotosha bunge letu.
Hivi kweli ukiwa na bodi ya kusimamia kampuni iliyogawanyika inaweza kuwa na ufanisi kweli? Ni madhambi mangapi ambayo bunge linayanyamazia kisa bunge limegawanyika ki vyama, ni mara ngapi tumeona kambi moja ikiweka msimamo maovu fulani yakemewe lakini kambi ya walio wengi ikipuuza, rasimali za taifa zinaporwa na wizi huo ukihalalishwa? ni wakati wa kutafakari ni wapi tulipokosea.
Suluhisho hapa ni kurejesha utawala kwa wananchi, na wananchi kwa umoja wao mhimili wao ni bunge hivyo ili kurejesha utwala kwa wananchi ni kurudisha bunge kuwa mhimili wa wananchi kutoka kwa vyama vya siasa vilivyopora mhimili huu. hii itafanyika kwa kila mbunge anayeingia bungeni kwa tiketi ya chama, anapoingia bungeni chama chake kinabaki mlangoni, mbunge awe ni mwakilishi mkazi wa eneo husika mda wote akifanya kazi katika ofisi ya mbunge jimboni kwake, kazi yake ni kufuatilia miradi ya maendeleo iliyopitishwa utekelezaji wake, kusikiliza matatizo ya wananchi na bungeni anakuja akiwa na takwimu alizokusanya jimboni kwake na huo ndio mjadala wa bunge.
mbunge awe full time mbunge na hapa tutakuwa tumetenga siasa na biashara kwa kiwango fulani. tunataka bunge liwe kitu kimoja katika kutetea wananchi. mojadala ya vyama irudi TCD