Bunge Maalum la Katiba

bumba

Member
Joined
Feb 13, 2014
Posts
53
Reaction score
3
Naona Bungeni kwachafuka. Baada ya Mhe. Jaji Warioba kupewa nafasi ya kwasilisha Rasimu ya Katiba Wahe. Wabunge wameendelea kupiga kelele, kugonga gonga meza na hivyo kukawa hakuna amani na baadaye kikao cha Bunge kikaahairishwa na Mhe. Spika. Kwa kweli siyo jambo la kiungwana kwa Wahe. Wabunge kufanya vitendo visivyo na maadili mbele ya Watanzania.
 
Ulitaka wafenyeje wakati sheria inataka ahutubie raisi kwanza then warioba.wap wamepindisha xx tufanyeje zaidi ya hivyo
 

Kama kanuni ilisema wazi kuwa Rais ahutubie kwanza ndipo Warioba awasilishe rasimu ya katiba tayari kwa kujadiliwa? Je wewe huoni Wabunge walifanya kitu sahihi ? Kama warioba angewahutubia bunge leo basi nadhani angepaswa kushtakiwa kwa kuchukua madaraka ya Rais. Wabunge walipiga kelele kwa kuwa Warioba siyo Rais. Kama kwa Mwenyekiti wa bunge hili yeye anaona kuwa Warioba ni Rais hilo ni tatizo lake mwenyewe. Ila hata warioba alijua kabisa kuwa anaingia kwenye kosa kubwa na ndo maana ikabidi akae kimya wakati wabunge wanapiga kelele kuwa kanuni zifuatwe. Sitta amepotosha bunge lakini siyo wabunge wote walikubaliwa kupotoshwa na ndo maana nao walipiga kelele.
Nadhani Sita afahamu kuwa hili ni bunge la katiba na siyo bunge la bajeti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…