Buriani Amina Chifupa!

Status
Not open for further replies.
dr slaa awakilishe bungeni ? he'll be next, tufanye vitu with cautions jamani. !!. lets take caution while we ask for justice to be done, otherwise tusije tukawa tunaomboleza msiba mwingine.
 
Mie nilikuwa nafikiria Mafia Wapo italy tu kumbe hata............!!!!!!!!!!!??????????
namuombea dada yetu Amina Chifupa Kwa mwenyezi mungu subhanna huwa taalah amsamehe madhambi yake yote na ailaze roho yake mahala pema peponi Tutamkumbuka na hatasahaulika, kifo chake hakijasababisha kupungua nguvu au kasi ya kupiga vita madawa haramu ya kulevya ambayo yanaathiri Taifa bali ndio changa moto na atatokea mwengine ambaye ataendeleza alipoishia mhe Marehemu Amina, kama sio mimi sijui!!!???
Amin
 

Mwanakijiji,
All you have said is quite true....just that you have missed my point COMPLETELY. You might need to go over my post to get a sense of what I said.
 
Nimekusoma Kada ingawa mzee Mwanakijiji bado anatafakuruuuuuuuu...kuanzisha hiyo petition...
 
Watanzania tupo kwenye majonzi makubwa, familia ya amina inahitaji faraja kwa wakati huu. But ni lini tutaweza kusimama kidete na kusema na kutaka tupewe taarifa zilizo sahihi kuhusu vifo vyene utata kama hiki !!!!!!. mungu ailaze roho yake mahala pema peponi amen..
 
Mwanakijiji and the rest mnaotaka ufanyike uchunguzi;

Thats the family choice.

Also, rejea to my previous post. Medical records zinaonyesha huyu dada was diagnosed with ngoma. Thats the fact. Now, am family don't want that information to go public that is why they are not pushing for any sort of investigation. (U need to get out of Detroit man, u can't cover news in bongo if u are chilling in front of your PC in US), as matter of fact Amina was on some sort of anti-viral cocktail until lilivopigwa somo, it is your choice to believe in kisomo, but she willingly agreed on somo, and that was btn her and Medi.

Mina alipagawa kabisa, family waliamua kumtibu kienyeji and at one time ilibidi anyolewe nywele zote, they took her to Lugalo when it was late. CCM and Govt had nothing to do with her. U are not serious if u think Amina was a threat to Serikali and CCM. We are talking about AC guys.

Again, Mola amlaze anapostahili, she was a role model to so many young females out there. She died so young and that what pains me the most.
 

Nakubaliana na wewe MKK, lakini ukweli uko pale pale kwamba kwa sasa hivi hawa mabwana (Mpakanjia na Nchimbi) ni just culprits and not convicted yet. tusiwahukumu lakini tuwahisi tu kwa sasa! Uchunguzi huru utatueleza ukweli.
 
ninachoweza kusema ni kwamba, uchunguzi kwa kweli hautofanyika hata kidogo na hiyo naapa. hata ukifanyika labda miaka ya baadae ( which i doubt ). naomba kesho azikwe mapema katika usingizi wa milele, apumzike kwa amani na sio kutishwa na akina nchimbi, medi, ccm, uchaguzi n.k

sikilizeni wimbo wa kirk franklin unaoitwa imagine me halafu put that pic of amina chifupa in front of u huku ukisikiliza maneno ya wimbo kwa makini, unaweza ukalia !!
 

Selemani,

You didn't answer my questions after your previous post here

Threats do not come from the powerful only; even the powerless can be a threat depending on how much they know about the governement and the size of audience they command. Amina may have had both these weapons, and so she was a threat.
 
JK kaomboleza pia...

JK amlilia Amina Chifupa
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, ameeleza kupokea kwa mshituko mkubwa taarifa ya kifo mbunge wa CCM Viti Maalum, Amina Chifupa.
Taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari, ilisema kifo hicho kimetokea wakati usiotarajiwa, huku akihitajika, lakini vivyo hivyo alikuwa ameanza kuvuma kisiasa.
"Wengi tutamkubuka marehemu Amina Chifupa kwa mchango wake muhimu alioutoa bungeni na katika jamii hasa mongoni mwa vijana.
"Alikuwa hodari katika kujkenga hoja na kutetea maslahi ya vijana wenzake na taifa kwa ujumla. Alikuwa kijana msema kweli na jasiri katika kutoa maoni yake kwa jambo analoliona," alisema Rais Kikwete.
Huku akinukuu misemo mbalimbali ya kijamii, Rais Kikwete alieleza kusikitishwa kwake na kifo cha mbunge huyo katika umri wa ujana wake.
"Kwa hakika kifo chake kinawagusa na kuwasikitisha watu wengi nchini. Wabunge wamempoteza mbunge mwenzao kipenzi, CCM wamempoteza nyota yao.
"Familia yake imempoteza nyota yao. Familia yake imempoteza mtoto na ndugu wa karibu. Mwanawe amempoteza mama.
"Mzazi mwenzake amempoteza mzazi mwenziwe wa kusaidiana naye kulea mtoto wao mdogo. Jamii imempoteza mwana jamii mwema, mkarimu na mwenye moyo wa huruma," alisema Rais Kikwete.
Aliwahakikishia jamaa za karibu wa marehemu, huzuni hiyo haikuwa peke yao, bali ni ya wote wanaoguswa na kifo hicho, huku akisisitiza ni "Mapenzi ya Mungu."
Katika hatua nyingine, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), umetoa rambirambi kutokana na kifo hicho cha Amina.
Rambirambi za UVCCM zilizotolewa katika taarifa iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa Taifa, John Nchimbi, zilisema hawataweza kumsahau kutokana na uwakilishi wake hasa wa kutetea maslahi ya vijana nchini wakati wote.
"Amina alikuwa ni mchapakazi hodari, mkweli na ambaye siku zote alitetea masuala ya vijana, sifa ambayo ilimfanya apendwe na wengi," ilisema taarifa hiyo.
Nchimbi katika taarifa yake, alibainisha kwamba wakati wote wataendelea kukumbuka kwa utashi aliokuwa nao katika utumishi wa uwakilishi wa jamii katika chombo hicho cha kutunga sheria.
"Tunaungana na wabunge, familia, ndugu na jamaa za Amina Chifupa, kuomboleza kifo chake na tunamwomba Mwenyezi Mungu awape uvumilivu, nguvu na afya katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo," ilihitimisha taarifa hiyo.
Wakati huo huo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alisema chama hicho na yeye binafsi wameshitushwa na kifo cha Amina.
Walimsifu marehemu kama mtetezi wa jamii ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo Watanzania wamempoteza kiongozi shupavu.
"CUF - tunatoa pole kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Jakaya Kikwete, Spika Samuel Sitta, wabunge, ndugu na jamaa wa marehemu na tunaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi,” ilisema taarifa ya CUF, iliyotiwa saini na msemaji Mbaralah Maharagande.
Naye Mwadini Hassan, anaripoti kutoka Dodoma kuwa, Chama cha Mapinduzi kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa habari za kifo cha Mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa, na kusema namna ya kumuenzi ni kutetea na kuyasimamia yote aliyokuwa akiyatetea.
Kauli hiyo ya CCM ilitolewa hapa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, makao makuu ya chama.
Alisema, marehemu Amina alikuwa kiongozi imara katika kutetea hoja, na hasa kupambana na dawa za kulevya, ambapo alidiriki kueleza hadharani kuwa "hata kama ni mumewe au yeye mwenyewe anajihusisha na biashara ya dawa hizo, watajwe ili wafikishwe katika vyombo vya sheria."
Makamba alisema, Amina alichukia biashara ya dawa za kulevya, ambayo imekuwa chanzo cha kuwaharibu vijana wengi nchini, ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa.
Makamba alitaja eneo jingine ambalo marehemu alilisimamia imara kulitetea, ni la watoto wa mitaani na wanaoishi katika maisha magumu, ambapo licha ya yeye kujitolea kwa hali na mali kupambana na tatizo hilo, alikuwa mara kwa mara akiitaka serikali kuchukua hatua madhubuti kuwasaidia kwa kuwapatia makazi ili waondokane na hali zao.
Marehemu Amina alisema Makamba, aliwahi kulia alipowatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu, hali ambayo ilionyesha alikuwa akiumizwa na hali hiyo na aliahidi kujitahidi kuwasaidia.
"Namna nzuri ya kumuezi, ni kuyaendeleza aliyokuwa akiyasimamia na kuyatetea, na hasa kwa Umoja wa Vijana ambao alikuwa akiuwakilisha bungeni," alisema.

Source: UHURU
Hilo jina ni sahihi kwa mwenye cheo hicho? au wamekosea?
 
Mwanakijiji and the rest mnaotaka ufanyike uchunguzi;

Thats the family choice.

Not completely true... Amina alikuwa ni kiongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na utaona jeneza lake kufunikwa na Bendera ya Taifa letu. Hivyo mauti yake siyo suala la familia tu bali la chama na nchi yake. Kama serikali ikitaka uchunguzi ufanyike utafanyika hata kama familia hawataki! (soma hiyo habari nyingine hapo juu)

Also, rejea to my previous post. Medical records zinaonyesha huyu dada was diagnosed with ngoma. Thats the fact. Now, am family don't want that information to go public that is why they are not pushing for any sort of investigation.

Classic red herring! je alikufa kwa ngoma? Hata kama vyeti vyake vya hospitali vinaonesha aliwahi kugundulika ana kifafa, kimeo, typhoid n.k ni uchunguzi wa kisayansi unaoweza kuonesha ni NINI CHANZO CHA KIFO. Hata wewe mwenyewe hapo hujasema kuwa amekufa na ngoma. Kama watu wanajua alikuwa na ngoma (maneno yako si yangu) na ya kuwa hata familia inajua hivyo, so uchunguzi huru utahusiana vipi na hilo, kama siyo ngoma iliyomuua kwanini uchunguzi huru ulitaje hilo, tunachoangalia ni nini kilichomuua period. Kama ni ngoma, kwani atakuwa mtu wa kwanza kuondoka nao? So that to me is a non-issue.

(U need to get out of Detroit man, u can't cover news in bongo if u are chilling in front of your PC in US),

Umezungumza kwa kujiamini kweli as if you really know where I AM.. usiamini kila unachosikia!

as matter of fact Amina was on some sort of anti-viral cocktail until lilivopigwa somo, it is your choice to believe in kisomo, but she willingly agreed on somo, and that was btn her and Medi.

kisomo hiki kilifanyika lini na wapi? Kama Amina alianza kuumwa tarehe 8 (kwa maelezo ya baba yake mzazi) na kuachika ilijulikana tarehe 7. Na mawasiliano yote yalikatishwa siku hiyo ina maana kisomo lazima kiwe kimefanyika kati ya siku hizo mbili. Hata hivyo hilo haliwezekani kwani hadi tarehe 10 wakati Mohd amezungumza na Habari Leo hakuwa ameonana naye na yeye pia alitaka "Amina aachiliwe huru aendelee na mambo yake ya kisiasa" na ni yeye aliyesema siku hiyo kuwa jambo hili la wao kutalikiana lisikuzwe. Sasa wewe mwenzangu uliye Mikocheni tuambie hicho kisomo kilifanyika lini na wapi na Amina alikuwa na hali gani ya kiakili? (kabla ya kujibu angalia sentensi yako hapa chini) Kumbuka unazungumza na nani katika sakata hili.

Mina alipagawa kabisa,

Unataka kuuambia umma wa JF kuwa Amina alifanyiwa kisomo wakati akiwa amepagawa kabisa?



for once you are right! Amina hakuwa tishio kwa CCM au serikali. Alikuwa tishio kwa maslahi ya watu binafsi! Ni kina nani hao?

Again, Mola amlaze anapostahili, she was a role model to so many young females out there. She died so young and that what pains me the most.

Agreed.
 
Selemani,
Naomba unieleweshe kitu kimoja tu. Umetaja Somo na anti-viral coctail. Kwani huko kwenye somo kuna kitu gani ambacho kingeweza kusababisha reaction kwa anti-viral au dawa alizokuwa anameza?
 
Jasusi.. nilikuwa nimekuwa na uso wa huzuni tangu jana.. lakini maneno yako hapo yamenifanya nicheke hadi nimejisikia vibaya
 
Selemani,
Hivi wagonjwa wa ngoma hutibiwa Lugalo?

Halafu hata kama familia yake waliamua kumtibu nyumbani kwao ilikuwaje kuwepo na askari walinzi ambao walizuia watu kumtembelea AC?.

Pili hata alipokuwa Lugalo inasemekana alikuwa kafungwa kamba, macho yake hayana focus yaani utadhani Mwendawazimu!... ni mgoma gani hiyo inayomfikisha mtu hatua hiyo hali Afya yake kimwili haikuwa na udhoofu mkubwa!
JK mwenyewe kamtembelea marehemu jana tu kama vile ndio kumwaga marehemu.... saa tatu usiku mtoto kavuta!
Selemani, usijifanye wewe una data za Bongo hata kidogo, hiyo ngoma angeondoka pia Mpokanjia ama naye kuwa positive!.
Hii tabia ya Wabongo kubisha ili mradi awe tofauti na watu sijui imetoka wapi na ndio maana watu roho mbaya kishenzi!.
Ushirikiano uliokuwepo enzi zetu haupo tena kila mtu na mzigo wake. Roho mbaya hadi chooni.. duh! jamani nyie wabongo jaribuni kumwogopa Mungu.

Kila unapokwenda ni mchawi tu.... Wazee na vijana wameingia imani za Uchawi kiasi kwamba wapo radhi kuua ndugu na jamaa zao kwa mali. Wengine kuwatoa watoto zao kama Mhanga!...ati wakitegemea kufanikiwa maisha. uchawi umekuwa big deal Bongo, kiasi kwamba Sumu ya Panya imekuwa ni moja ya uchawi wa kamati za ufundi!.
Hakuna biashara, safari wala nyumba isiyojengwa bila uchawi!... jamani ama kweli Utandawazi na soko huria umekuja na Mengi!
 
Mi sifungamani na upande wowote ila naomba kukuelimisha Mkandara kuwa ngoma siku hizi kutibiwa ni popote, private kwa govt, hospital kwa health centre, kwa hiyo kutibiwa ngoma lugalo ni NORMAL.
Halafu kitu kingine, ngoma ina magonjwa nyemelezi kibao, mengine yana-affect brain eg cryptococcal meningitis, ama hata viral encephalitis yenyewe, mtu achanganyikiwa anakuwa kama wagonjwa wengine uliowazoea wa mental illness!
Na tatu, progression from HIV to AIDS ina-differ among watu mbalimbali, usitegemee mume na mke kufa wakati mmoja, at times kuna discordance, ambapo partner mmoja anakuwa positive mwingine negative!
 
Amina Chifupa: Fears of foul play in the air

DAY OF SORROW: The Chief Sheikh, Mufti Shaaban bin Simba, leads prayers for departed Member of Parliament Ms Amina Chifupa Mpakanjia at her parents� home in Mikocheni, Dar es Salaam yesterday. INSETS: (bottom right) Ms Chifupa in her heyday, (top left) husband Mohamed Mpakanjia and their young son Rahmanino.
-Death clouded in murky circumstances
THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THE mysterious death of Ms Amina Chifupa Mpakanjia, a youthful legislator who will be especially remembered for pushing the anti-drugs war in parliament, has ignited a raging controversy in the country with friends and supporters openly suggesting foul play.

Ms Chifupa, who was elected to represent the youth as a special seats legislator on a CCM ticket, died at around 8.45 pm on Tuesday night at the Lugalo Military Hospital in Dar es Salaam, where she had been admitted for several days.

Aged just 26, she had recently emerged as virtually a lone crusader against the spectre of drug trafficking in Tanzania, and ironically she passed away on the same day as the International Day against Drug Abuse and Illicit Drug Trafficking (June 26) was being observed both at the national level and on a global scale.

Her shocking death has now been complicated by widespread speculation that she may have been targeted by the same drug traffickers she once famously threatened in parliament to uncover.

Asked yesterday about the suspicions of foul play in her death, the Minister for Public Safety and Security, Bakari Mwapachu, said simply that it was premature to speculate on the actual cause of the death.

’’It’s too early to talk about that right now, since the family is still in mourning. I will consult with my aides later about the allegations of foul play,’’ Mwapachu told THISDAY.

The minister responsible for crime prevention matters acknowledged that he personally had also received reports of possible foul play in the death of the young MP, but stressed that law enforcers needed more time to look into the matter.

News that the MP had passed away started filtering in as early as Tuesday night and rapidly spread across the country via mobile phone text messages and other means of communication.

By yesterday morning, reports of Ms Chifupa’s death were virtually the talk of the town, dominating discussions everywhere from government office corridors to daladala bus conversations.

Although purely speculation at this stage, it is no secret that most of the talk about the legislator’s sudden demise appeared to centre around the possibility that she may have been poisoned by alleged drug barons as a way of silencing her.

Officially, the cause of her death was reported as a combination of malaria and diabetes, but almost everybody who heard that seemed to take it with a pinch of salt.

Ms Chifupa’s own estranged husband, Mohamed Mpakanjia, appeared to further fuel speculations of foul play when he said in a media interview that the cause of her death was also a source of mystery to immediate family members.

’’I don’t know what caused her death...Her blood sugar level was so high that even the doctors were amazed and actually told us that they had never before seen such a high blood sugar rate in a single human being,’’ Mpakanjia said in a live radio show monitored yesterday.

Even the late MP’s own father, Hamisi Chifupa, was adamant that his daughter was not diabetic - although doctors at the hospital ultimately blamed her death on high fever and diabetes.

’’The doctors at Lugalo Hospital fought hard to save her life, but unfortunately they didn’t succeed. On our side, it came as a surprise to all of us to hear that our daughter was diabetic,’’ said Mzee Chifupa, a retired army brigadier.

In Dodoma, members of parliament were in a sombre mood after the Speaker of the National Assembly, Samuel Sitta, confirmed the news of Ms Chifupa’s death immediately after the customary morning prayers at the start of yesterday’s session at around 9 am.

Sitta adjourned parliament shortly after confirming the news, and called an emergency meeting to deliberate on the matter.

In an unprecedented move, the National Assembly was adjourned for the whole day and the Speaker announced that he would be leading a delegation of more than 30 MPs from Dodoma to Dar es Salaam for the last rites, and later to Lupemba Village, Njombe District in Iringa Region for today’s funeral.

Thousands of people from all walks of life gathered at yesterday’s last rites in Dar es Salaam, including veteran politician Mzee Rashid Mfaume Kawawa, the Chief Sheikh, Mufti Shaaban Simba, and scores of other personalities.

The MP’s friends, who knew her simply as ’Amina’, were overcome with emotion and explained their shock at her sudden death.

’’Of all people, she didn’t deserve to die at this age,’’ said journalist Furaha Thonya, who introduced herself as one of the late Ms Chifupa’s friends.

According to Ms Thonya, Amina had high political ambitions, including contesting for the powerful post of national chairman of the CCM youth wing (VIJANA), as well as a seat on the ruling party’s national executive committee (NEC).

Despite the allegations of foul play, there has been no formal call so far from the late MP’s family for an official enquiry into her death. (See more photos on Page 4)
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…