Buriani Amina Chifupa!

Status
Not open for further replies.
Admin/invisible,

mbona kuna baadhi ya post hazionekani kwenye hii thread au zimekuwadeleted?
 
niliweka post zaidi ya tatu zinazotoa ushahidi wa talaka tatu katika uislam mbona sizioni? hata zile za mtumwitu pia hazipo na za kichunguu? ziko wapi hizo post
 
Barabara18,

Wajua kila kitu duniani kina chanya na hasi! Hivyo sio kila tutakalolisema litakubalika kuwa ni chanya au hasi kwa mtafsiri.

Tetesi za kuumwa hadi kufikia kifo cha mpendwa AC zilirindima humu JF, kuna waliokataa katukatu!

Leo twaambiwa SIMU YA MKONONI YA MEDI MPAKANJIA IMEIBIWA MSIBANI! Medi alishasema ile simu ina kumbukumbu na vielelezo ambavyo vingeweza tibua hii deal, mojawapo ni hizo meseji za pole kabla ya kifo! Hivyo hiyo simu haikuwa halali yake tena! Ndo kusema Medi alikosea kuyasema hayo hadharani kwani MAFIA akiwemo yeye mwenyewe ndanimo alikiuka "FIRST RULE OF THE DEAL"
 
medi bwaba crazy ..leo nimesoma wabunge waloenda kule iringa wanalalamika kitendo cha medi kuingilia protocal kwa kwenda kulalamika kwa mkuu wa wilaya kwa kuibiwa simu...kitendo ambacho lilisimamisha shughuli za mazishi kwa muda kadhaa...huku wageni wakiwemo wabunge ,wakuu wa mikoa ,wasubiri mkuu wa wilaya akiomba simu irudishwe..hii imewashangaza wabunge wengi akiwemo muheshimiwa makweta aliyehojiwa waliyesema kitendo kile ilibidi apime uzito kati ya msiba na simu...hasa kwa kuwa pale ni ukweni ina maana ni kama tusi kwa wakwe as if ameibiwa simu na wakwe ..
 
Simu hiyo ni muhimu mno kama ingepatikana humu!Kwani nina uhakika ingesaidia sana kujua Mchawi ni nani haswa!Kuna maswali mengi yangejibiwa kwa Ushahidi mkubwa!
 
BURIANI MWANANGU AMINA CHIFUPA: PRINCESS WA TANZANIA

Na Ummie-Mahfoudha Alley Hamid

Kifo hakina wakati, huruma wala subira, huja kwa saa na muda uliopangwa na mwenyewe Subhana wa Taala Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mwanaadamu hawezi kukipangua. Ya laiti ingelikuwa uwezekano huo upo, basi tungalipangua vifo vya wengi ambao ni vipenzi vyetu kikiwemo hichi cha juzi cha mbunge wa Viti Maalum CCM anaewawakilisha vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia.

Wa kale walisema chema hakidumu. Nimeuthibitisha ukweli wa usemi huu kwa kifo cha binti huyu. Marehemu Amina alikuwa na sifa zote za kupendeza. Alikuwa kijana, mrembo, mtanashati, mcheshi, msomi kwa kiasi chake na zaidi ya yote alikuwa mtu wa watu.

Si muda mrefu tangu nimjuwe Marehemu. Nilimsikia sauti yake wakati akiwa mtangazaji wa redio, na nikamjuwa kupitia magazeti na runinga. Nikaja kumjuwa baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa vijana kupitia chama tawala cha CCM. Kabla ya kumjuwa fika, nilikuwa najisemea ki moyo moyo, "Hmmmm, binti kama huyu mwenye sifa zote hizi, kweli atakuwa na uwezo wa kuongea na watu wa hali ya chini anaowawakilisha? Hivi huyu si anaringa na kujiona kuwa hakuna wa kumgusa?" Hakika dhana ni dhambi na kweli nilipata dhambi kwani nilivyomdhania ikawa ni tofauti na nilivyomjua. Ukweli nilijikumbuka mimi enzi zangu nilipokuwa natikisa na namna watu walivyokuwa wanaona najivuna

Nilimwmjuwa Amina kwa muda wa miaka chini ya miwili ya ubunge wake. Aliniita "mama" nikamwitika "mwanangu". Alikuwa ni mtu "Simpol" kwa lugha ya mjini. Alikuwa mchangamfu na pia alikuwa ni mtu mwenye sikio la kusikiliza watu na shida zao ingawa shida nyengine zilikuwa si rahisi kwake kuzitatua.

Umaarufu, ujana, urembo, wema wake ulimfanya alengwe shabaha na kila chombo cha habari, iwe kwa wema au utelezi alioufanya. Ujana wake ulimfanya awe au afanye mambo mengi ambayo yanafanywa na yalifanywa na wengi ambao walio na umri wake. Binaadamu tunasahau kuwa "ujana ni moshi" na mwishowe hupita tu. Tunasahau kuwa tumepitia hatua zote hizo na zaidi ya hizo katika ujana wetu.

Alifanya mambo ya kawaida ya ujana na urembo, alikuwa mlevi? Sikumfahamu hivyo, mvuta sigara au bangi? Sikumjuwa hivyo, mtumiaji wa madawa ya kulevya? Sikumuona na sidhani kama alikuwa hivyo. Lipi geni alilokuwa nalo Marehemu Amina hata kusakamwa na kudhalillishwa hadi kufikia kupoteza roho yake changa?

Tujiambie na tujiulize, hivi sisi tukiwa kama waandishi wa habari, ni lazima tuwe na habari mbaya (negative) ndio tuandike au ndio ziuzike? Hatuwezi kuwa na upande mzuri (positive) side of issues? Kwa nini muandishi wa habari mwenzetu anaeanza maisha na malengo yake awe ndio chanzo chetu cha habari mbovu zilizopo na zisizokuwepo? Vijarida vya udaku haviuziki bila ya kuwepo uwongo usokifuniko?

Nasema hivi kwa sababu nimesikitishwa na muandishi Eric Shigongo wa gazeti la IJUMAA ambalo slogan yake ni "We belong to God" yaani wao ni waja wa Mungu, na namna alivyomsakama mwana wa watu na kusahau hiyo slogan yake ya kuwa yeye ni mja wa Mungu na Marehemu Amina pia ni mja wa Mungu. Amemuekea makala spesheli ya kumdoboa na kumnazi'i kadmnas bila kimeme. Anamkashifu na kuashiria kuwa Marehemu amefika kumfata kwake na kujitakisha!

Shigongo amemkejeli Marehemu eti asijifananishe na Mhe. Migiro na Mhe. Meghji. Kwa nini iwe vibaya kuwa na malengo? Hata Waheshimiwa hao walimhusudu Margaret Thatcher, Golda Meyer, Bandaranaike, Madeline Albright, Indira Ghandi na Bi Titi hawa wakiwa wachache tu kati ya wengi. Hakuna aliezaliwa na ujuzi usio weza kufikiwa na wengine. Hakuna kati yetu aliejuwa tu bila kuiga au kuweka malengo. Amemkejeli kwa bezo eti hata nae awe katika NEC na awe Mwenyekiti UVCCM. Mbona huyu Mwenyekiti wa sasa nae ni mjumbe wa NEC? Kwa nini kilicho "Good for the goose" kisiwe "Good for the gander?" Au hii ni kwa sababu ya jinsia yake? Kwa Marehemu alijiwekea malengo kuwa "Even the Sky was not the limit" because there is Outer Space after the sky, and may be that is where she wanted to set the limit.

Nathubutu kusema kuwa nilivyomjuwa Marehemu kwa muda mfupi na tukawa karibu sana kiasi cha kuwa wiki haipiti bila kujuliana hali siamini kama alikwenda kwa Shigongo na kukaa kwa saa sita kupindukia usiku wa manane kwa lengo la kutumia ujanajike wake. Maalesh, na iwe kweli kenda kwa lengo hilo, kwani Marehemu Amina atakuwa wa kwanza kujitakisha? Eric Shigongo hajapata kutaka au kutakwa na mwanamke? Anasema alimshikisha Marehemu kitabu kitakatifu ili aape kama aliwahi kutakiwa na Shigongo, na Marehemu akakataa kukishika; jee Shigongo anajuwa sharia za Kiislamu na sababu zinazomfanya mwanamke wa Kiislamu kukataa kushika Mas-hafu kwa sababu na nyakati fulani fulani?

Shigongo ameendelea na makala zake za kashfa juu ya uhusiano wa Marehemu na Mheshimiwa mmoja bungeni, jee tumuite yey ni mtafiti wa habari za ndani za wabunge wote walio bungeni? Ni kweli anajuwa mahusiano binafsi ya baina wabunge wote au alimkandia Marehemu tu? Kama anazijuwa habari zote mbona asiziandike kwa mapana na marefu na akakazania za Marehemu tu? Mbona asitoe habari za kina za huyo mbunge wa kiume na kumuandama Marehemu peke yake? Wangereza wanasema "It takes two to tango and it takes two to quarrel". Au hii ni ile dhana ya mfumo dume uliotutawala kuwa mwanamke ndie anaefaa kuitwa M……a (siwezi kuliandika hili neno) na mwanamme anafaa uitwa "KIJOGOO". Kama kazi hii ni ya wawili, vipi iwe sifa kwa mmoja na kashfa kwa mwengine? Shigongo anaogopa mwanmme mwenziwe na akamuonea Marehemu. Au ana ajenda ya siri?

Nimemjuwa Marehemu Amina kwa muda mfupi, na nikajuwa ni mtu mkweli, muaminifu, mwenye ithibati, asiekwenda kinyume na kauli yake. Nasema hivi kwa uthibitisho kamili nilionao binafsi. Miezi michache nyuma alitowa kauli yake kwa mtu mmoja kwamba angempa msaada fulani. Baadhi ya watu hawakupenda Marehemu afanye vile na akawekwa kiti moto na majopo si mawili si matatu, ya watu wazito sana ili aende kinyume na kauli yake ile. Marehemu Amina aliwasikiliza, na baadae akawajibu kuwa hangeweza kwenda kinyume na kauli yake na kwamba kama alivyoahidi, atampa mtu yule msaada wake.

Hapa niliweza kuona tafauti baina ya Marehemu Amina na wanawake na wanaume wengine wengi, wakiwemo vijana kama yeye waliotokea huko Umoja wa vijana CCM, na wanawake na wanaume wakongwe waliokomaa waliotokea katika vilele vikubwa vya Chama. Tafauti ilikuwa wengi wao walitia ulimi puani na kwenda kinyume na walivyotamka, wengine wakawa washiriki wa kumuweka Marehemu kiti moto na kumtishia kuwa wangemfanyia hivi au vile.

Marehemu Alikuwa hamtishi mtu wala hatishiki au kutikisika. Alikuwa ni mtu ambae akishatoa kauli yake, basi hata ashuke malaika gani haibadili abadan. Aliweka msimamo wa kupiga vita madawa ya kulevya kwa nguvu zake zote, jambo ambalo lingemtetemesha mtu mkubwa na mwenye nguvu. Niliwahi kuongea nae na kumwambia "Mwanangu pole pole, wasije wakakudhuru!". Kauli aliyonijibu ni kuwa amejitolea nafsi yake katika ukweli na haki na chochote kitachomfika ni maktub na hakifutiki. Kweli kilichoandikwa hakifutiki.

Nikiacha hili nitakwenda kwenye utanashati wake ambao ulifika kumponza bungeni kwa kuambiwa na Mheshimiwa Spika atoke nje ya kikao aende akabadili kivazi kwani hakistahili bungeni. Bila kinyongo Marehemu alitoka na tabasamu na akaenda akafanya kama alivyoamriwa. Binafsi wakati huo mimi nilikuwa katika maeneo ya Bunge Dodoma. Kivazi kilichomponza hakikuwa cha uchi au kuvunja heshima, kilikuwa na kidokezo cha kofia ambapo kwa sharia za bungeni tulizorithi kwa wakoloni, kilipaswa kiendane na uvaaji wa gloves na ndipo kiwe kimetimia. Marehemu Amina alitoka nje na akavua kofia ile na kurudi bungeni. Alifika hata kufanyiwa usaili na stesheni moja ya runinga na ilipoletwamada hiyo Marehemu alicheka na kusema kuwa hiyo ilikuwa ni changa-moto ya ukomavu wake na zaidi ya yote ilikuwa ni funzo la kupitia kanuni kabla kutenda jambo.

Wacha niwambie unafiki wa sisi watu. Kwenye runinga nimeona watu wanalia karibu ya kugaragara na kutiririkwa na machozi wakimsifia Marehemu. Jamani wengine katika hao ni wale ambao walichekelea Marehemu alipoamriwa kutoka nje kwa ajili ya kivazi chake, wengi ya hao walidiriki kumbeza na kusema kuwa pale ni pahala pa kazi na si pahala pa fashen na ubishoo. Wengi wetu ambao wakati umeshatupita kushoto na jua limekuchwa tulijisahau kuwa nasi kwa wakati wetu tulipiga vimini na kutesa mjini. Wengi ya wale ambao bado ni vijana walijawa na wivu wa kutomiliki vivazi vya "designer goods" vya Marehemu Amina, au ki maumbile kutopendeza kama yeye. Wivu na choyo vilitutawala na tukasahau kuwa "kila ndege anaruka na ubawa wake na nyota ya mwenzio usiisafiire".

Kila mtu ana mapungufu yake. Kwa sasa, ilivyo khulka ya binaadamu, utasikia sifa tu atakazo mwagiwa Marehemmu Amina. Kashfa zitatulia kwa wengi wetu kwa ile dhana ya "Never speak evil of the dead". Bwana Shigongo alisema katika makala yake ya Ijumaa iliopita kuwa anasitisha kuandika mengine kemkem ya Marehemu Amina na kashfa zake kwa vile ni mgonjwa kitandani. Aliahidi kuwa atatuletea uhondo huo baada ya kupona Marehemu Amina. Naomba nimnukuu marehemu bibi yangu ambae alikuwa ndio mentor (muongozi au dira) wangu. Alipokuwa katika "sakarati-l-mauti" nilikuwa namsomea na kumuombea dua huku nikilia na kumwambia "Bibi utapona". Alinitupia macho akanijibu "Nikipona nimepona, nikifa nimepona". Nami namuomba bwana Shigongo aliemsakama Marehemu hata wakati alipokuwa mgonjwa mahtuti kitandani, asitunyime conclusion ya uhondo wa hadithi yake tamu maana sasa Mhe. Amina AMEPONA na ni rukhsa kwake kutumalizia makala yake na asituache na shauku na duku duku la kutaka kujuwa kulikoni.

Kwa makala hii namuombea marehemu Amina malazi pema peponi, Mungu amsamehe madhambi yake, ampe kauli thabit, ampe kitaabu chake kwa mkono wa kulia, malaika wema wawe marafiki na wapokezi wake kaburini, apate nuru katika kaburi lake, liwe linatoa harufu ya rehani nasumini na mawaridi, awe mkono wa kulia wa Bwana Mtume siku ya Kiama pamoja na Ma-abrar wema, awape subira wazee wake, mwanawe, marafiki zake na kila aliempenda na aliependwa na Marehemu.

Marehemu Amina namfananisha na Princess Diana wa Uingereza alivyoandamwa na mapaparazi wa ulaya hadi akato(ka)lewa roho yake. Wema, Utanashati,ukarimu, ukweli, huruma, usaidizi na mengi mazuri ya Princess Diana yanafanana na yale ya Mrehemu wetu. Vifo vyao vinatafautiana mazingira lakini vinafanana sababu nazo ni kuandamwa kwa hili na lile. Tarehe pia zinapishana kidogo kama mwezi tu kufikisha miaka kumi kamili.

Diana alikuwa ni Princess wa Uingereza ambae ana andamwa hadi leo miaka 10 baada ya kifo chake. Marehemu Amina ni Princess wetu Tanzania. Natumai Paparazzi wenzangu tutakuwa na hishma za Ki Afrika na utu wa Ki Tanzania na tutamwacha marehemu apumzike kwa amani baada ya kumpa Bwana Shigongo nafasi ya mwisho ya kutueleza yaliyobaki juu ya Marehemu Amina. Baada ya hapo tutamwachia Mungu atamhukumu kwa amali zake nzuri, na zikiwa mbaya atamsamehe.

Naomba kumaliza kwa kunukuu maneno ya Jesus Christ alipowambia Mayahudi walipokuwa wanataka kumpiga mawe Mary Magdalene kwa sabau eti alikuwa mzinzi. Jesus aliwaambi hivi: "Let that among you with no sin cast the first stone". Yaani naanze kati yenu yule asie na dhambi kutupa jiwe la kwanza. Jee tupo kati yetu tulio malaika bila dhambi? Tukumbuke kuwa mtu akimyooshea mwenziwe kidole kimoja, basi vidole vine vinamgeukia yeye na kumsuta. Upo Bwana Shigongo?


Buriani mwanangu Princess Amina. Mungu akulaze pema peponi Amin.

Wakatabahu

Mahfoudha Alley Hamid
 
Nadhani simu ile ilikuwa na mambo mazito sana na ndiyo maana akaingilia mpango wa mazishi. Nadhani alitaka kupata umaarufu wa kutaka watu wajue alikuwa na simu au wajue alikuwepo msibani hilo anajua yeye. Huyu bwana ni kinara wa unga na kumbukumbu nyingi ziko katika simu ile kwa kweli aliyeichukua aipeleke polisi ili kazi ianze. Pia nilishangaa wakati akihojiwa na Clouds FM mtangazaji alitaka kujua jinsi taarifa za kifo cha Amina zilivyomfikia naye alisema hivi namnukuu "Asante ndugu mtangazaji kwa kweli ilikuwa saa kumi na moja mimi nilitoka pale hosipitali nikawa nimeenda kufuatilia gari gereji na ilipofika saa mbili nilipigiwa simu na mama mkwe akisema nahitajika kwa Daktari, nikaondoka moja kwa moja hado hospitali lakini sikuingia chumba cha Daktari nikaenda moja kwa moja hadi wodini nikakuta manesi wanaufunika mwili wa 'mke wangu' alikuwa tayari ameshafariki" Nilijisikia kuchefuka kwani Amina hakuwa mke wake. Pili hata mimi naungana na Waheshimiwa Wabunge kumshangaa mwili huu hapa wa aliyewahi kuwa mkeo wewe unaingiza mikono mfukoni ili uwapigie mafia wenzio kuwajulisha sasa ndiyo anazikwa ghafla unaona simu huna halafu unagwaya unapayuka 'nimeibiwa simu' ningekuwa ni mimi ningefyata mkia simu si lolote mbele ya kipenzi kwa kweli kuanzia mwisho wa maisha ya Amina huyu Mpaka njia aendelee kupaza njiani tu, hatapata mwanamke mzuri kama Amina Hamis Chifupa. Hii inadhihirisha kwamba umaarufu wa huyu bwana uliibuka baada ya kumuoa Amina sasa hana thamani tena mbele ya jamii. Alichokuwa akifanya katika sehemu mbali mbali iwe katika kumbi za starehe akawa anashangiliwa sana asidhani ni kwa ajili ya yeye kama yeye bali ajue ilikuwa ni kwa sababu ya yule Binti Amina H Chifupa na ndiyo maana hata vyombo makini vya habari vilikarabati jina lake vikafutilia mbali Mpakanjia. Msongo wa mawazo uliomkumba Amina hadi kupelekea kifo chake kuna neno zuri sana kwa lugha ya Kihehe na Kibena "Kwidzuma manga" Tatizo hili tiba yake ni tambiko tu kwa kiswahili ni msongo wa mawazo. Kutambika huko huenda sambasamba na mgonjwa kuwa karibu sana na wapendwa wake ili asijisikie upweke zaidi. Hata hivyo kwa kuwa wengi hatukujua nini kilichokuwa kinamsumbua lakini kwa umri wa Amina si rahisi kwa mtu wa kawaida kuamini kwamba Amina amefariki kwa kisukari na homa kali jambo ambalo nikweli kwani katika hali ya kuwa katika msongo wa mawazo mwili huwa dhaifu sana na baadhi ya organs huacha kufanya kazi kama inavyotakiwa na hii ndiyo iliyotokea kwake kwani amedevelop matatizo mengi ya kiafya kutokana na hilo. Kihehe/Kibena wanasema "Akidzumile manga" Tafadhali kutoka na hili mchawi wa matatizo haya ni huyu aliyewahi kuwa mume wake. Hana chembe ya huruma kwani kama ni kumtuhumu kwa kufanya ngono na Zitto mbona yeye pia ni mhuni tu? Je hakuna maandiko katika dini ya Kiislam yanayomtaka Mwisl;amu halisi asamehe mbona maandiko hayo yapo kwanini usingemsamehe Amina? Kwa huahiki kama ungemsamehe Amina ungekuwa umepata mwanamke bora maana angejirekebisha na kuwa bora kama utakavyo tatizo lingekuwa kwako Mpakanjia wewe nawe fuska vile vile. Kwanini ulimpa talaka mwenzio wakati na wewe kwa kutembea na wanawake nje ya ndoa ni mwenyewe swali umeacha wanawake wangapi ukampata Amina na baada ya Amina umetembea na wanawake wangapi. Mbona ulioa kabisa kule Kigamboni mkawa mnakanusha katika vyombo vya habari hadi yule mzee akawalaani wewe na binti yake. Mwisho nachukua fursa hii kuwapa pole wenzangu wote waliompenda Binti yule kwa juhudi zake katika kupambana na ufisadi hadi uhai wake ukapotea. Jambo lakushangaza katika kifo chake ni haya mambo manne.
1. Amefariki akiwa na umri wa miaka 26
2. Amefariki tarehe 26/6/2007
3. Alidhamiria kupambana na madawa ya kulevya
4. Amefariki siku ya kuadhimisha mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.
Kwangu mimi napenda kuungana na Rafiki yangu Martin Malera kwamba siku ya kuadhimisha mapambano dhidi ya madawa ya kulevya nitaiita Amina Chifupa Day. Si lazima kila kitu kitoke kwa wazungu ndipo tufuate hata sisi tunalojema linaloweza kufuatwa na wazungu. Amina Chifupa hakuwa mtu wa kawaida kwanza alikuwa ni Mh. Mbubnge hivyo ni kweli alidhamiria hilo kwani alikuwa ni mtu wa vitendo.
Mwisho kwa leo nawapa pole Baba na Mama Amina poleni sana kwa kuondokewa na binti yenu. Na tuzidi kumuombea kwa Mungu ili ailaze roho yake mahala pema peponi. Amina.
 
Bright flower that is no more

 
Waungwana,

Kuna email ina makala, nimeileta hapa, ila sina uhakika kama imeshawekwa hapa kwani hii thread imekuwa ndefu sana kuisoma yote. Labda tunaweza tukajifunza kitu hapa.

Muhingo Rweyemamu on Amina's death

Salaam wana Tumaini na wapenzi wa ukweli kote mliko. Tangu Amina alipofariki usiku wa juzi, mimi binafsi kama Mhariri wa gazeti la Rai, nimepokea simu na ujumbe mwingi wa simu. Nimepokea emails nyingi tu. Nimewasikia waheshimiwa, vijana kwa wazee wakiomboleza kifo chake. Wengine kama tunavyojua wanajaribu kwa kila wanavyoweza kutaka kubashiri kwa nini Amina kafariki katika umri huu mfupi. Mimi ninajiuliza tumejifunza nini kutokana na kifo cha mwanamapinduzi huyu? Jawabu ninalolipata, ni kwamba sisi ni wanafiki.

Wakati fulani, nilikuwa kuandika makala ya ukurasa mzima katika Rai nikisema: "WANAOMPENDA AMINA, WATAMLINDA." Kwanza wana Tumaini nataka niwaeleze kwamba Amina alikuwa rafiki yangu na mshauri wake. Siku alipopata matatizo ya kuanzisha urafiki na mume wa mtu mwaka 1999 wakati huo akiwa Tambaza kidato cha tano, mimi na aliposongwa na mashutumu na majaribu mengi, mimi na mwandishi mwenzangu, Absalom Kibanda, ndiye tulimpa ushauri wa kuwaambia walimu wake. Tulimshauri akubali na awaeleze kuwa yule mwanaume alimuingia kwa gia ya kutaka kumuoa. Akasema yeye kama Mwislam, hakuwa na kipingamizi. Amina alitoa sababu hizo shuleni, wakazikataa. Akaenda shule ya private ya Makongo. Wakati tunamshauri, alikuwa akifanya kazi ya utangazaji pale Clouds FM. Ofisi yake ilikuwa ghorofa ya tano ya jengo la Kitega Uchumi na mimi ofisi yangu ilikuwa ghorofa ya sita. Kwa hiyo tulikuwa karibu sana yeye na mwimbaji maarufu Lady Jaydee. Kipindi hicho, alionekana kijana anayeimudu fani yake katika umri mdogo. Absalom Kibanda alimfanyia interview na kuchapishwa kwenye jarida la Wiki Hii ambalo baadaye ndiyo liligeuka jina na kuitwa Mwananchi. Wakati huo nilikuwa Mhariri Mtendaji.

Katika siku za hivi karibuni, watu wenye malengo mengi, wamekuwa wakimtumia Amina. Wakati wa vita ya biashara ya dawa za kulevya hakuwa peke yake. Kuna kundi kubwa la wafanyabiashara mashuhuri lilikuwa nyuma yake. Kwa sababu yeye ni jasiri, walimpatia orodha ndefu sana aipeleke kwenye mamlaka zinazohusika. Siku moja Rais Kikwete alitueleza kuwa kama angeamua kuishughulikia orodha hiyo, hakuna watu wangeshikana uchawi. Anasema kwamba baadaye, iligundulika kwamba majina mengi kwenye orodha hiyo, yaliwekwa si kwa sababu ni wafanyabiashara ya dawa za kulevya. Hakufafanua zaidi lakini wengi tulijua kwamba ni vita za kibishara zinazotembea katika nchi zote zilizoamua kuukumbatia ubepari.

Kasi ya Amina ilinitisha, kama mhariri na kama rafiki yake. Nilimwita tukazungumza naye. Akaniambia kwamba hiyo ndiyo njia aliyoamua kupandia kisiasa. Niliamua kukubaliana naye lakini nikamwambia achukue tahadhari. Nilimwambia kwamba Morocco ni nchi ya kwanza kulima bangi duniani. Shamba kubwa la bangi mjini Rabat liko upande wa kulia wa njia inayokwenda uwanja wa ndege wa nchi hiyo. Bangi imepigwa marufuku nchini Morocco lakini hakuna kiongozi yeyote wa kisiasa anayekubali kuzungumzia shamba hilo la bangi wakati wakienda uwanja wa ndege kuwachukua wageni wao au hata wakisafiri. Nilimuonya kama ni ajenda yake, aende nayo taratibu, kama siyo yake, awaachie wenye nayo. Hakukubali wala kukanusha kwamba kuna watu wanataka kupandia mgongoni mwake.

Niliamua kuandika makala ya kuwaonya wale wanaomtumia (kwa sababu nilikuwa na habari zao kamili). Amina akapunguza kuwa public, akaamua kuifanya kazi hiyo kisayansi kwa kushirikiana na polisi chini kwa chini kama alivyosema Tibaigana.

Sasa likafuata hili suala la ndoa yake na wanasiasa walioingilia kati. Hilo jambo lilikuja kwa kasi sana . Yeye wakati huo alikuwa na ambition ya kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM. Akaenda kumwomba mwenyekiti wa sasa amuunge mkono. Kwa bahati mbaya kwake Amina, Mwenyekiti huyo akakataa kwa kumwambia point blank kwamba hatamuunga mkono. Kwa bahati mbaya tena, mwenyekiti huyo alikuwa rafiki mkubwa wa mume wake. Mume wake tayari alikuwa akimhisi kufanya mapenzi na Zitto Kabwe. Amina akachanganya mambo, akadhani Mwenyekiti wa UVCCM, ndiye amemchongea kwa mume wake. Ikafuata talaka. Amina akaahidi kwenda kwenye vyombo vya habari pale Maelezo kuanika yote. Yaani kutoa dukuduku lake. Kwa bahati mbaya, wakati vyombo vyote vya kitaifa na kimataifa vikimsubiri pale, baba yake ndiye akatokea. Kwa hiyo Amina akabaki na fundo lake. (wale walioko Tumaini chuoni wanaochukua shahada ya Councelling au walimu wao wanaweza kutueleza hapa). Kilichotokea ni depression. kwa walimu wetu wa councelling nadhani watakubaliana nami kwamba depression can disrupt, disable, and kill.

In terms of human suffering, the consequences of untreated depression are beyond measure. They include loss of self-esteem, family and career disruption, chronic disability and, in many cases, death. Suicide, is the outcome of depression. Kwa wale wanaojua siku za mwisho za Amina, watakubaliana nami kwamba kilichomuua ni depression.

Wataalam wanatueleza kwamba depression inaweza kuua sawa na ugonjwa wa moyo au magonjwa mengine. Kwa mfano Dr. Joseph Gallo, wa Chuo Kikuu cha Pennsylvania katika jarida la kitabibu nchini Marekani linalojulikana kama Geriatric Psychiatry, anasema kuna uwezekano kwamba depression inaingilia mfumo wa moyo pamoja na kushambulia immunity system ya mwili. Hivi ndivyo anavyosema:

"How depression increases death rates is not clear," said Dr. Joseph Gallo. "Possibly depression makes people less likely to take care of themselves, or acts directly on the immune system in ways we do not completely understand."

Kosa kubwa alilolifanya baba yake Amina, ni kumzuia kwenda kuzungumza na waandishi wa habari. Kwa yeyote anayejua mambo haya, atakubaliana nami kwamba Amina alianza kufa siku aliyozuiliwa kukutana na waandishi wa habari. Kwa sababu tangu siku hiyo, alianza kuwa recluse. Alianza kukataa kukutana na watu na tunaambiwa alifungiwa ndani, akaanza kujinyoa nywele, na wakati mwingine kuwasahau hata marafiki zake.

Kwa nini nasema sisi ni wanafiki? Nasema hivyo kwa sababu kulikuwa na uwezekano wa kuokoa maisha yake. Jamii haijajiandaa kuwasaidia vijana kutimiza malengo yao na kuvivuka vikwazo vya kimaisha. Amina amekuwa akipambana na mambo mengi ya maisha. Najua hivi kwa sababu ingalau najishughulisha na matatizo ya vijana. Wakati magazeti ya Shigongo yamemwandama kumchafulia jina, jamii ilikaa kimya. Amina akawa analia wakati akiwa chumba cha habari cha Clouds, watu wanasema shangingi huyo. Leo ni wale wale wanaomsifu na kumwagia sifa. Napenda kumaliza kwa kusema Amina hajafa. Waliokufa ni sisi tunaodhani tuko hai. Sisi wanafiki wa kupeleka maua kwenye majeneza wakati tungeweza kutoa maua hayo kukamilisha azma yake ya masha. Aliyekufa ni mwenyekiti wa CCM na Katibu Mkuu wake waliokataa kusuluhisha mgogoro wake wakidai ni wa kifamilia. Aliyekufa ni Spika wa Bunge aliyesema mambo ya Zitto na Amina hayalihusu bunge lakini sasa wanatoa ndege ya serikali kwenda kwenye mazishi. Aliyekufa ni mtuhumiwa Zitto Kabwe ambaye pamoja na kuendelea kukataa hadharani, alikuwa akiendelea kuwasiliana naye kwenye simu. Aliyekufa ni Shigongo na magazeti yake ambayo hata baada ya kufariki, waliendelea kuandama maiti yake kwa kutumia vyombo vyake vya habari. Amina hajafa na ndiyo sababu amepumzika siku ya kupiga vita dawa za kulevya; njia aliyoichagua kumjenga kisiasa.

muhingo
 

Kidogo kidogo ukweli unaanza kudhihiri....


Msondo ngoma... mambo HADHARANI...
 
baba yake marehemu chifupa kwa mara nyingine jana alitinga ukumbi wa habari maelezo jijini dar na kusema kuwa chanzo cha kifo cha mwanaye ni uchawi na kisukari habari kamili hapa chini


http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=3232
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…