Itakuwa si haki kwa serikali na TBC yetu, mali yetu tunayoilipia kodi kutokurusha bunge letu la kutunga katiba yetu (Wananchi). Katiba ni mali yetu si mali ya Serikali, CCM, CHADEMA, CUF, NCCR na vyama vingine.
Tunayo haki ya kusikiliza live kinachozungumzwa na kuona kama kweli wawakilishi wetu wanavyotuwakilisha, ili tujue wale wanaotetea yale ambayo tumewatuma.
Hapa inavyoonekana Serikali inataka kufichaficha ili itakapoibuka unaambiwa Serikali mbili imepita tuipigie kura, pasipo sisi wenye katiba bila kusikiliza au kuona kinachoendelea.
Wapenda nchi yao (Tanzania) wasio na vyama na wenye vyama tunawaomba kama kweli Serikali itazuia kurusha matangazo live tunawaomba msiendelee na bunge.
Waachieni hao CCM na wanaotaka katiba bila kutushirikisha sisi wenye katiba (Wananchi) waendelee na tutapambana nao kwenye kura ya kuipitisha na watakapokuja kwenye uchaguzi kuanzia mwaka huu na mwaka ujao.
Mfano mdogo tu jana kutotuhusiwa waandishi wa habari kuingia bungeni imesababisha/tumepata usumbufu wa kutopata habari za uhakika kutoka bungeni. Haki yetu (Wananchi) kuona/kusikiliza live toka tarehe 18/02/2014 hadi mwisho wa bunge, tunahaki ya kuona kila kitu kinachoendelea hata kama kuelekezana kanuni.
Tunayo haki ya kusikiliza live kinachozungumzwa na kuona kama kweli wawakilishi wetu wanavyotuwakilisha, ili tujue wale wanaotetea yale ambayo tumewatuma.
Hapa inavyoonekana Serikali inataka kufichaficha ili itakapoibuka unaambiwa Serikali mbili imepita tuipigie kura, pasipo sisi wenye katiba bila kusikiliza au kuona kinachoendelea.
Wapenda nchi yao (Tanzania) wasio na vyama na wenye vyama tunawaomba kama kweli Serikali itazuia kurusha matangazo live tunawaomba msiendelee na bunge.
Waachieni hao CCM na wanaotaka katiba bila kutushirikisha sisi wenye katiba (Wananchi) waendelee na tutapambana nao kwenye kura ya kuipitisha na watakapokuja kwenye uchaguzi kuanzia mwaka huu na mwaka ujao.
Mfano mdogo tu jana kutotuhusiwa waandishi wa habari kuingia bungeni imesababisha/tumepata usumbufu wa kutopata habari za uhakika kutoka bungeni. Haki yetu (Wananchi) kuona/kusikiliza live toka tarehe 18/02/2014 hadi mwisho wa bunge, tunahaki ya kuona kila kitu kinachoendelea hata kama kuelekezana kanuni.