Bunge la Marekani lamthibitisha Joe Biden kuwa Rais wa Marekani

Bunge la Marekani lamthibitisha Joe Biden kuwa Rais wa Marekani

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Baada ya kikao kilichochukua muda mrefu, hatimaye Bunge la Congress limemthibitisha Joe Biden kuwa Rais wa Marekani na Kamala Harris kuwa Makamu wa Rais kwa muhula unaotarajiwa kuanza rasmi Januari 20, 2021 kwa kura 306 dhidi ya Donald Trump aliyepata kura 232.

Hatua hii inaashiria kukamilika rasmi kwa uchaguzi wa Marekani na kuwahakikishia Biden na Harris kuapishwa hapo Januari 20, licha ya jitihada za Trump kuzuia kufanikiwa kwa tukio hilo.

Trump akubaliana na uamuzi wa bunge
Rais anayemaliza muda wake, Donald Trump ametoa kauli kuwa anakubaliana na uamuzi wa bunge licha ya kutokubaliana na matokeo ya uchaguzi huo, akiahidi kuwa kutakuwa na makabidhiano ya madaraka kwa njia ya amani hapo Januari 20.

Chanzo: Al Jazeera
 
Dah kweli watu wana democracy yani jamaa alishinda kura za majimbo na popular vote lakini bado anatakiwa tena kuthibitishwa na bunge kwa kupigiwa kura??
 
Dah kweli watu wana democracy yani jamaa alishinda kura za majimbo na popular vote lakini bado anatakiwa tena kuthibitishwa na bunge kwa kupigiwa kura??
Huko hakuna janja janja kama za Tanganyika.

Kura zinahesabiwa kwenye geto la ndugai mara paap kesho yake mtu kashaapishwa.

Huwezi hata kuelewa mchakato umeendaje. Janja janja na uswahili uswahili!
 
Ila Biden naye ni mtu mzima Sana I doubt his ability to make decisions, ukimsikiliza Sana, kwakweli kuna mapungufu Sana.

Anyways marekani wameamua.
 
Ila Biden naye ni mtu mzima Sana I doubt his ability to make decisions, ukimsikiliza Sana, kwakweli kuna mapungufu Sana.

Anyways marekani wameamua.
Sasa biden na trump kuna tofauti gani
 
Ila Biden naye ni mtu mzima Sana I doubt his ability to make decisions, ukimsikiliza Sana, kwakweli kuna mapungufu Sana.

Anyways marekani wameamua.
Nyuma yake yupo Obama na washauri wengine ile nchi hataongoza mwenyewe.

Hapa nyumbani tuna “Sipangiwi” ndo maana sometimes unaona mambo yanaenda ndivyo sivyo.
 
Dah kweli watu wana democracy yani jamaa alishinda kura za majimbo na popular vote lakini bado anatakiwa tena kuthibitishwa na bunge kwa kupigiwa kura??
Ujinga mtupu chukulia ameshinda kwa kura halafu wabunge akaota wachache bungeni jina likipelekwa anaerza piga chini chukulia mfano Tundu Lisu Angepata kura nyingi za uraisi miliki za Magufuli halafu wabunge akapata huyo mbunge mmoja wa Nkasi ubunge likajaa wa CCM wangempiga chini
 
Back
Top Bottom