Bunge letu ni Bunge la ovyo? Bunge linafanya Uhuni? Wabunge Wetu ni Wahuni? Tumshauri Spika naye aanze kuita Watu kwenye Kamati, au waachwe tu?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kama kawa kila nipatapo fursa, huja na makala zangu hizi za kwa maslahi ya taifa ambazo ziko kwa mfumo wa maswali, halafu majibu utayatoa mwenyewe wewe msomaji.

Maswali ya leo ni Bunge Letu ni Bunge la Hovyo? Bunge Letu Linafanya Uhuni? Wabunge Wetu ni Wahuni? Tumshauri Spika Aanze Kuita Watu Kwenye Kamati, au Waachwe Tuu?.

Maswali haya ni kufuatia mkutano wa jana na waandishi wa habari Bandari na DP World: Dkt. Slaa asema ni uuzaji wa Nchi. Adai Serikali iliyopo ina uhalali wa wasiwasi


Baada ya kuzisoma hizo hoja, kabla sijaandika, nikatafuta kwanza clips ili kujiridhisha ni kweli maneno haya ameyamtaka kweli?, maana fani ya uandishi wa habari siku hizi imevamiwa, kuna waandishi wa habari wa kila aina kuanzia comedians, wasanii, na waandishi wengine wa hovyo sana, usipokuwa makini, sometimes waandishi hawa wa habari wa hovyo hovyo, hawachelewi kukulisha maneno!, hivyo nikamsikiliza mwanzo mwisho na kujirishisha kuwa ni kweli maneno hayo ameyasema, na sio tuu ameyasema, bali pia ameyaandika kwanza kisha akaja kutusomea sisi waandishi wa habari.


Kabla sijaendelea, naomba kuwakuwakumbusha wasomaji wangu, tujifunze kutofautisha definite statements na maswali. Hakuna statement kwenye bandiko hili, ni bandiko la swali! Natoa angalizo hili kwasababu mimi mwenzenu nimeisha wahi kuitwa all the way from Dar to Dodoma, kufika kule nikaulizwa kwanini umetoa hii statement? Nikajibu hiyo sio statement ni swali! Hivyo hapa nasisitiza hili ni bandiko la swali sio bandiko la statement!

Dr. Slaa ameliita Bunge Letu ni Bunge la Hovyo, na kilichofanyika kuridhia IGA ni uhuni? Ndio maana nauliza waungwana humu, hiki alichokisema Dr. Slaa kinaukweli kuhusu Bunge letu ni Bunge la hovyo?. Kilichofanywa na Bunge letu kuridhia IGA ya DPW ni uhuni?. Wanaofanya uhuni ni wahuni, jee Wabunge wetu ni Wahuni?.

Bunge letu Tukufu haliwezi kudhalilishwa hivi tukanyama! Je, tumshauri Madam Spika aanze ule utaratibu kama wa mtangulizi wake kuita watu kwenye Kamati, watu wowote watakao toa kauli za kulidhalilisha Bunge, au waachwe tuu kwasababu wanatoa maoni yao kwa mujibu wa ibara ya 18 ya katiba kuhusu uhuru wa kutoa maoni?

Nashauri Daktari aitwe mbele ya Kamati!. Mimi nilipouliza tu, hili swali Je, Bunge letu tukufu linajipendekeza kwa Serikali? niliitwa Bungeni kuhojiwa na kamati!, sasa leo Bunge linaitwa la hovyo! na kilichofanyika ni uhuni!, mtu huyu hawezi kuachwa hivi hivi tuu au aitwe mbele ya kamati kuthibitisha kauli yake?

Na ikitokea asipoitwa, jee hii haitaaminisha alichosema ni kweli?, ndio maana nawauliza waungwana humu, jee ni kweli Bunge letu ni Bunge la hovyo? Jee ni kweli kilichofanyika kwa Bunge kuridhia hii IGA ya serikali yetu na Mwarabu wa Dubai ni uhuni? Mtu anayefanya uhuni ni muhuni, jee waheshimiwa wabunge wetu ni wahuni?

Paskali
Rejea za mtoa mada kuhusu Bunge
- Baadhi ya Wabunge ni Stupid!, Tanzania haina Demokrasia!, Bunge ni Rubber Stamp!- TBC, Watch Now!
 
Unamtengaje tulia ili yeye ahoji wakati naye ni mbunge ?

Even yourself uliipigia salute uuzaji huu wa bandari.

Yaani bandari zote, hati mabwawa, sijui kama huko kwetu nyumba ya Mungu kama imepona.

Tuseme ni msiba mkubwa.
 
Nakujibu kuwa wabunge wa CCM Ni wahuni au niseme hivi wabunge walioko Bungeni Ni wahuni na hawajitambui hata kidogo!

Wanajadilije kitu ambacho kimeshaandikwa kwamba kikitiwa saini hakitavunjwa, au kubadilika?
Na wakaletewa mzigo ulishatiwa sahihi tayari na wamwpewa siku moja ya kuchakata!
Ni wahuni bwana P!

Ila pia nimesoma andiko la Thadeus Ole Mushi, mama asipoangalia anahujumiwa as per urais wa 2025
 
Mzee unaogopa kuitwa tena kwenda kujieleza? Hivi unataka kusema Tanzania tuna bunge la wananchi kweli? Walichaguliwa na wananchi gani?

Maana kilichotokea 2020 hata mtoto mdogo anajua kilikuwa ni kitendo cha kihuni. Hivyo hata hao walioko ndani ya yale majengo, watakuwa ni wahuni tu.
 
Kwahiyo Pascal anamzidi umri Steven Wasira au Bulembo?
Wasira, ni Mwenyekiti wa Board hana mshahara. Uzoefu wake ni mkubwa kutoa ushauri

Pili, lini Wasira au Bulembo wame post au kutoa taarifa za kujipendekeza hata kama ni za uongo toka Samia awe Rais?
 
Wanabodi,

Kama kawa kila nipatapo fursa, huja na makala zangu hizi za kwa maslahi ya taifa ambazo ziko kwa mfumo wa maswali, halafu majibu utayatoa mwenyewe wewe msomaji.
 
Wale ni wahuni tu.Hata kuingia bungeni waliingia kihuni.Mambo mengi wanayosifia na kupongeza ndiyo ymefanya maisha yetu kuwa magumu. Sheria za hovyo kama zile za kutoa Kinga kwa viongozi wasiostahili Kinga,Sheria za Kodi na tozo zinazofanya maisha yetu kuwa magumu,sheria za mafao tofauti kwa wanasiasa na watumishi wa umma (kikotoo) haya yote ni mtu mbinafsi tu anaweza kupitisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…