Bunge la kipuuzi na upuuzi

Bunge la kipuuzi na upuuzi

EJM_

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
3,836
Reaction score
2,100
Tangu Bunge la awamu hii lianze, kumekuwa na wingu kubwa la upuuzi unaondelea kiasi cha kuanza kutia kichefuchefu. Siku hizi ni rahisi sana kubashiri nini kitatokea leo bungeni na si kama ilivyokuwa zamani. Ningefurahi sana kama madabiliko haya yangekuwa chanya kuelekea kwenye ubora lakini nachelea kusema kwamba badala yake limekuwa bunge la upuuzi, ujinga na utoto.

Kinachonikera zaidi ni kuona namna wabunge badala ya kujadili mambo muhimu juu ya mustakabali wa nchi yetu, bungeni sasa kumejaa utumbo, maneno ya mtaani, matusi, methali za khanga na ubabe wa kipuuzi kiasi cha kunifanya nijiulize kama kodi yangu ndio inawalipa wale watu pale ndani kufanya upuuzi ule wa kipuuzi. Ni kawaida sasa kuona hoja nyingi tena nyingine zenye maana kubwa kwa nchi yetu zikipingwa kwa itikadi ya vyama kwasababu tu zimetolewa na mtu kutoka upande mwingine (what the hell is this!!?)

Jamani lazima wabunge wetu mjue kwamba wananchi wa sasa sio wale wa mwaka ule, hawa wa sasa wanajua kuchuja na kupembua (tumejionea wenyewe kule Mtwara na Lindi) hebu tuweni serious la sivyo ipo siku wananchi hawa watawadai kodi zao zote mlizowahi kula kwa kwenda kufanya upuuzi ule mnaoufanya kule Bungeni.

"Bunge la kipuuzi hufanya mambo ya kipuuzi na watu wapuuzi"
 
M'Jr Bunge letu limekosa kiongozi shupavu wa kupambana na hoja na kuzibalance kila upande uweze kuridhika, kinachosumbua hapa si vyama ni itikadi ambayo kiti cha spika (SIO MTU) kimejiweka, Kiti kikiwa na itikadi fulani lazima mwenye mawazo tofauti na kiti wakinzane. Hoja za wabunge zingine ni nzuri sana ila kiti kinaona hazina maslai sababu haziko kwenye ilani ya chama ambacho kiti kimejiweka chenyewe (uvunjaji wa kanuni-kiti hakina chama wala itikadi), Kama ulivyosema tutawadai kodi zetu, mfano mzuri ni leo wameingia bungeni wamesign mahudhulio siku imeingia, wamekaa dakika kadhaa wakatibuana wakaamua kuondoka, ila ukiangalia kwenye malipo hii siku iko na wengine wanalalamika kuwa posho hazitoshi..Mtu mwenye nia dhabiti na Bunge letu asipambane na wabunge apambane na KITI kiwe na mtu safi, asiwe na mahaba na chama chochote, asiwe mfuasi wa kundi fulani, asiwe mpenda sifa, asiwe jeuri, asiwe Mungu mtu, asiwe mwenye upendeleo wa aina yoyote,.. Na wabunge wetu wawe watu makini, mfano jana sijui kama walitumia vizuri MIC walizopewa na wapiga kura, maana kila msemaji wa jana alikosea kwa njia moja au nyingine.. nashauri warudi nyuma hata kama ni kwenye vikao vya vyama vyao wajirudi waelezane ukweli.
 
mbona lawama zako za jumla sana?
Mkuu sikutaka kumnyooshea yoyote kidole kwasababu hayo yameshafanyika sana na hakuna lolote lililobadilika badala yake hali inazidi kuwa mbaya. Kuna wakati nahisi kuna idadi kubwa zaidi ya wabunge mule hawajui hata kwanini wako mule (Huenda wanahitaji kamati kama ile ya TFF ili kuchagua nani aende na nani hastahili) Kwasababu pamoja na kuwa na ma profesa na madokta na wataalm wa kutosha mule bado they are acting like kindergarten kids.
 
Mkuu sikutaka kumnyooshea yoyote kidole kwasababu hayo yameshafanyika sana na hakuna lolote lililobadilika badala yake hali inazidi kuwa mbaya. Kuna wakati nahisi kuna idadi kubwa zaidi ya wabunge mule hawajui hata kwanini wako mule (Huenda wanahitaji kamati kama ile ya TFF ili kuchagua nani aende na nani hastahili) Kwasababu pamoja na kuwa na ma profesa na madokta na wataalm wa kutosha mule bado they are acting like kindergarten kids.
Sawa lakini kutoa lawama za jumla ni wazi kuwa humgusi yeyote na humwajibishi yeyote. kwa lugha rahisi Bunge lote haliwezi kutoka hapo kwa lawama za jumla. Nani chanzo? Kikundi gani chanzo? Chama gani chanzo? Hapo ndipo uwajibikaji huanzia
 
Back
Top Bottom